The Zanzibar Echo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2025
- 490
- 836
Rais wa Urusi Vladimir Putin amedhamiria kuendeleza vita dhidi ya Ukraine hadi pale mataifa ya Magharibi yatakapokubali kujadili amani kwa masharti yake, licha ya tishio la Rais Donald Trump kuiwekea Urusi vikwazo zaidi.
MigogoroUlaya
Putin apuuza vitisho vya Trump, aapa kuendeleza vita Ukraine
Iddi Ssessanga
Saa 15 zilizopitaSaa 15 zilizopita
Rais wa Urusi Vladimir Putin amedhamiria kuendeleza vita dhidi ya Ukraine hadi pale mataifa ya Magharibi yatakapokubali kujadili amani kwa masharti yake, licha ya tishio la Rais Donald Trump kuiwekea Urusi vikwazo zaidi.
Putin alianzisha mashambulizi makubwa dhidi ya Ukraine mnamo Februari 2022, baada ya mivutano ya muda mrefu kati ya wanajeshi wa Ukraine na waasi wanaoungwa mkono na Urusi mashariki mwa nchi hiyo. Anaamini kuwa jeshi la Urusi na uchumi wake vina nguvu za kustahimili vikwazo vya Magharibi.
Trump alitangaza kutuma silaha zaidi kwa Ukraine, zikiwemo makombora ya kisasa ya kujihami angani aina ya Patriot, huku akitoa onyo kwa Urusi kwamba ikiwa haitakubali makubaliano ya amani ndani ya siku 50, itakabiliwa na vikwazo vikali zaidi.
Vyanzo hivyo vinasema kuwa licha ya mawasiliano ya mara kwa mara kati ya Trump na Putin, bado hakuna majadiliano ya kina kuhusu msingi wa mpango wa amani. Putin anaamini hakuna mtu kutoka Magharibi aliyemshirikisha kwa dhati katika mazungumzo ya maana.
Putin anataka NATO isitanue mipaka yake kuelekea mashariki, Ukraine iwe nchi isiyoegemea upande wowote, iweke mipaka kwenye jeshi lake, walindwe Warusi wanaoishi Ukraine, na Urusi kutambuliwa kwa maeneo ambayo tayari imeshayachukua.
Urusi inadai kuwa imefanikiwa kusonga mbele katika uwanja wa vita, ikichukua zaidi ya kilomita 1,400 za mraba ndani ya miezi mitatu. Putin anaonekana kuongeza tamaa ya eneo zaidi kwa kuwa mafanikio ya awali yanampa motisha wa kuendelea.
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema vikosi vyake vinazuia mashambulizi ya Urusi licha ya maadui kuwa wengi. Anasisitiza kuwa Ukraine haitakubali kamwe kupoteza maeneo yake wala kuachana na azma ya kujiunga na NATO.
Urusi yatamba kwenye uzalishaji wa kivita
Vyanzo viwili vinaeleza kuwa uchumi wa Urusi unaolenga vita sasa unazalisha silaha, haswa makombora ya ardhini, kwa kasi inayozidi hata jumuiya ya NATO inayoongozwa na Marekani.
Trump anajaribu kuonyesha msimamo mkali dhidi ya Urusi, lakini vyanzo vya Kremlin vinaamini kuwa hana ushawishi wa kweli wa kumbadilisha Putin. Wanaona bado anaepuka kumkasirisha Putin kupita kiasi.
Ingawa kulikuwa na mazungumzo mazuri kati ya Putin na mjumbe maalum wa Marekani Steve Witkoff, hakuna hatua zilizopigwa kuelekea mpango wa kweli wa amani. Putin anahisi kuwa mazungumzo hayo hayakuelekezwa kwenye suluhu ya msingi.
Urusi inadhibiti maeneo kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na Crimea, Donetsk, Luhansk, na sehemu kubwa za Zaporizhzhia na Kherson. Putin anasisitiza kuwa maeneo hayo ni sehemu ya Urusi na Ukraine lazima ijitoe kabla ya amani yoyote kujadiliwa.
EU yakwama kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi
Katika jitihada za kuongeza mbinyo kwa Urusi, mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wameshindwa kufikia makubaliano ya pamoja kuhusu kifurushi cha 18 cha vikwazo dhidi ya Urusi, baada ya Slovakia kuweka turufu yake.
MigogoroUlaya
Putin apuuza vitisho vya Trump, aapa kuendeleza vita Ukraine
Iddi Ssessanga
Saa 15 zilizopitaSaa 15 zilizopita
Rais wa Urusi Vladimir Putin amedhamiria kuendeleza vita dhidi ya Ukraine hadi pale mataifa ya Magharibi yatakapokubali kujadili amani kwa masharti yake, licha ya tishio la Rais Donald Trump kuiwekea Urusi vikwazo zaidi.
Putin alianzisha mashambulizi makubwa dhidi ya Ukraine mnamo Februari 2022, baada ya mivutano ya muda mrefu kati ya wanajeshi wa Ukraine na waasi wanaoungwa mkono na Urusi mashariki mwa nchi hiyo. Anaamini kuwa jeshi la Urusi na uchumi wake vina nguvu za kustahimili vikwazo vya Magharibi.
Trump alitangaza kutuma silaha zaidi kwa Ukraine, zikiwemo makombora ya kisasa ya kujihami angani aina ya Patriot, huku akitoa onyo kwa Urusi kwamba ikiwa haitakubali makubaliano ya amani ndani ya siku 50, itakabiliwa na vikwazo vikali zaidi.
Vyanzo hivyo vinasema kuwa licha ya mawasiliano ya mara kwa mara kati ya Trump na Putin, bado hakuna majadiliano ya kina kuhusu msingi wa mpango wa amani. Putin anaamini hakuna mtu kutoka Magharibi aliyemshirikisha kwa dhati katika mazungumzo ya maana.
Putin anataka NATO isitanue mipaka yake kuelekea mashariki, Ukraine iwe nchi isiyoegemea upande wowote, iweke mipaka kwenye jeshi lake, walindwe Warusi wanaoishi Ukraine, na Urusi kutambuliwa kwa maeneo ambayo tayari imeshayachukua.
Urusi inadai kuwa imefanikiwa kusonga mbele katika uwanja wa vita, ikichukua zaidi ya kilomita 1,400 za mraba ndani ya miezi mitatu. Putin anaonekana kuongeza tamaa ya eneo zaidi kwa kuwa mafanikio ya awali yanampa motisha wa kuendelea.
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema vikosi vyake vinazuia mashambulizi ya Urusi licha ya maadui kuwa wengi. Anasisitiza kuwa Ukraine haitakubali kamwe kupoteza maeneo yake wala kuachana na azma ya kujiunga na NATO.
Urusi yatamba kwenye uzalishaji wa kivita
Vyanzo viwili vinaeleza kuwa uchumi wa Urusi unaolenga vita sasa unazalisha silaha, haswa makombora ya ardhini, kwa kasi inayozidi hata jumuiya ya NATO inayoongozwa na Marekani.
Trump anajaribu kuonyesha msimamo mkali dhidi ya Urusi, lakini vyanzo vya Kremlin vinaamini kuwa hana ushawishi wa kweli wa kumbadilisha Putin. Wanaona bado anaepuka kumkasirisha Putin kupita kiasi.
Ingawa kulikuwa na mazungumzo mazuri kati ya Putin na mjumbe maalum wa Marekani Steve Witkoff, hakuna hatua zilizopigwa kuelekea mpango wa kweli wa amani. Putin anahisi kuwa mazungumzo hayo hayakuelekezwa kwenye suluhu ya msingi.
Urusi inadhibiti maeneo kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na Crimea, Donetsk, Luhansk, na sehemu kubwa za Zaporizhzhia na Kherson. Putin anasisitiza kuwa maeneo hayo ni sehemu ya Urusi na Ukraine lazima ijitoe kabla ya amani yoyote kujadiliwa.
EU yakwama kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi
Katika jitihada za kuongeza mbinyo kwa Urusi, mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wameshindwa kufikia makubaliano ya pamoja kuhusu kifurushi cha 18 cha vikwazo dhidi ya Urusi, baada ya Slovakia kuweka turufu yake.