Radio Free Africa mna shida gani??

Radio Free Africa mna shida gani??

Ni wiki sasa nikifungulia radio yenu kusikiliza vipindi vya asubuhi vya magazeti na matukio nakutana na miziki na matangazo ya biashara tu. Kulikoni???
Tunasubiri kampeni zianze turuke mubashara na mgombea wetu
 
Transmitter zake za mikoani zimefifia sana mikoa mingine haisikiki tena
azam atampiku dialo, azam ana mredio wake unaitwa Ufm unakata mawimbi kukaribia mikoa ya kati, pia kuna viredio vya dini navyo vinakuja juu kwa usikivu mzuri nchi nzima
 
Radio Free Africa na Azam Tv ni mapacha wenye aleji na mvua, hivi vituo viwili havipatani na mvua kwani kukiwa na mvua matangazo yake hukatika. RFA magazeti husomwa toka Dar es Salaam Kinondoni huku wakiunganishwa na kituo kikuu cha kurusha matangazo kilichoko Mwanza lakini kukiwa na mvua mawasiliano hukatika na tatizo hili lipo tangu RFA ilipoanzishwa na kwa miaka yote wameshindwa kulitatua tatizo hilo vivyo hivyo na Azam Tv nayo mvua ikinyesha matangazo husikia baridi na kutetemeka! Nao tangu kituo kianze wameshindwa kulitatua tatizo hilo kutokana na vifaa wanavyotuuzia kuwa ni vya hali ya chini sana kiasi inawalazimu watumie gharama kuvifanyia matengenezo bure! Hii si bure kwani mwisho wa siku mteja unaambiwa ununue kingine ambacho nacho hakitadumu huku TBS( Mamlaka ya Viwango) ikiwagwaya.
Kwa hilo ni kweli ila nauliza hata kusoma magazeti kutoka Mwanza wameshindwa? Kujiunga na BBC asubuhi nayo wameshindwa?
 
Hii ndo Redio yangu bora kwa vipindi vya asubuhi hasa DW na Magazeti lakini hata mimi nashangaa wiki nzima wanaweka muziki tu mara matangazo yakate inakua kimya.

Dialo kama kashijdwa bora aiuze kwa Jambo.
Mimi pia redio yangu pendwa asubuhi. Namtafuta Dialo nimpe matangazo aweze kulipa wafanyakazi!
 
Jambo 106.9 fm Mwanza
Mapinduzi ya tasnia ya radio nchini Tanzania, kwa mwanzo huu naimani kubwa ya kuwarudisha watu katika kisikiliza redio kama ilivyokuwa miaka ya 90-2000 kupitia Jambo fm,, wamejipanga vizuri sana,, nawatakia kila lenye kheri kwao,,
Inasikika nchi nzima?
 
Jambo 106.9 fm Mwanza
Mapinduzi ya tasnia ya radio nchini Tanzania, kwa mwanzo huu naimani kubwa ya kuwarudisha watu katika kisikiliza redio kama ilivyokuwa miaka ya 90-2000 kupitia Jambo fm,, wamejipanga vizuri sana,, nawatakia kila lenye kheri kwao,,
Hiyo ni ya nani mkuu na imeanzishwa lini?
 
Radio ina wasikilizaji wa kutosha Nchi nzima sijui wanakwama wapi , very disappointing
 
azam atampiku dialo, azam ana mredio wake unaitwa Ufm unakata mawimbi kukaribia mikoa ya kati, pia kuna viredio vya dini navyo vinakuja juu kwa usikivu mzuri nchi nzima
Siyo redio ni redio, wana vipindi vizuri?
 
Ni wiki sasa nikifungulia radio yenu kusikiliza vipindi vya asubuhi vya magazeti na matukio nakutana na miziki na matangazo ya biashara tu. Kulikoni???
Alafu inapoteapotea hewani mara kwa mara
 
Back
Top Bottom