Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,681
- 1,698
Wakuu, hapa Tabora mjini eneo la Ipuli pana huyu punda kaonekana siku ya jumapili akiwa na jeraha mguuni. Jumatatu akiwa hoi nikaamua kumpa maji na kufanya jitihada za mmiliki aje kumchukua.
Ajabu mwenye punda huyu hupita tu kwa pikipiki na kumtazama. Jumatano wakaja vijana watatu wakimletea majani hayo makavu na ndoo ya maji, nikawafuata na kuwasisitizia kumchukua lakini hawajaonekana tena hivo naendelea kumpoelekea maji ya kunywa nae kaanza nizowea maana akiniona tu na ndoo yangu ya maji husimama na kuanza kunywa.
Naomba ushauri wa kufanya maana ananitia huruma kwani yupo jirani tu na makazi yangu.
Ajabu mwenye punda huyu hupita tu kwa pikipiki na kumtazama. Jumatano wakaja vijana watatu wakimletea majani hayo makavu na ndoo ya maji, nikawafuata na kuwasisitizia kumchukua lakini hawajaonekana tena hivo naendelea kumpoelekea maji ya kunywa nae kaanza nizowea maana akiniona tu na ndoo yangu ya maji husimama na kuanza kunywa.
Naomba ushauri wa kufanya maana ananitia huruma kwani yupo jirani tu na makazi yangu.