Kuna mambo mawili yaliyonifanya nisiwe nasikiliza clouds. Hapana mambo matatu.
1. Kipindi cha nyuma, nilikuwa msikilizaji mzuri sana wa njia panda. Nakumbuka hiyo jumapili mtangazaji alikuwa ana mhoji au anasoma barua ya mdada (sikumbuki vizuri). Huyo mdada alikuwa anasema ameambukizwa HIV na jamaa ambaye ni mfanyakazi wa ubalozi (sikumbuki ni nchi gani).
Alivyoelezea ni kwamba walikuwa na mahusiano na huyo jamaa, lakini akamwambukiza huyo mdada HIV makusudi. Kuna mdada mwingine alipiga simu studio wakati kipindi kinaendelea kutokana na maelezo yaliyotolewa, akasema anamfahamu huyo jamaa aliyemwambukiza mdada na akamtaja jina na na ubalozi anaofanya kazi.
Wakati haya yote yanaendelea, moyoni nikasema kama jamaa wa ubalozi ana mke, basi itakuwa imekula kwake. Lakini wakati kipindi kinaendelea huyo jamaa anayesemekana ameambukiza HIV, akapiga simu na kukanusha hiyo taarifa. Akasema alishaenda kupima na ikaonekana hana HIV.
Hiyo issue japo siikumbuki vizuri, sijui iliishia wapi. Lakini nilisikitika sana kwa chombo cha habari kupokea tuhuma kumhusu mtu, halafu hawahoji upande wa pili kupata ukweli.
Vipindi vya live, vina masharti yake na inatakiwa kama mtangazaji uwe maakini sana.
2. Kuna kipindi kilikuwa kinarushwa na mtangazaji wa kike usiku. Yule mdada akawa anatoa chance ya msikilizaji kupiga simu, na kumkumbuka mpenzi wake wa zamani na kuulizia yuko wapi na jinsi gani anamiss.
Hii ndiyo niliona utoto kabisa. Nikajiuliza, mume au mke akisikia mwenzake anakumbukwa na lijamaa atajisikiaje? ''kwamba nimeyamiss mahaba yetu ya zamani''. Nikasema huu ni utoto.
3. Matangazo muda wote na hasa vipindi vya asubuhi.