Vladimir Putin amesema kuwa Iran haijaonyesha nia ya kushirikiana na Urusi katika mifumo ya ulinzi wa anga.
Siku ya Jumatano tarehe 18 mwezi Juni 2025 , Rais wa Urusi aliandaa kikao na wahariri wakuu wa mashirika ya habari, ambapo suala la vita vya Israel na Iran lilijadiliwa.
Kuhusu usaidizi kwa ulinzi wa anga wa Iran amesema: "Tuliwahi kutoa pendekezo kwa marafiki zetu wa Iran kwamba tushirikiane katika uga wa mifumo ya ulinzi wa anga, lakini washirika wetu hawakuonyesha nia kubwa wakati huo, na ndivyo ilivyokuwa."
Bw. Putin pia alisema: "Pendekezo letu lilikuwa kuunda mfumo kamili, sio uwasilishaji tofauti wa vifaa; mfumo mmoja.
Mwishowe, tulizingatia suala hili mara moja tu, lakini upande wa Iran haukuonyesha nia kubwa na suala hilo lilisitishwa.
Siku ya Jumatano tarehe 18 mwezi Juni 2025 , Rais wa Urusi aliandaa kikao na wahariri wakuu wa mashirika ya habari, ambapo suala la vita vya Israel na Iran lilijadiliwa.
Kuhusu usaidizi kwa ulinzi wa anga wa Iran amesema: "Tuliwahi kutoa pendekezo kwa marafiki zetu wa Iran kwamba tushirikiane katika uga wa mifumo ya ulinzi wa anga, lakini washirika wetu hawakuonyesha nia kubwa wakati huo, na ndivyo ilivyokuwa."
Bw. Putin pia alisema: "Pendekezo letu lilikuwa kuunda mfumo kamili, sio uwasilishaji tofauti wa vifaa; mfumo mmoja.
Mwishowe, tulizingatia suala hili mara moja tu, lakini upande wa Iran haukuonyesha nia kubwa na suala hilo lilisitishwa.