Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Jana Jumapili ilikuwa siku ya kazi kwa sisi wengine. Niliamua kupanda basi kwa usumbufu wa parking na si kuwa na safari nyingine zaidi ya kazi na kurudi nyumbani.
Kituoni nilikaa na mama mmoja aliyenizidie umri kidogo. Kilicho tufanya tuanze kuongea ni kijana aliyetuomba hela akapate kifungua kinywa. Tulijikuta tuna something in common. Huyu mtoto tunaeweza kumzaa asiende kazini wakati sisi mama zake tunasubiri bus kwenda kazini.
Baada ya hapo nilipata shost tukaanza kusogoa. Shost aliniambia alikuja Dar miaka ya 1977-78. Ni mjomba wake alimuomba kwa wazazi wake. Baada ya kumaliza shule aliajiriwa na kupata nyumba ya National Housing ya vyumba viwili.
Kazini mkataba uliisha alilipwa kiinua mgongo na kuamua kujenga Guest House mkoani alikozaliwa. Guest ilikwisha na kuanza biashara.
Siku moja kanisani alikutana na mdada aliyeanza nae darasa la kwanza. Huyu dada ni mwalimu na amekuja Dar kumfuata mume wake. Wana watoto watatu lakini ndoa ina matatizo makubwa. Baada ya kubadilishana namba za simu mwalimu alimuomba msaada wa pango la nyumba ili ahame kwa mumewe.
Kwakuwa shost hakujaliwa kuwa na mtoto alimkaribisha mwalimu kwenye flat yake. Walijibana na watoto akimpa mwalimu muda wa kujipanga upya. Huku na huku akahisi anaibiwa pesa kwenye Guest House yake mkoani. Kwakua hana ajira mjini aliamua kwenda kusimamia biashara yake. Alimuacha mwalimu kwenye flat kwa makubaliano aiangalie.
Alikaa mkoani miaka miwili. Alikuja kugundua mzunguko wa pesa mkoani si kama Dar. Hakuna cha kuibiwa wala nini. Baada ya miaka miwili alirudi mjini akifikiria biashara ya mama ntilie mjini na vipesa vya Guest vitamsogeza.
Amerudi anakuta mwalimu amebadilisha mkataba na kuwa sasa yeye ndiye mpangaji halali wa NHC. Shost amepangisha chumba. Nilimpa pole sana.
Tenda Wema uwende, umdhaniae ndiye.
Kituoni nilikaa na mama mmoja aliyenizidie umri kidogo. Kilicho tufanya tuanze kuongea ni kijana aliyetuomba hela akapate kifungua kinywa. Tulijikuta tuna something in common. Huyu mtoto tunaeweza kumzaa asiende kazini wakati sisi mama zake tunasubiri bus kwenda kazini.
Baada ya hapo nilipata shost tukaanza kusogoa. Shost aliniambia alikuja Dar miaka ya 1977-78. Ni mjomba wake alimuomba kwa wazazi wake. Baada ya kumaliza shule aliajiriwa na kupata nyumba ya National Housing ya vyumba viwili.
Kazini mkataba uliisha alilipwa kiinua mgongo na kuamua kujenga Guest House mkoani alikozaliwa. Guest ilikwisha na kuanza biashara.
Siku moja kanisani alikutana na mdada aliyeanza nae darasa la kwanza. Huyu dada ni mwalimu na amekuja Dar kumfuata mume wake. Wana watoto watatu lakini ndoa ina matatizo makubwa. Baada ya kubadilishana namba za simu mwalimu alimuomba msaada wa pango la nyumba ili ahame kwa mumewe.
Kwakuwa shost hakujaliwa kuwa na mtoto alimkaribisha mwalimu kwenye flat yake. Walijibana na watoto akimpa mwalimu muda wa kujipanga upya. Huku na huku akahisi anaibiwa pesa kwenye Guest House yake mkoani. Kwakua hana ajira mjini aliamua kwenda kusimamia biashara yake. Alimuacha mwalimu kwenye flat kwa makubaliano aiangalie.
Alikaa mkoani miaka miwili. Alikuja kugundua mzunguko wa pesa mkoani si kama Dar. Hakuna cha kuibiwa wala nini. Baada ya miaka miwili alirudi mjini akifikiria biashara ya mama ntilie mjini na vipesa vya Guest vitamsogeza.
Amerudi anakuta mwalimu amebadilisha mkataba na kuwa sasa yeye ndiye mpangaji halali wa NHC. Shost amepangisha chumba. Nilimpa pole sana.
Tenda Wema uwende, umdhaniae ndiye.