... Maendeleo ya waumini au dini ni ubunifu binafsi, wala si kutegemea nani yupo madarakani. Endeleeni kuitegemea siasa kufanya maendeleo ya dini, kama ambavyo mlipewa matumaini kwenye ilani ya CCM ya uchaguzi wa mwaka 2005. Sijui mwaka 2015 watawaahidi kitu gani, nasema endeleeni kuitegemea siasa na CCM kuwa itatimiza ahadi inazowapa kila uchaguzi unapokaribia! Nikikumbuka maneno ya JK alivyoruka kuwa sio yeye aliyeweka ahadi ya Mahakama ya Kadhi kwenye ilani ya CCM, nawaonea huruma wanaoendelea kujipa matumaini. Maybe 2015 tutapata muisilamu mwingine wa kumtegemea, au maybe JK ataongezewa muda wa kipindi cha tatu! Wenzenu wanapiga kazi kila idara za umma na private kwa kutumia taaluma zao, ninyi mnasubiri JK awateue, sasa sijui nafasi za kuteua ziko ngapi!