Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,509
- 16,734
Miongoni mwa miujiza ya Qur'an na kwamba ni kitabu chenye muongozo kwa wanadamu wote ni kule kutoonewa haya waarabu ambao kitabu hicho kimeteremshwa kwa lugha yao.
Kuonesha kuwa ni maneno ya Allah aliyeumba ulimwengu wote basi hata Mtume Muhammad rehma ziwe juu yake haikumoenea haya wala haikumpa fursa akaingiza lolote la kwake.Mfano maarrufu ni pale siku moja alipokuwa ameshughulika na kuwalingania matajiri na watu maarufu wa Makka ili waingie kwenye Uislamu.Muda huo huo akatokea maskini mmoja ambaye ni kipofu akaomba naye afahamishwe jambo.Mtume akakunja uso kuona anamkera katika muda muhimu wa kuzungumza na watukufu wa Makka.Sura nzima ikashuka kumkemea kwa kitendo chake hicho.Sura hiyo akaendelea kuisoma na alipokufa imebaki hivyo hivyo.
Mwanamke aliyetajwa ni mmbora ni mama yake Yesu as na wala mama yake mwenyewe wala mtoto wake wa kike kipenzi wala mke wake yeyote yule.
Qur'an kujulisha kuwa ni ya watu wote ina matamko mengi sana yanayowaita ENYI WATU kwa ajili ya wachina ,wajapani,wahindi na wote wengine ambao hawajinasibishi na vitabu kutoka kwa Allah.
Vile vile kwa ajili ya kuwaita kwenye uislamu ina matamko yanayowaita wakristo na mayahudi kuachana na upotovu na kufuata mafundisho ambayo yameboreshwa yaliyo kwenye uislamu.Matamko hayo ni kama vile ENYI WATU WA KITABU!
Upande wa waarabu wale waliokuwa kabla ya Mtume saw na wale alioishi nao hawakuachwa kutajwa kwa maovu waliyokuwa wakiyatenda.yote hayo ni kuonesha Qur'an ni kwa ajili ya muongozo kwa wote.
Waarabu walio hai miaka hii nao wamepewa vidonge vyao kwenye aya nyingi za Qur'an,baadhi yake ni kwenye surat Towba.Tuone aya mbili tu kati ya hizo, ya 19 na 20
Wale walio amini, na wakahama, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao, hao wana cheo kikubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hao ndio wenye kufuzu.20
Wanaodharauliwa hapo ni wale ambao wanaujenga msikiti wa Makka (Alkaaba) na kuuwekea teknolojia za kisasa kila mwaka na kuwakirimu vya kutosha mahujaji.Wanawapa maji ya zam zam mpaka mengine wanabeba makwao.Baada ya hapo wanaamini ndio wamemaliza ibada na kutenda wema katika dunia na wanabweteka kusubiri msimu ujao..
Wanaodharaulika ni wale ambao wanaojaza malori eneo la Rafah na wakawacha bidhaa ziharibike huku wanaohitaji na wanaokufa kwa njaa wapo mita chache tu kutoka hapo,
Wakudharauliwa na walimwengu wote ni wale wanaonunua silaha na kuzinduka kwenye maghala bila kuzitumia kupigana na yule anayeuwa ndugu zao masafa mafupi tu kuliko wanapoishi.Hao hao ambao wanatoa zawadi ya ndege na mapesa kwa yule anayeongoza kuua ndugu zao wa kiimani.
Kuonesha kuwa ni maneno ya Allah aliyeumba ulimwengu wote basi hata Mtume Muhammad rehma ziwe juu yake haikumoenea haya wala haikumpa fursa akaingiza lolote la kwake.Mfano maarrufu ni pale siku moja alipokuwa ameshughulika na kuwalingania matajiri na watu maarufu wa Makka ili waingie kwenye Uislamu.Muda huo huo akatokea maskini mmoja ambaye ni kipofu akaomba naye afahamishwe jambo.Mtume akakunja uso kuona anamkera katika muda muhimu wa kuzungumza na watukufu wa Makka.Sura nzima ikashuka kumkemea kwa kitendo chake hicho.Sura hiyo akaendelea kuisoma na alipokufa imebaki hivyo hivyo.
Mwanamke aliyetajwa ni mmbora ni mama yake Yesu as na wala mama yake mwenyewe wala mtoto wake wa kike kipenzi wala mke wake yeyote yule.
Qur'an kujulisha kuwa ni ya watu wote ina matamko mengi sana yanayowaita ENYI WATU kwa ajili ya wachina ,wajapani,wahindi na wote wengine ambao hawajinasibishi na vitabu kutoka kwa Allah.
Vile vile kwa ajili ya kuwaita kwenye uislamu ina matamko yanayowaita wakristo na mayahudi kuachana na upotovu na kufuata mafundisho ambayo yameboreshwa yaliyo kwenye uislamu.Matamko hayo ni kama vile ENYI WATU WA KITABU!
Upande wa waarabu wale waliokuwa kabla ya Mtume saw na wale alioishi nao hawakuachwa kutajwa kwa maovu waliyokuwa wakiyatenda.yote hayo ni kuonesha Qur'an ni kwa ajili ya muongozo kwa wote.
Waarabu walio hai miaka hii nao wamepewa vidonge vyao kwenye aya nyingi za Qur'an,baadhi yake ni kwenye surat Towba.Tuone aya mbili tu kati ya hizo, ya 19 na 20
أَجَعَلْتُمْ سِقَايَةَ الْحَاجِّ وَعِمَارَةَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ كَمَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَجَاهَدَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ۚ لَا يَسْتَوُونَ عِندَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
١٩﴾ الَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ أَعْظَمُ دَرَجَةً عِندَ اللَّهِ ۚ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَائِزُونَ ﴿
Je, mnafanya kuwanywesha maji Mahujaji na kuamirisha Msikiti Mtakatifu ni sawa na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu, na Siku ya Mwisho, na akapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu? Hawawi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu.19أَجَعَلْتُمْ سِقَايَةَ الْحَاجِّ وَعِمَارَةَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ كَمَنْ آمَنَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَجَاهَدَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ۚ لَا يَسْتَوُونَ عِندَ اللَّهِ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
١٩﴾ الَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ أَعْظَمُ دَرَجَةً عِندَ اللَّهِ ۚ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَائِزُونَ ﴿
Wale walio amini, na wakahama, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao, hao wana cheo kikubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Na hao ndio wenye kufuzu.20
Wanaodharauliwa hapo ni wale ambao wanaujenga msikiti wa Makka (Alkaaba) na kuuwekea teknolojia za kisasa kila mwaka na kuwakirimu vya kutosha mahujaji.Wanawapa maji ya zam zam mpaka mengine wanabeba makwao.Baada ya hapo wanaamini ndio wamemaliza ibada na kutenda wema katika dunia na wanabweteka kusubiri msimu ujao..
Wanaodharaulika ni wale ambao wanaojaza malori eneo la Rafah na wakawacha bidhaa ziharibike huku wanaohitaji na wanaokufa kwa njaa wapo mita chache tu kutoka hapo,
Wakudharauliwa na walimwengu wote ni wale wanaonunua silaha na kuzinduka kwenye maghala bila kuzitumia kupigana na yule anayeuwa ndugu zao masafa mafupi tu kuliko wanapoishi.Hao hao ambao wanatoa zawadi ya ndege na mapesa kwa yule anayeongoza kuua ndugu zao wa kiimani.