Hello, habari zenu wapendwa? Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nilikua na mchumba angu (sio mpenzi na hatukuwahi kukutana kimwili) ambaye tumedumu kwa miaka miwili, hatukuwahi kugombana wala sikumfanyia kosa lolote kwa mtazamo wangu, nilimjali kwa kila kitu hadi marafiki zake wakawa wanamwambia kwamba wangetamani na wachumba wao wawe kama mimi.
Nilimpenda kwa vitendo, nilijitoa sana kwake, and alijua kwamba kweli nampenda. Sasa miezi kama miez 5 ilopita, alianza kumfukuzia dada mmoja hv, nilipomuuliza alinijibu vibaya vibaya, nikamvumilia bila kupunguza upendo wangu kwake, lakini kadri siku zilivyoenda aliendelea kuwa karibu sana na dada yule. Niliamua kumuuliza yule dada kama ana mahusiano na mchumba angu, alikataa kabisa japo alikiri kwamba alitongozwa na mchumba angu.
Lakini kwa walivyokuwa karibu sana, ilionekana tayari wana mahusiano. Hivi juzi tu nilipomuuliza mchumba angu khs mipango yetu alinambia kwamba "kama bado ulikua na malengo na mm delete, siwezi kumsaliti (........)wangu" alitaja jina lake, jambo ambalo liliniuma sana. Sikulia sababu nilikua nishaona direction ya uhusiano wetu. Bas, nilikubaliana na matokeo sababu sipendi kumlazimisha mtu ktk mahusiano.
Sasa, kazi ipo hapa... Mmoja wa marafiki za x wangu walioujua uhusiano wetu vyema anataka anioe (kwa mujibu wake). Nimemuuliza maswali baadhi lakini kubwa likiwa "unawezaje kumuoa mtu ambaye kabisa unajua alikua ni wa rafiki yako wa karibu sana"?
Huyu kaka amenijibu kwamba CV yangu inajiuza, anapenda nilivyokua namtendea mchumba angu, na anataka anioe next year.
Hapa nimebaki dilemma, hivi kweli ni busara kuolewa na rafiki wa ex wako? Ktk moyo wangu sidhani kama nampenda maana bado nina mawazo sijatulia kias cha kuanzisha mahusiano tena. Nahitaji busara zenu wapendwa. Busara zenu pamoja na maombi nayofanya yatanipa mwisho mzuri.
Kwa wenye midomo iso tohara tusameheaneni tu. Hili halinisaidii tu mleta mada bali na wengine kama huyu mleta mada.