Rafiki wa kike wa mume wangu ananitesa

Rafiki wa kike wa mume wangu ananitesa

Mi ningekuwa nimeisha achana naye siku nyingi.Siwezi kuvumilia huo upuuzi.
 
Na wewe tafuta rafiki wa kiume na wewe uwe naye close hivyo hivyo!halafu uone na yeye atalichuliaje!

By the way mimi ni rafiki mzuri tu!
Wee ndo unamwingiza chaka mazima
 
Hilo picha limechezwa kitaalamu sana, yaani umefanywa Fala kiwango cha Drimulaina..

Hapo unaibiwa Live and Direct, Chukua hatua
 
Nimekuwa mfuatiliaji wa mikasa ya watu humu leo na mimi nikaona nilete jambo langu linalonitesa kwa muda mrefu ili nijue nini cha kufanya. Mimi ni binti niko ndani ya ndoa, wakati naolewa mume wangu alikua na rafiki yake wa kike ambaye wenyewe wanadai urafiki wao ni wa kawaida tu kwani wanajuana muda mrefu. sasa tatizo huu urafiki wao umekuwa kero kwangu yani ni ule urafiki uliopitiliza kiasi kwamba kilasiku nikiangalia kwenye cm ya Mr lazima nikute wamewasiliana hata mara 50 text ndo usiseme. Kila sehemu wanaenda wote na huyo binti yani kama kumbikumbi mimi niko chuo wakati mwingine nikiwa chuo nikirudi hom namkuta huyo binti na Mr sebuleni inamaana ana courage ya kuja kwangu mimi nikiwa sipo, mara nyingine weekend tuko nyumbani na Mr, binti anampigia Mr cm njoo nyumbani kwangu ule nimepika, mume naye kilasiku lazima aripoti nyumbani kwa binti, mara binti aje nyumbani kumpitia Mr amsindikize sehemu, wakati mwingine tumelala weekend asubuh saa 1 binti kapiga cm kwa mr unafanya nini amka twende kwa fulani {mshikaji wao} yani full tafrani hana adabu kabisa ila nilichogundua ni kua mr nae ndo anampa ujeuri coz kuna kipindi niligombana sana na huyu binti kuhusu tabia zake huwezi amini alinijibu kuwa mimi siwezi kuwatenganisha kamwe nikitaka nimwambie mume wangu ndio ampige yeye marufuku kua na ukaribu nae ila sio mimi. Jamani cm wanapigiana mpaka saa 6 usiku. wenyew wanadai wao ni marafiki wa kawaida tu na hakuna kinachoendelea. nimejaribu kuuvunja urafiki huo unaoniumiza nimeshindwa mimi wenyewe hawana hata habari. Je kuna urafiki wa aina hii kweli kati ya mwanamke na mwanaume tena mume wa mtu? kwanini kusiwe na mipaka jamani..Huyo mwanamke ni mjeuri hatari ukimwambia anakujibu kwa dharau sana, mume naye ndo kwanza hana habari nisaidieni jamani nifanyaje?
Nawewe tafuta rafiki wa kiume
 
Nimekuwa mfuatiliaji wa mikasa ya watu humu leo na mimi nikaona nilete jambo langu linalonitesa kwa muda mrefu ili nijue nini cha kufanya. Mimi ni binti niko ndani ya ndoa, wakati naolewa mume wangu alikua na rafiki yake wa kike ambaye wenyewe wanadai urafiki wao ni wa kawaida tu kwani wanajuana muda mrefu. sasa tatizo huu urafiki wao umekuwa kero kwangu yani ni ule urafiki uliopitiliza kiasi kwamba kilasiku nikiangalia kwenye cm ya Mr lazima nikute wamewasiliana hata mara 50 text ndo usiseme. Kila sehemu wanaenda wote na huyo binti yani kama kumbikumbi mimi niko chuo wakati mwingine nikiwa chuo nikirudi hom namkuta huyo binti na Mr sebuleni inamaana ana courage ya kuja kwangu mimi nikiwa sipo, mara nyingine weekend tuko nyumbani na Mr, binti anampigia Mr cm njoo nyumbani kwangu ule nimepika, mume naye kilasiku lazima aripoti nyumbani kwa binti, mara binti aje nyumbani kumpitia Mr amsindikize sehemu, wakati mwingine tumelala weekend asubuh saa 1 binti kapiga cm kwa mr unafanya nini amka twende kwa fulani {mshikaji wao} yani full tafrani hana adabu kabisa ila nilichogundua ni kua mr nae ndo anampa ujeuri coz kuna kipindi niligombana sana na huyu binti kuhusu tabia zake huwezi amini alinijibu kuwa mimi siwezi kuwatenganisha kamwe nikitaka nimwambie mume wangu ndio ampige yeye marufuku kua na ukaribu nae ila sio mimi. Jamani cm wanapigiana mpaka saa 6 usiku. wenyew wanadai wao ni marafiki wa kawaida tu na hakuna kinachoendelea. nimejaribu kuuvunja urafiki huo unaoniumiza nimeshindwa mimi wenyewe hawana hata habari. Je kuna urafiki wa aina hii kweli kati ya mwanamke na mwanaume tena mume wa mtu? kwanini kusiwe na mipaka jamani..Huyo mwanamke ni mjeuri hatari ukimwambia anakujibu kwa dharau sana, mume naye ndo kwanza hana habari nisaidieni jamani nifanyaje?
Kuumizwa ni jambo la kawaida kwa kila binadamu lakini kuendelea kuvumilia kuumizwa ni uamzi wako mwenyewe.
 
Hakuna urafiki wa simba na swala hata siku moja,,, na huwezi kutembelea mua kama mkongojo lazima utaitafuna tuu,,,, kifupi unaibiwa
 
Alikuwa Na urafiki kabla ata ajafunga ndoa Na wewe . Utamchagulia mpaka lini mumeo marafiki ... Lipiza Basi nayeye aumie si 50/50 .. mpe limbwata awe zuzu Na akiwa zuzu yeye Na kizazi chake watoto wenu watakuwa masikini mbwa milele amini ... Dai talaka Basi ...ko kama nimefunga ndoa Na ww nisiambatane Na rafiki zangu ... Kunywa sumu Basi ...jichome kisu Basi

Rafiki mwenyewe atakua ndo wewe
 
Bi dada jifunze mumeo anapenda nini umkeep nacho busy akose muda na bestbyake mdoho mdogo wataachana, kiufupi yakupasa ujifunze kwa huyo dada ana nini mumeo anachokipenda na hakimchoshi. Japo ukweli mchungu ni kwamba mumeo anampenda huyo dada sema walianza kuwa marafiki akashindwa kupendeza mapenzi but deep down humwambii kitu.

Hauwezi kumkeep mtu busy kama hajaamua,

Mabadiliko ya mtu yapo ndani yake!
Nadhani umri nao unachangia a matured man wouldn't treat his lady like this
 
Sikia,
Changamka mama. Mwambie mumeo asiendekeze hiyo tabia...
Narudia, usimbembeleze, mchane live.

Sema leo, kesho itakuwa too late.

Achana na wanaoku-judge. Maumivu unaumia mwenyewe.
 
Hahahaa pole dada. Umenikumbusha mie nililetewa kabisa ndani tuishi nae tena bila taarifa. Nilipotaka binti aondoke nikaambiwa ntaondoka mimi binti ndo amefika na ole wangu nimguse au kumsumbua ntajuta kuzaliwa!!!
 
Alikuwa Na urafiki kabla ata ajafunga ndoa Na wewe . Utamchagulia mpaka lini mumeo marafiki ... Lipiza Basi nayeye aumie si 50/50 .. mpe limbwata awe zuzu Na akiwa zuzu yeye Na kizazi chake watoto wenu watakuwa masikini mbwa milele amini ... Dai talaka Basi ...ko kama nimefunga ndoa Na ww nisiambatane Na rafiki zangu ... Kunywa sumu Basi ...jichome kisu Basi
Bila shaka wewe ndo rafiki mwenyewe maana sio kwa povu hili
 
Back
Top Bottom