Pwani: Askari Wawili wa Usalama Barabarani wauawa kwa kupigwa risasi Kibiti

Duuu hii hali inatisha, Poleni sana wafiwa kwa masaibu hayo ambayo binadamu yoyote kwenye akili timamu na hofu ya Mungu hawezi tenda.

Nimefuatilia mijadala huku ndani maana nilikuwa sijui na najiuliza kwanini haya yatokee na ukimya na usiri mkubwa huu wa kutojulikana wahalifu? Kuna vitu Vingi sana vinatajwa na watu na wengine wanasema huenda serikali inajua ukweli wake ila haitaki kuusema maana ni kama msemo ule usemao, "Jini ulilifuga mwenyewe liwadhuru wengine sasa linakurudia"
Sasa swali LA kujiuliza kwanini hali hii mpaka sasa, je, ukweli kila siku kuhesabu idadi ya waliouawa ni sawa? Poleni sana sana Kibiti, Mkuranga & Rufiji. Je, haya yanayosemwa kuna ukweli wowote?
HYPOTHESIS zilizopo kwa mijadala ya humu ndani.
(1)Haya yanayotokea ni kutokana na dhuluma kwa wananchi kupigwa na kuteswa na viongozi wa huko kwa ishu za kiuchumi za mazao ya misitu, yasni Mbao, Mkaa, Kuni na kulima kwenye misitu hiyo, sasa baadae ya kuzuiwa wamekosa shughuli za kiuchumi hivyo hasira kurudi kwa viongozi wasimamizi wa maeneo hayo.
(2)Huenda yanatokana na kubanwa kupitisha nyara za serikali kama Magogo na Vipusa (pembe za ndovu), maana inasemekana kutokana na misitu ya huko sasa wale majangili ndo ilikuwa njia yao rahisi kupita, sasa wamebanwa na waneona warudishe hasira zao kwa hao wasimamizi?
(3)Huenda ni kutokana na nadharia ya kuwa mikoa ya kusini kusahaulika katika rasilimali za nchi, hawafaidiki kwa chochote na haya ishu ya bomba LA gesi na umeme kanda hiyo ilipata msukosuko sana, waliteswa na kupigwa walipotaka kuleta upinzani gesi isitoke kwanza kabla hawajafaidika. Maana ukweli tulisoma na kuona kwenye vyombo vya habari watu wa kanda hiyo kusumbuka, sasa huenda wameona ndo pakutolea hasira, sasa swali tena linakuja, hawa wanaouawa je, ndio wasimamizi wa hiyo gesi na umeme? Inabaki haieleweki.
(4)Huenda ni kutokana na siasa na utofauti na chuki tuuu bila kuwa na uhalisia. Hii nayo inaacha maswali kama ni chuki ya kisiasa, je kanda hiyo ndo wanajua siasa kulikoni maeneo mengine? Mbona maeneo mengi kuna mchanganyiko wa siasa lakini haya hayaonekani?
(5)Huenda ni mambo ya utofauti wa kiimani na nini, hili pia nalo linaacha maswali mengi, mbona maeneo mengi nchini yana mchanganyiko wa imani tifautitofauti na misimamo tofautitofauti mbona haya yanayotokea huko, huko kwingine hayapo? Au wa huko ndo kwenye imani na misimamo mikali tofauti na mahala pengine nchini?
(6)Huenda ni kutokana na tetesi na haya kipindi Fulani cha nyuma iliwahi kusemwasemwa na haya humu jamvini wengine wamewaza hivyo. Kulisemekana kuna makundi ya vijana walikuwa wanakusanywa na kusafitishwa nje ya nchi kufundishwa mambo mbalimbali, ila familia zao waliahidiwa kupewa hela na wao pia kulipwa kwa mafunzo hayo. Na inasemekana viongozi wa maeneo ya huko ndo walikuwa na tenda hiyo kukusanya vijana nao pia kufaidika kwa idadi ya aliowarecruit, sasa swali linakuja, makundi kama hayo serikali yetu na wanausalama wetu walilijua? Je, hatua gani zilichukuliwa? Je, hao vijana kwa makundi hayo wanajulikana? Na je, wapo wapi kwa sasa wanafanya nini? Je, viongozi waliohusika kufanya udahili huo wanajulikana?, wapo wapi? Na je, hayo mafunzo yalilenga nini? Nadhani hapa kunaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu kwa sisi RAIA, ila serikali na wanausalama lazima wanamajibu.
(7)Huenda ni ugaidi ndo unajijenga nchini, kama ilivyo BokoHaram, Alshaababy mmmh Mungu atuepushie hili, ila nalo linaacha maswali, hao magaidi woote huwa wsnalengo lao na huelezea nini wanataka ili waache dhuluma hiyo, sasa hawa mbona hakuna Maelezo yoyote? Au huenda Mimi ndo sijui, maana kwa kufuatilia media za habari sijaona lolote.

Sasa tuje Hypothesis nyingine hii ya uwezo wao wa kufanya matukio kila Mara na hawakamatwi. Hii inaonesha hao wafanyadhuluma wapo Trained na kwenye siri Kubwa sana, je, watu wa namna hiyo ni RAIA wa kawaida kweli? Je, wanaishi wapi na akina nani bila kujulikana? Je, wenyeji wa maeneo hayo hawana chochote cha kusema ili hili likomeshwe? Je, wananchi kwanini wawafiche wahalifu wanaowasababishia kula na kulala SAA 12jioni kila siku? Je, wanausalama wetu huko wanaushirikiano mzuri na wananchi ili wawape ya ndani wanayojua? Maana wakati mwingine RAIA wema huogopa kusema anachojua maana siri zake zitavuja na anajikuta yupo matatani kwa yule aliyetajwa kuhusika.
Kwa mantiki hii, haya maswali tukijiuliza kwa uzalendo na kuyapatia ufumbuzi unaweza saidia kutuliza na kumaliza tatizo. Binafsi bado ninaimani kwa vyombo vyetu vya usalama, wanaweredi wa kutosha. Na huenda haya niwazayo wanamajibu yao. Kila LA kheri kwa vyombo vyetu vya usalama, na Mungu atusimamie kama nchi kadhia hii iishe kabisa.
 
uSIWALAUMU polisi bila sababu ya msingi, kazi yao ni kutii maagizo ya viongozi wa kisiasa, serikali na mahakama. Hii ndivyo kazi ya polisi ilivyo duniani kote. Wako kama mbwa kutii amri ya boss. Tatizo sio polisi bali wanasiasa.
Hiyo Ni kweli mkuu
 
Hawa watakua nimagaidi, ili saga limeanza tangu 2015 kabla ya uchaguzi.
Kama watu watakumbuka mwaka jana kulitokea vurugu mapango ya amboni tanga nahii habari ilimake headlines sana kwenye magezet.
(1) Kibiti pwani; kuwepo kwa bahari namsitu mkubwa kunakufanya kibiti kuwe nisehem rahis zaid kwahawa watu kuingia nakutoka bila mtu kujua.
(2) wanachohitaji; jambo kubwa wanalolipenda hawa watu nikuonekana, mfano wastegate, london hakuna walichopata zaid yakupata airtime kwenye media
(3) watu wanaouliwa;
wameu viongozi wa vyama ili kupotosha serikali kua hili niswala lachuki za vyama, polis ilionekane watu wasioipenda serikali, nikutopoteza focus.

Serikali ilitizame hili kama ugaid naipambane nahili kwakufatilia technic zakupambana naugaidi kabla hatujachelewa
 
Hawa watakua nimagaidi, ili saga limeanza tangu 2015 kabla ya uchaguzi.
Kama watu watakumbuka mwaka jana kulitokea vurugu mapango ya amboni tanga nahii habari ilimake headlines sana kwenye magezet.
(1) Kibiti pwani; kuwepo kwa bahari namsitu mkubwa kunakufanya kibiti kuwe nisehem rahis zaid kwahawa watu kuingia nakutoka bila mtu kujua.
(2) wanachohitaji; jambo kubwa wanalolipenda hawa watu nikuonekana, mfano wastegate, london hakuna walichopata zaid yakupata airtime kwenye media
(3) watu wanaouliwa;
wameu viongozi wa vyama ili kupotosha serikali kua hili niswala lachuki za vyama, polis ilionekane watu wasioipenda serikali, nikutopoteza focus.

Serikali ilitizame hili kama ugaid naipambane nahili kwakufatilia technic zakupambana naugaidi kabla hatujachelewa
Watanzania wa kawaida hawana weledi Wala organization skills kuendesha Black ops kama hizi.
Kwa nature ya watu wetu ilivyo,NI lazima Kuna uhusika wa ama wageni+ high profile Tanzanians AU high profile Tanzanians only.
Vyombo vya dola vielekeze uchunguzi mkubwa ndani ya serikali,ngos,balozi,vyama vya siasa,majeshi,taasisi za dini and the likes.
 
Kwanini hawa jamaa hawatoi sababu....shida yao nini..

Mbona wenzao al shaabab na boko haram madai yao yanajulikana..
Hawa kenge wanaua tu..
Wapuuzi sana.
Tatizo hawajitokezi, ...si unakumbuka kwny kampeni kuna mtu alisema kuwa ataingia serikalini hata kama kwa kupitia kwny venti, labda timuulize huyo alimaanisha nini.
 
Swali: Hivi wale Mazombi, Mungiki na.... huwa wanapotelea wapi baada ya chaguzi? Hivi ni kwanini wakati wa uchaguzi hulindwa na vyombo dola? Hivi walipovamia mkutano wa CUF walitokea wapi? Je haiwezekani ndio haohao wamesigana na waliowatumia sasa wanajaribu kuonesha ubavu wao? (ile ile hadithi ya kutotambulika uwepo wa mazombie iko katika hili la mauaji ya Pwani) Nina mashaka sana na majipu tunayoyaunda nyakati za "uchafuzi" (uchaguzi) na kulinda makundi ya wahalifu sasa tunaanza kulipa gharama zake.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Muda mfupi uliopita askari polisi wawili wa kikosi cha usalama Barabarani Bungu, Kibiti wamepigwa risasi na kufa papo hapo wakiwa kazini eneo kati ya Bungu na Jaribu! Walikuwa watatu, mmoja wa kike kasalimika!

=========

UPDATES:

Watu wasiojulikana wamemuua askari wa Usalama Barabarani katika Kijiji cha Bungu B wilayani Kibiti, mchana huu.

Taarifa za kuaminika zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa gari la askari hao pia limechomwa moto na kwa sasa vikosi vya ulinzi na usalama vinaelekea eneo la tukio.

Tutaendelea kukujuza jina la askari huyo na namna mauaji hayo yalivyotokea hivi punde.

Chanzo: Mwananchi

UPDATES 2:

Rufiji. Askari Polisi wawili wa kikosi cha usalama wa barabarani wilayani Kibiti ambao majina yao bado hayajatambulika wapigwa risasi na watu wasiojulikana katika Kijiji cha Msafiri,Kata ya Bungu wakiwa kazini.

Mbali na kupigwa risasi, pia watu hao wamechoma moto gari moja na pikipiki moja za askari hao kisha kutokomea kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa tukio na kusema anafuatilia.

Tukio hilo limetokea kilomita chache kutoka eneo ambalo waliuawa askari polisi wanane kwa kupigwa risasi katika eneo la Mkengeni walipokuwa wakitoka doria katika Kijiji cha Jaribu.
View attachment 528379
An eye for an eye will make the whole world blind
 
Kuna clip ya Lema anasema, watu wakinyimwa Uhuru wa kusema na kukosoa kwa njia halali basi watazitafuta kwa njia haramu, kwanini Nyerere alinusurika mapinduzi mengi kwenye utawala wake, wakati Mwinyi pamoja na kuharibu sana hakuna aliyefikiria kumpindua? Jibu ni moja...UHURU WA KUSEMA NA KUKOSOA

Hao magaidi wana viongozi wao, kungekuwa na Uhuru wa kusema lazima wangeropoka au kutisha kuwa madai yao yasipotekelezwa watafanya... Sasa bila Uhuru, hakuna wa kuzungumza nae.
 
Kuna clip ya Lema anasema, watu wakinyimwa Uhuru wa kusema na kukosoa kwa njia halali basi watazitafuta kwa njia haramu, kwanini Nyerere alinusurika mapinduzi mengi kwenye utawala wake, wakati Mwinyi pamoja na kuharibu sana hakuna aliyefikiria kumpindua? Jibu ni moja...UHURU WA KUSEMA NA KUKOSOA

Hao magaidi wana viongozi wao, kungekuwa na Uhuru wa kusema lazima wangeropoka au kutisha kuwa madai yao yasipotekelezwa watafanya... Sasa bila Uhuru, hakuna wa kuzungumza nae.
Hata Historia inatambua mixhe za LUDISM, CHATISM, TRADE UNIONS nk, so wataujua tu mchongo wao
 
Mpaka wanachoma moto gari na pikipiki, sidhani kama majirani wa matukio hayo hawajui. Tatizo wamekuwa terrorised kiasi kwamba hakuna wa kukupa taarifa! Niliandika wakati fulani - nadhani ISIS in the making!
 
Kwa nn waseme? Ndio style yao. Kwani lazima wawaige hao? Kwani umejuaje lengo lao ni moja? Hawajawaji kusema pia kwamba wao ni nani kwa hiyo yawezekana wala sio watu walewale au kikundi kimoja. Kuna siku kitaeleweka tu. Salamu zimefika
Nimekuelewa
 
Back
Top Bottom