Mkuu umenikumbusha siku moja tulijaza mafuta hapo, jamaa yangu kiherehere chake kuwahi foleni akaondoa gari kabla mhudumu hajafunga kizibo cha tank, tukaingia barabarani tunamwona mhudumu anatusimamisha, jamaa akasema asitusumbue kama amepunjika ujinga wake, tumeingia vichochoroni kumbe mafuta yanamwagika tunashangaa watu wanatazama gari kila linapopita, sikumbuki alipita njia za wapi tumefika Bunju gauge imeinama


, kimlango cha tank kilijifunga na mafuta yakaendelea kuevaporate, siku ya pili tunakwenda Msata tumefika Total filling station Bagamoyo karibu na pale round about jamaa anashangaa wanamuuliza kizibo kipo wapi? Akaanza kuwalaumu wale wa Puma Mbezi, ikabidi aombe mtu dar aende Puma Mbezi akachukue kizibo aagize kwenye bus mpaka Bagamoyo, tangu saa 3 asubuhi tuliondoka saa 9 jioni.