Public Debate on Land Grabbing in Tanzania

Public Debate on Land Grabbing in Tanzania

Mwanahabari,

Lease ya miaka 99 na umilikaji hakuna tofauti. Tusidanganyane.

Na hatukatai wawekezaji katika kilimo. Tunakataa kuwapa ardhi kubwa kupindukia. Si sawa kumpa mwekezaji ekari karibu milioni moja. Tutakosa ardhi sisi tukifanya hivyo. Tutajaishia kuwa manamba katika ardi yetu.

Kama kweli nia ni kuzalisha miwa, kwanini isifanyike kama inavyofanyika Morogoro? Wananchi waoteshe miwa kwenye ardhi yao, kwa kushirikiana na mwekezaji, kisha miwa anunue mwekezaji.
 
Kama kuna mtu atatulete terms and conditions za mkataba then itakuwa easy kwa watu kufanya critical analysis.

I am not protectionist lakini nataka kufahamu kuhusu mkataba wenyewe. Kama mkataba unawapa 100% ownership ya ardhi kwa kila kitu kwa miaka 99 includes hata kama kutakuwa na gas underneath then hapo nina shaka na mkataba.

Kama hilo bonde lina wakulima wadogo wadogo then wamepatiwa solution gani, wameamisha? Na kama wamehamishwa jee wamepewa compersation kiasi gani?

Lingine jee kuna feasibility study yoyote ilioyofanywa kuonyesha kama kilimo cha miwa kwa ajiri ya mafuta kitaadhiri kiasi gani food supply? Jee kuna possibility yoyote hicho kilimo kitachangia food inflation? Na kama kutatokea food inflation jee serikali wamehedge vipi kuavoid hilo. Swala la vilimo sababu ya mafuta limesababisha bei ya vyakula kupanda kwa asilimia kubwa sana kwenye kila pembe ya dunia nzima. Na baadhi ya nchi wameanza kukataza hivi vilimo, jee nchi za wawekezaji ni moja kati nchi ambazo zimekataza au zimepunguza kilimo kwa ajili ya uzalishaji wa mafuta?

Hiki kilimo kinaweza kuingizia taifa million of dollar au kikaingizia taifa hasara ya million of dollar na tukawa cripple kwa maisha. I think more studies zinatakiwa kabla ya kukubali kwamba ni smart move, nadhani kama tutawatumia wakunzi wetu pale Sokoine University of Agriculture (SUA) ambao wamebobea kwenye Agroeconomy hawa wanaweza kufanya analysis na kuonyesha kwamba jee ni smart move au domb move kukubali kilimo cha miwa kwa ajiri ya mafuta.

Kumbuka miwa ni source ya Sukari, and if damn move zitachukuliwa then tunaweza kuona sukari imepanda to the roof and Tanzanian people can't afford that. Tumeona jinsi ethanol production ilivyopandisha bei ya maindi kwa nchi za magharibi.
 
I am sick and tired with these short term programs to make a quick buck just because it sound "profitable'

Tanzania tumejishushia hadhi na kuwa na wale malaya changudoa ambao wanagawa uchi kwa yeyote mwenye pesa au chochote, alimuradi anapewa hela.

Why not be an expensive whore? get paid like Spitzer escort big money? why are settling for cheap projects as long as someone shows us pennies?

Anza mradi wa magadi, wakulima kuacha kulima mazao ya chakula, sasa wavamizi kutoka ughaibuni wananunua ardhi nzuri ambayo priority ingekuwa ni kulima chakula cha kutosha na kutuwezesha kutumia pesa nyingi kuagiza chakula.

I tell you the problem we have is Leadership and Management! and until we have strong leaders who have good management skills and crafty decision making, we will continue to see these garbage from someone like Ole Naiko!
 
alafu watu wanasema kikwete alikuwa chagua kutoka kwa mwenyezi Mungu, Mungu atutakii mabaya hata siku moja ndi=ugu zangu

Kikwete na serikali yake ni wagumu na wavivu wa kufikilia na ndio maana haya yote yanatokea.

Baba H, bado hujategua kile kitendawili cha thank God for giving us Kikwete?
 
Kuna tatizo la kimsingi hap: Moran75 ametuambia kaenda Manyara, na akataka hekta 200 kwa ajili ya kilimo, wakamkatalia. Anasema wamemwambia wanawapa wanaotaka zaidi ya hekta 10,000.

Sasa nawahakikishieni kwamba mmoja wetu akienda Ardhi Wilayani Kisararwe au Mkoani Pwani akasema anataka hekta 5,000 (elfu tano) kwa ajili ya kilimo, watamnyima. Lakini akitokea Mzungu anataka hekta laki nne watasema ni mwekezaji na wataanza kuhaha kuhamisha watu. Nani kawaambia hawa Waswahili kwamba mwekezeji lazima awe mweupe?

Huu ni ukoloni. Tena ni ukoloni wa kizamani, sio ukoloni mamboleo. Ndugu zetu wa CCM, definition yenu ya UHURU ni ipi?
 
As long as the public is educated, and laws allow, sioni tatizo...Sheria zetu zipo nzuri tu, watendaji ndio wanatuangusha. Joint Ventures are whats needed in Tanzania. Should be the Law for investing in TZ, no foreign company can own more than 50% of anything in TZ...and to do business you have to have Tanzanian Parntership --- labda mpaka tukipata bunge na uongozi wa maana, sheria mpya zitatungwa ambazo hazi fukuzi investments but at the same time makes it fair for Tanzanians to benefit from these deals.
 
As long as the public is educated, and laws allow, sioni tatizo...Sheria zetu zipo nzuri tu, watendaji ndio wanatuangusha. Joint Ventures are whats needed in Tanzania. Should be the Law for investing in TZ, no foreign company can own more than 50% of anything in TZ...and to do business you have to have Tanzanian Parntership --- labda mpaka tukipata bunge na uongozi wa maana, sheria mpya zitatungwa ambazo hazi fukuzi investments but at the same time makes it fair for Tanzanians to benefit from these deals.

Sheria inayosema kila mwekezaji ni lazima awe na Tanzanian partners bila kuclarify hao Tanzanian partners wawe kina nani ndio inayozaa mafisadi na kujenga ukuta baina ya matabaka nchini.

Alichosema Moshi hapa unaweza kukichukulia pia kama ni partnership ambayo inamuwezesha mwananchi kuendelea kumiliki ardhi yake na mwekezaji kuitumia ardhi hiyo na wote wawili wakanufaika.

Kwa kutumia sheria iliyopo sasa, atajitokeza "fisadi" fulani ambaye atashirikiana na "mwekezaji" wa nje kuwadhurumu wananchi ardhi yao.

Na si sahihi kwa viongozi wa kitaifa kusema makubaliano yafanyike moja kwa moja na wamiliki wa maeneo hayo. Ni jukumu la serikali kuwawezesha wananchi kuuza mali zao kwa faida, kwa hiyo iwapo wameshindwa kabisa kuona umuhimu wa alichoandika Moshi basi ni bora waweke bei per unit ili wawekezaji wasiwalalalie wanavijiji ambao wengi wao wakisikilia milioni wanachanganyikiwa!
 
I am sick and tired with these short term programs to make a quick buck just because it sound "profitable'

Tanzania tumejishushia hadhi na kuwa na wale malaya changudoa ambao wanagawa uchi kwa yeyote mwenye pesa au chochote, alimuradi anapewa hela.

Why not be an expensive whore? get paid like Spitzer escort big money? why are settling for cheap projects as long as someone shows us pennies?

Anza mradi wa magadi, wakulima kuacha kulima mazao ya chakula, sasa wavamizi kutoka ughaibuni wananunua ardhi nzuri ambayo priority ingekuwa ni kulima chakula cha kutosha na kutuwezesha kutumia pesa nyingi kuagiza chakula.

I tell you the problem we have is Leadership and Management! and until we have strong leaders who have good management skills and crafty decision making, we will continue to see these garbage from someone like Ole Naiko!

Rev naona you sick and tired of CCM bullshit. Yaani i can't get a picture what need to be done. Jee tunaitaji wote tupelekwe ulaya na kuona wazungu wanavyolinda sources zao za wealth, au sijui tufanye nini.

Yaani kila siku hawa CCM wanatupeleka kwenye deep sea, why lakini? Wakati JK yeye anazurura na kukenua sura kama mfalme Mswati atazamapo mabinti wa kishona. Yaani ni hivyo hatuna ujanja, lakini i think tungeweza kuprove kwamba JK aliingia madarakani kwa EPA money, then we could declare kwamba uraisi wake ni illigitimate, then tungeita uraisi mpya na ubunge mpya.

I expected JK angesema jamani subiri(hold) any mkataba on anything mpaka tuangalie kila sheria ya kufanya mkataba. Sema anachofanya yeye ni kutembea kifua mbele kama anaumwa pumu. I am sick and tired of him, i can't wait 2010. It's time for him kwenda ukwereni akaendeleze biashara ya viyunga vya minazi, i believe he can do the best job on such kind of business. What a looser!
 
Ndugu zangu, kama nyinyi kwa mtazamo wenu mnaona wawekezaji wanachukua urithi wenu kwa wanakijiji sio hivyo. Kwa wanakijiji wa maeneo ya Kisarawe kulikotolewa ekari elfu tisa wanasumbuliwa sana na wadudu waaribifu wa mazao hasa nyani na nguruwe. Usipokaa kulinda shamba lako ndugu yangu utavuna mabua na mihogo utapata.

Kwa wakulima huyu akilima eneo hilo lote maana yake nyani na nguruwe wameamishiwa mbali na shamba lake, atapata mazao bila kulinda shamba. Kwa kipindi kirefu watu hawa hata kulima ilionekana ni kupoteza wakati maana yataliwa na nyani na nguruwe.

Ndugu zangu wana JF kilimo mumewachia wakulima, wakulima ambao kwa mtazamo wa wengi ni watu duni wasioenda shule, watu wanaolaliwa na wafanyabiashara na kuendelea kuwa duni miaka nenda miaka rudi.

Ndio maana mtu akitaka kusema ametoka kwenye familia maskini anaseme yeye mtoto wa mkulima, huo ndio mtazamo wetu na ndivyo tulivyowaweka wakulima wawe.

Wengi wetu tunajua kuwa mtu akistaafu anaenda kuanzisha shamba, nani aliyetupa mawazo haya kuwa wasio na nguvu wanaosubiri kufa ndio wakawe wakulima. Wengi wetu humu ni wafanyakazi na mawazo yetu yanaweza kuwa ya namana hiyo hiyo kuwa utakapostaafu ndio ukawe mkulima ukisubiri miaka yako michache iliyobaki kabla ya kufa shambani. Huu ndio ujinga nambari wani wa wafanyakazi wengi wa Tanzania. Yeyeto ambae alimi chakula na yupo hapa nchini aanze kutafuta shamba vijijini.

Ndugu zangu, unapokuwa na shamba kijijini na kwenda kulima uendi kulima tu bali unafundisha kwa wanakijiji kuona unafanya nini, kwa mazungumzo pamoja nao na hata kuwapa matumaini ya wapi wanapaswa kuangalia na kujua waendako na kupanga maisha yao.

Ndugu zangu, mnachopaswa kujua ni hili mtu mmoja maamuzi yako yanachukua muda mfupi kuliko serekali. ukiamua kulima leo, kesho utakuwa shambani. Sina kipimo cha serekali itachukua muda gani ila ni muda mrefu kuliko mtu binafsi. maana kuna kuandaa dokezo halafu kabrasha, halafu semina elekezi, hakafu kongamano, halafu uamasishaji wakati wanaanza kulima mtu bibafsi utakuwa umevuna mara tatu au hata mara tano.

Ndugu zangu kama kweli mnataka maendeleo ya nchi hii nendeni mkalime, sio kuchukua mapori na kutufugia nyani na nguruwe. Sina hakika ni darasa lipi kama si la tatu basi la nne wakati wetu kulikuwa na shairi "Karudi baba mmoja.........., watu wa enzi zangu mnakumbuka.

Ukweli ndio huu aridhi ya kilimo Tanzania ni kubwa tunachopaswa kufanya Watanzania wenyewe ni kwenda kulima, usipolima ndugu yangu watalima wazungu.

Unalalamika wanapewa ekari nyingi wewe una eka ngapi? Nashukuru kuna mtu ametupa moyo kuwa alikuwa anatafuta ekari mia mbili za kilimo, huyu hayupo mbali na ufalme wa Mungu.

Kama mnataka aridhi isuzwe kwa urahisi na nyinyi muwepo katika kundi la wanakijiji sio kuwaacha peke yao mtazamo usio mzuri, ukiwepo waweza kuwapa mtazamo sahihi. Chukua shamba lima ufukuze nyani na nguruwe ili tupumzike kushinda mashambani kulinda mazao yetu.
 
Ndugu zangu, kama nyinyi kwa mtazamo wenu mnaona wawekezaji wanachukua urithi wenu kwa wanakijiji sio hivyo. Kwa wanakijiji wa maeneo ya Kisarawe kulikotolewa ekari elfu tisa wanasumbuliwa sana na wadudu waaribifu wa mazao hasa nyani na nguruwe. Usipokaa kulinda shamba lako ndugu yangu utavuna mabua na mihogo utapata.

Kwa wakulima huyu akilima eneo hilo lote maana yake nyani na nguruwe wameamishiwa mbali na shamba lake, atapata mazao bila kulinda shamba. Kwa kipindi kirefu watu hawa hata kulima ilionekana ni kupoteza wakati maana yataliwa na nyani na nguruwe.

Ndugu zangu wana JF kilimo mumewachia wakulima, wakulima ambao kwa mtazamo wa wengi ni watu duni wasioenda shule, watu wanaolaliwa na wafanyabiashara na kuendelea kuwa duni miaka nenda miaka rudi.

Ndio maana mtu akitaka kusema ametoka kwenye familia maskini anaseme yeye mtoto wa mkulima, huo ndio mtazamo wetu na ndivyo tulivyowaweka wakulima wawe.

Wengi wetu tunajua kuwa mtu akistaafu anaenda kuanzisha shamba, nani aliyetupa mawazo haya kuwa wasio na nguvu wanaosubiri kufa ndio wakawe wakulima. Wengi wetu humu ni wafanyakazi na mawazo yetu yanaweza kuwa ya namana hiyo hiyo kuwa utakapostaafu ndio ukawe mkulima ukisubiri miaka yako michache iliyobaki kabla ya kufa shambani. Huu ndio ujinga nambari wani wa wafanyakazi wengi wa Tanzania. Yeyeto ambae alimi chakula na yupo hapa nchini aanze kutafuta shamba vijijini.

Ndugu zangu, unapokuwa na shamba kijijini na kwenda kulima uendi kulima tu bali unafundisha kwa wanakijiji kuona unafanya nini, kwa mazungumzo pamoja nao na hata kuwapa matumaini ya wapi wanapaswa kuangalia na kujua waendako na kupanga maisha yao.

Ndugu zangu, mnachopaswa kujua ni hili mtu mmoja maamuzi yako yanachukua muda mfupi kuliko serekali. ukiamua kulima leo, kesho utakuwa shambani. Sina kipimo cha serekali itachukua muda gani ila ni muda mrefu kuliko mtu binafsi. maana kuna kuandaa dokezo halafu kabrasha, halafu semina elekezi, hakafu kongamano, halafu uamasishaji wakati wanaanza kulima mtu bibafsi utakuwa umevuna mara tatu au hata mara tano.

Ndugu zangu kama kweli mnataka maendeleo ya nchi hii nendeni mkalime, sio kuchukua mapori na kutufugia nyani na nguruwe. Sina hakika ni darasa lipi kama si la tatu basi la nne wakati wetu kulikuwa na shairi "Karudi baba mmoja.........., watu wa enzi zangu mnakumbuka.

Ukweli ndio huu aridhi ya kilimo Tanzania ni kubwa tunachopaswa kufanya Watanzania wenyewe ni kwenda kulima, usipolima ndugu yangu watalima wazungu.

Unalalamika wanapewa ekari nyingi wewe una eka ngapi? Nashukuru kuna mtu ametupa moyo kuwa alikuwa anatafuta ekari mia mbili za kilimo, huyu hayupo mbali na ufalme wa Mungu.

Kama mnataka aridhi isuzwe kwa urahisi na nyinyi muwepo katika kundi la wanakijiji sio kuwaacha peke yao mtazamo usio mzuri, ukiwepo waweza kuwapa mtazamo sahihi. Chukua shamba lima ufukuze nyani na nguruwe ili tupumzike kushinda mashambani kulinda mazao yetu.

Mzee Pwinda asante sana kwa nasaha zako.
Hatuwezi wote kuwa wakulima, nakubaliana na wewe miono ya zamani ilikuwa ni kuretire na kwenda kulima ndizi au mananasi, lakini dunia ya leo ni tofauti kidogo. Nafahamu kuna nguruwe mwitu, nyani na wanyama wengine ambao ni kero kwenye sector ya kilimo.

Sio kweli kwamba kilimo ni sector ya kimasikini, bali serikali yetu imefanya kilimo kuwa sector ya kimasikini kwa kutowasaidia wakulima kuchannel market, vile vile kwa kuto increase infrastructure ndani ya nchi. Leo hii nikitaka kutoa mchele pale Shinyanga ili nipeleke pale muheza Tanga itanichukua masaa kwa masaa sababu ya kutokuwa na barabara zinazolink zone moja kwenda nyingine.

Hatuwezi sote kukimbilia kwenye mashamba bali tunaweza sote kunyoosha kidole pindi tunapoona kuna jambo la kinyonyoji linawakalibia wananchi. Serikali yetu ni kichwa cha mwenda wazimu, kila mtu anakinyoa. Sasa kama hatutakiamsha pindi anapokuja mnyoaji boam basi tutakwisha habari yetu.
 
Wabunge wataka ardhi wasipewe wageni
Maulid Ahmed, Dodoma
Daily News; Saturday,November 01, 2008 @22:45

Wabunge wameelezea wasiwasi wa Wakenya kutaka kutumia kofia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ajili ya maslahi yao na kutaka Tanzania isikubali wanachama wa jumuiya hiyo kumilikishwa ardhi hapa nchini.

Wakichangia katika semina juu ya Soko la Pamoja la Afrika Mashariki iliyoandaliwa na Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wabunge hao walieleza kuwa sasa hivi Wakenya wamejiandaa kutaka kunufaika na rasilimali za Tanzania ikiwamo kumilikishwa ardhi, kibiashara na kupata ajira hapa nchini.

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM) alisema, "tuwe makini na shirikisho, Wakenya wana maslahi kwetu, tuwe makini nao, wanatudharau na wanataka mali zetu, wao wanadai mali zetu kuwa ni zao kama Mlima Kilimanjaro na niliwahi kuwatukana waache kuutangaza kama wao".

Naye Mbunge wa Musoma Mjini, Vedastus Manyinyi(CCM) akichangia alisema kuwa Wakenya ni wabinafsi na wanajali bidhaa za kwao huku wakiweka vikwazo vya chinichini ili Tanzania isifaidike kibiashara.

Mbunge wa Lulindi, Suleiman Kumchaya (CCM) aliitaka serikali na Watanzania kutokubali kuburuzwa uanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuonya kuwa wanachama wa nchi za Jumuiya hiyo wanaitaka ardhi ya Tanzania ambayo ni kubwa kuliko nchini kwao.

Kwa upande wa Mbunge wa Longido, Michael Lekule Laizer (CCM), alisema, "Wilaya ya Longido na mimi Mbunge wao hawaitaki Jumuiya ya Afrika Mashariki...., kule Kenya ardhi inamilikiwa na matajiri hivyo Wamasai hawana sehemu ya malisho wanataka kuja Tanzania".

Mbunge wa Mpanda Kati, Said Amour Arfi(Chadema) aliitaka serikali kutopuuza hofu ya Watanzania kujiunga na Shirikisho la Afrika Mashariki na kuchukuliwa rasilimali zake. Wawakilishi wa serikali walisema katika semina hiyo kwamba hawapuuzi maoni yanayotolewa na wananchi.

Kuhusu dai la Zanzibar kutoshirikishwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki lililotolewa na Mbunge wa Dimani,Hafidh Ali Tahir(CCM) ambaye alisema:"Zanzibar haishirikishwi katika maamuzi, inaburuzwa, Naibu Waziri (Mohamed Abood) ni kivuli tu, ulimsikia lini akiitetea Zanzibar?" Naibu Waziri, Mohamed Abood alisema si kweli.

Akijibu hoja hizo, alisema serikali imeshabaini Watanzania kama wana hofu ya kuchukuliwa ardhi yao na kuongeza, "suala la ardhi litabaki katika ngazi ya utaifa, wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hawataweza kumiliki ardhi yetu".

Alisema kwa mujibu wa takwimu za ardhi kwa nchi, Mtanzania ana uwezo wa kupata hekta 25,000, Mkenya hekta 16,000 huku nusu yake ikiwa jangwa; Mganda anapata hekta 7,800; Burundi hekta 350 na Rwanda hekta 271. Hivyo Tanzania inaongoza kuwa na ardhi kubwa zaidi ya nchi zote za jumuiya hiyo.

Akizungumzia Zanzibar, Abood alisema uamuzi wote wa Jumuiya hiyo unaihusisha Zanzibar katika ngazi zote na kuongeza kuwa miradi mingi ya Tanzania iliyoingizwa katika Jumuiya hiyo ni ya Zanzibar kama ujenzi wa Bandari ya Unguja, Upanuzi wa uwanja wa Ndege wa Pemba na miradi ya kilimo na uvuvi.

Awali akifungua semina hiyo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Deodorus Kamala alisema, "ardhi na uhamiaji si masuala ya Soko la Pamoja, baadhi ya wanachama wa Afrika Mashariki wanafikiria wakija kufanya kazi hapa au wakaja kama wakimbizi watapatiwa ardhi na wawe wakazi wa kudumu, Soko la Pamoja sio njia mpya ya kupanua mipaka ya nchi". Alisema mauzo ya Tanzania katika jumuiya yaliongezeka kutoka dola za Marekani milioni 95.4 mwaka 2004 hadi dola milioni 117.1 mwaka 2006, huku manunuzi yaliongezeka kutoka dola za Marekani milioni 137.7 mwaka 2004 hadi dola milioni 174.4.
 
Kutoa ardhi kwa wageni ni sawa na kuuza utu au kumleta mwanaume nyumbani kwako akulindie mkeo...
 

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango (CCM) alisema, "tuwe makini na shirikisho, Wakenya wana maslahi kwetu, tuwe makini nao, wanatudharau na wanataka mali zetu, wao wanadai mali zetu kuwa ni zao kama Mlima Kilimanjaro na niliwahi kuwatukana waache kuutangaza kama wao".

Utasemaje Bungeni kwamba umetukana Wakenya ?

Huyu Mama Mbunge ni walking time bomb.
 
Awali akifungua semina hiyo, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Deodorus Kamala alisema, "ardhi na uhamiaji si masuala ya Soko la Pamoja, baadhi ya wanachama wa Afrika Mashariki wanafikiria wakija kufanya kazi hapa au wakaja kama wakimbizi watapatiwa ardhi na wawe wakazi wa kudumu...

Kwani hakuna wageni (ambao hata hawatoko Afrika Mashariki) ambao wameshapewa ardhi nchini?
 
Nilikuwa naangalia Al Jazeera kulikuwa na repoti kuhusu food security, ikaonyesha ramani ya sehemu zilizonunuliwa na China kwa ajili yua kuzalisha chakula kwa ajili ya China. Tanzania na Zim zilikuwa kwenye ramani.
Mwenye habari kamili atujulishe kinachoedelea.
 
Si ajabu kwani kuna sehemu nyingi zinauzwa kwa wageni kinyemela.
 

Land ‘grabs’ by foreigners on the rise

By FRANCIS AYIEKO

THE EAST AFRICAN

Posted Monday, June 8 2009 at 00:00

Thousands of poor people in East Africa could be among millions on the continent at risk of suffering evictions or losing access to their land to foreigners who are on an acquisition spree.

Related Stories

Kenya seeks to abolish absolute land ownership by aliens

According to a new report by the Food and Agriculture Organisation, land acquisitions by foreigners are on the increase in Africa, yet many countries on the continent do not have sufficient mechanisms to protect local land rights and take account of local interests.

This, the report says, is going to increase landlessness among the poor who would not think twice about selling their parcels of land to foreigners.

“Land acquisitions are on the increase in Africa and other continents, raising the risk, if not made properly, that poor people will be evicted or lose access to land, water and other resources,” says the report.

The report reveals a lack of transparency and checks and balances in contract negotiations, a fact that more often than not promotes deals that do not guarantee public interest.

It says that insecure local land rights, inaccessible registration procedures, vaguely defined productive use requirements, legislative gaps and other factors too often undermine the position of local people.


This means that East African countries like Kenya and Uganda where land laws are still weak and unco-ordinated, are likely to witness massive landlessness as their mainly poverty-stricken citizens sell their parcels of land at throwaway prices to moneyed foreign investors.

Kenya, for instance, has never had a single and clearly defined national land policy that could address such loopholes. A draft national land policy, which among other things, would address sensitive issues like how much land can be owned by foreigners and under what terms, is yet to be approved by the Cabinet.

Titled, Land Grab or Development Opportunity? Agricultural Investments and International Land Deals in Africa, the new study covered Ethiopia, Ghana, Kenya, Madagascar, Mozambique, Sudan, Tanzania and Zambia, among other countries.

It warns that such deals can bring many opportunities — guaranteed outlets, employment, investment in infrastructures, increases in agricultural productivity — but can also cause great harm if local people are excluded from decisions about land allocation and if their land rights are not protected.

The study highlights a number of misconceptions about what have been termed land grabs. It found that land-based investments have been on the rise in the past five years. But while foreign investment dominates, domestic investors are also playing a big role in land acquisitions.

Private sector deals are more common than government-to-government ones, though governments are using a range of tools to indirectly support private deals, it reveals.

Concerns about food and energy security are key drivers, but other factors such as business opportunities, demand for agricultural commodities for industry and recipient country agency are also at play.

Related Stories

Kenya seeks to abolish absolute land ownership by aliens

Although large-scale land claims remain a small proportion of suitable land in any one country, contrary to widespread perceptions there is very little “empty” land as most remaining suitable land is already under use or claim, often by local people.

The report found that many countries do not have sufficient mechanisms to protect local rights or take into account local interests, livelihoods and welfare.

“A lack of transparency and of checks and balances in contract negotiations can promote deals that do not maximise the public interest. Insecure local land rights, inaccessible registration procedures, vaguely defined productive use requirements, legislative gaps and other factors too often undermine the position of local people,” it says.

It calls for carefully assessing of local contexts, including existing land uses and claims; securing land rights for rural communities; involving local people in negotiations, and proceeding with land acquisition only after the citizen’s free, prior and informed consent.

“Ultimately, whether international land deals seize opportunities and mitigate risks depends on their terms and conditions — what business models are used, how costs and benefits are shared, and who decides on these issues and how,” says Lorenzo Cotula, one of the co-authors.

“This calls for proper regulation, skillful negotiation and public oversight,” she said.
 
Kunahabari kuwa wale mafisadi kutoka nchi za kiarabu wameelekea Ufilipino kununua hekari kibao kwa ajili ya kilimo cha wali.Kwa habari za ndani kabisa ambazo nilizipata nikiwa pale ubalozini Manila ,nikisoma magazeti ambayo huwa yanaletwa hapo ubalozini kila siku ,limeandika kuwamwanasiasa mpinzani ajulikanae kama Rafaeli ametaka kuwepo na inquiry kuhusiana na mipango hiyo ambayo tayari serikali imeshaingia na wageni hao ambao ni kutoka mataifa matano ya waarabu. Ingawa raisi wa nchi hiyo ambae ni mwanamama ameyatilia nguvu makubaliano yake kuwa ni mpango ulioridhiwa na United Nation kuruhusu nchi tajiri kuekeza kwenye kilimo ,mwanasiasa huyo maarufu kwa ungangari kama Seif Sharif na mtu wa kulipuwa mabomu kama Dr Slaa amesema Mataifa hayo tajiri yanafanya uhuni na pia ni ujinga wa mwisho kwa viongozi wa Ufilipino kukubali dili hilo la kuitoa ardhi yao kubwa kwa ajili ya food securiti ya nchi nyengine.Akizidi kurapu mteja huyo wa siasa za upinzani alisema jambo hilo linakwenda kinyume na taratibu za nchi hiyo na haswa zinazowahusu wananchi ambao wamekuwa wakisumbuliwa katika kujipatia hati miliki za ardhi iwe ya kujenga au kulima.

Ingawa duru za kuekeza katika nchi hiyo zimesema kuwa kuwekeza kilimo sio jambo baya na litasaidia wananchi kuajiriwa na kuendeleza kipato chao lakini jambo hilo katika nchi zenye siasa inayobadilikabadilika huwa kama ni kutega mabomu.

Kama haitoshi mwanasiasa huyo alimwaga unga aliposema kuwa dili lote halijulikani mwanzo wake wala mwisho wake kwa sababu linajadiliwa kwenye milango na madirisha yaliofungwa ila kuna tetesi zilizopatikana kutokana matembezi ya mmoja wa mafisadi hao kuwa kuna mpango usiopungua dola za kimarekani 300 milioni hao ni waQatari kuna waKuwait na pia kuna WaSaudiya nao dili ni hilo hilo la 300m kuendeleza hekari 20000 katika sehemu ya Mindanao huko nilikopanga kwa ajili ya shughuli zangu za kibiashara.

Dondoo:- Kuna Mwarabu mmoja aliefungua hoteli ya kitalii hapa Tz na kuhudhuriwa na Raisi Jakaya ,habari zake kumbe ni fisadi wa kutupwa aliekuwa akikwapua mamilioni ,amefukuzwa Uwaziri huko kwao baada ya kuwa alikuwa akitumia saini ya Waziri wa fedha kuchota hela katika akiba za Ulaya ambazo nchi yao ilikuwa imeekeza. Habari zake zipo hapa ubalozini Philipinnes wanazielewa.
 
Last edited:
Tuliyasema kwa muda mrefu ,sasa yanaanza kutimia, CCM wameaza kuuza ardhi ya watanzania kwa wawekezaji kwa miaka 99!

Nilisha sema, bila kumwaga damu nchi hii hawa mafisadi watatuuza mpaka sisi!

CCM will sell their mothers for money, its time to wake up and smell the coffe!

Mgeni apewa ardhi miaka 99


NA RESTUTA JAMES

9th May 2010
  • Wananchi walilia madini, maliasili
  • headline_bullet.jpg
    Watoa masharti kwa mwekezaji

Serikali inakusudia kumilikisha eneo la kilometa za mraba 4,450 kwa kampuni ya Agrisol ya Marekani kwa miaka 99, imefahamika.

Eneo hilo ni lile lililokuwa kambi za wakimbizi la Katumba lenye ukubwa wa kilimota za mraba 2,500 na Mishamo kilometa za mraba 2,050 yote yaliyopo wilaya ya Mpanda, mkoani Rukwa.

Taarifa za uhakika kutoka wilayani humo zinaeleza kwamba pamoja na kwamba kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya hiyo imepinga kusudio hilo, taratibu za kutoa ardhi hiyo kwa kampuni hiyo zinaendelea kama kawaida.

Badala yake, kamati hiyo inapendekeza muda wa ukodishwaji wa kipande hicho cha ardhi uwe wa miaka 20 na kwamba kampuni ya Agrisol ifanye shughuli za kilimo na si vinginevyo.

“Makubaliano yaweke bayana kuwa kampuni ya Agrisol itajishughulisha na kilimo tu na si vinginevyo kwa mfano yasihusishe uchimbaji wa madini au uvunaji wa maliasili nyinginezo…wakati wa kuingia mkataba wa uendelezaji wa maeneo haya manufaa ya halmashauri na jamii yawekwe wazi,” ilisema sehemu ya taarifa ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, Philip Kalyalya.

Kamati hiyo ya mipango imependekeza kuwa muda wa ukodishaji urekebishwe ili usizidi miaka 20 na kueleza kuwa ukodishwaji wa ardhi hiyo kwa miaka 99 hautakuwa na tija.

Aidha, Kamati hiyo inapinga kifungu cha mahusiano baina ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Kampuni ya Agrisol kilichopo kwenye rasimu ya makubaliano ya ukodishaji wa ardhi hiyo.

"Tunashauri kuwa Halmashauri isihusike katika kuijenga Agrisol mbele ya wakopeshaji kwani wakishindwa kulipa itafanya Serikali iwajibike mbele ya wakopeshaji na wawekezaji," alisema Kalyalya.

Kalyalya alifafanua kuwa gharama za ukodishaji wa ardhi hiyo bado hazijaandaliwa kwa kuwa suala hilo lipo kwenye hatua ya majadiliano.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpanda, Emmanuel Kalegero, alikiri kupokea maombi ya Agrisol kutaka kukodisha ardhi hiyo lakini akasema kwamba kwa sasa suala hilo linajadiliwa kwenye vikao vya halmashauri.
“Tumepokea maombi kutoka kwa Agrisol na tumeanza kuyajadili kwenye vikao vyetu, kampuni hiyo imeomba pia muda wa kufanya utafiti ili ijue nini kinafaa kulimwa na utafiti huo utachukua miezi sita nadhani baada ya hilo tutajua ukodishaji uwe wa namna gani,” alisema.

Mbunge wa Mpanda Kati (Chadema), Said Arfi alipoulizwa kuhusiana na kusudio hilo la Serikali alisema hakuwa na taarifa lakini akatahadharisha kwamba ukodishwaji wake uweke mbele maslahi ya wananchi wa Mpanda.

“Ardhi inagusa maslahi ya wananchi wengi, tuna migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, nadhani hili lingeangaliwa ili tusirudie makosa ya nyuma kwa kumilikisha ardhi kubwa kwa wachache wakati watu wengi wakiteseka,” alisema.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Hii ni Good new kwa nchi na wananchi watapata ajira na maendeleo tatizo lipo wapi hapo ?
 
Back
Top Bottom