Propaganda kama za CCM ndizo zilileta maafa Rwanda

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
Mfa maji haachi kutapatapa. Kutapatapa kwa CCM kunaleta hatari kubwa. CCM kimekuwa chama cha propaganda hawazungumzi sera tena, matusi kuliko hata DP. Wazee wa nchi hii wakemeeni CCM hizi propaganda ni hatari kwa usalama wa nchi. Kama ni kufa CCM ife lakini isituachie madimbwi ya damu kwa tamaa za madaraka. Watu wenye busara ndani ya CCM wako wapi jamani?
 
Ndani ya CCM mwenye burasa ni JK. Si ulimuona alivyowananga madaktari pale Diamond Jubilee. Huyo ndiye mwenye busara kuliko wote. Wale wasio busara ka Salim Ahmed Salim, Butiku, Mwinyi wamejiweka kando wamewaachia werevu kina Lusinde na Mwigilu wawatukane watz. Kwani watz wana akili?
 
Ndani ya CCM mwenye burasa ni JK. Si ulimuona alivyowananga madaktari pale Diamond Jubilee. Huyo ndiye mwenye busara kuliko wote. Wale wasio busara ka Salim Ahmed Salim, Butiku, Mwinyi wamejiweka kando wamewaachia werevu kina Lusinde na Mwigilu wawatukane watz. Kwani watz wana akili?

The kicks of a dying horse
 
Mfa maji haachi kutapatapa. Kutapatapa kwa CCM kunaleta hatari kubwa. CCM kimekuwa chama cha propaganda hawazungumzi sera tena, matusi kuliko hata DP. Wazee wa nchi hii wakemeeni CCM hizi propaganda ni hatari kwa usalama wa nchi. Kama ni kufa CCM ife lakini isituachie madimbwi ya damu kwa tamaa za madaraka. Watu wenye busara ndani ya CCM wako wapi jamani?
Ufie mbali na propaganda zako za umwagadi damu. mnyarwanda nini wewe? Nchi yetu haiwezi kufika huko hasa ukizingatia uongozi thabiti wa Rais JK. Rais ambaye hana papara, hana visasi, majungu, ubinafsi. JK atakumbukwa daima kwa uongozi wake imara pamoja na kashfa, chuki, changamto za hapa na pale zenye lengo la kumchafualia. Ukianza kusema habari za Rwanda hapa unagusa vyama fulani fulani ambavyo sera yao kubwa ni umwagaji damu, umajimbo, ukabila, uduni. Utakuaje na slogani ya hakula kulala mpaka kieleweke? hata kama siyo halali? Tuwaepuke sana watu wa aina hiyo.
 
Ndani ya CCM mwenye burasa ni JK. Si ulimuona alivyowananga madaktari pale Diamond Jubilee. Huyo ndiye mwenye busara kuliko wote. Wale wasio busara ka Salim Ahmed Salim, Butiku, Mwinyi wamejiweka kando wamewaachia werevu kina Lusinde na Mwigilu wawatukane watz. Kwani watz wana akili?
Tatizo Wa-tz tunapenda sana nyoro nyoro badala ya kufanyakazi tunakalia majungu, fitina , chuki binafsi na kuhadaiwa na akina MBOWE na SLAA eti tunachangia chama, wakati pesa wanatumbukiza kwenye matmbo yao. Wewe unaona pale Mhimbili kulikuwa mgomo kweli? mgomo wa akina MNYIKA, BISIMBA, ANALILEA na ULIMBOKA? JK alivyowambia ukweli si walichanganya na akili zao wakaona ni upuuzi. Acha kuwatukana wazee wa wtu na kisingizia kuwa Rais aliwapuuza kwa sababu tu madaktari waliamua kusitisha mgomo? kwani wewe uukuwa unapata faida gani wao kuendelea kugoma?
 
Nimekuwa nikifuatilia maneno na matamshi ya viogozi wa CCM kuhusu CDM. Nimeona kuwa sasa CCM inajaribu kuwaadaa wananchi waweze kuamini kuwa CDM ni ya watu wa Kaskazini na inaendekeza Ukabila. Maneno haya yamesemwa na Nauye katika matukio tofouti. Na hata wanajaribu kumtumia Shibuda aweze kuingiza Mgogoro ndani ya CDM ili CDM ishindwe kutawalika. Hivi karibuni Shibuda alitoa kauli hiyo hiyo ya Ukanda na Ukabila kama ambavyo viongozi wa CCM wanavyofanya. Maneno hayo ya Shibuda yanadhihirisha kuwa Shibuda sio mpambanaji na anikitumikia CCM kijahja ndani ya CDM.
Miaka kati ya 1995-2005 CCM iliweza kufanikiwa kukiuwa CUF kwa kutumia propaganda kuwa CUF ni chama cha Waislamu na Chimbuko lake ni huko Pemba. Pia iliweza pia kuwataja waanzilishi wa CUF ambao walioonishwa na Uislam wenye msimiamo mikali. Propaganda hii iliweza kuwaingia watanzania enzi hizo ambao bado walikuwa hawajakuwa na muamko wa mabadiliko na kweli watu wakaichukia CUF kama Chama Cha Uislamu. Kitendo hiki kilichafua sana CUF hasa maeneo ya TZ-Bara.Bahati mbaya sana CUF walishindwa kuua hii propaganda.
Ushauri wangu kwa wananchi na wanachama wa CDM ni kuwa macho na CCM kwa kuwa wanawatalaam wa propaganda na wanaweza kufanya lolote. Wengi wao walisomeshwa China na Urusi enzi za Chama kimoja ili waweze kukiongoza CCM kwa kutumia propaganda.
Wapenzi wa CDM sasa kaeni macho na kauli zozote za Viongozi wa CCM hasa Nauye kwa kuwa zinaweza kuwakatisha Tamaa ya M4C. Nchi yetu inahitaji mabadiliko hata iweje maana CCM sasa wameshafanya Tanzania mali yao. Wanauza kila kitu. Sasa Hivi kuna Tajiri Mmoja wa Marekani(Mwenye asili ya Ukraine) ameshaanza kuchimba dhahabu kule Majimoto maeneo ya Ring'wani wilaya ya Serengeti. Huyu Mzungu ni tajiri sana na anamiliki kampuni moja inayoitwa MPG Global. Huyu ni rafiki yake kikwete na eneo hilo ameuziwa kinyamela.Someni hapa mjue MPG Global ni ya akina nani: MPG Global - Board of Directors
Nawasilisha.
 
unayoyasema ni kweli sana kaka..CHADEMA ili iende mbele zaidi inabidi iwekeze pia katika utaalamu wa propaganda...watanzania wengi si watu wa kudadisi mambo kwa undani ndo maana wanapenda kusikiliza mambo ya juu juu au hata ya udaku..tusipowekeza nguvu katika kuzalisha wataalamu wa propaganda tutasumbuliwa sana na hawa watu japo nao propaganda zao siku hizi si za kitaaluma sana(hii ni ki refer mtu kama NAPE ambaye anaonekana sio inteliigent sana katika kutunga propaganda zenye mashiko zaidi ya kueneza hoja ambazo ukizichunguza kidogo tu unabain ni utumbo)...lakini all in all bado tuna haja ya kuwekeza katika propaganda sana
 
CDM wanatakiwa kutuaminisha kuwa sio chama cha kikanda kwa vitendo na si kwa maneno kama unavyojaribu kufanya. Mfano:-
1. Kwa nini Kafulila aliondoka CDM
2. Kwa nini Zitto alilazimishwa kuondoa jina kugombea umwenyekiti (shinikizo kubwa lilitoka kwa Mtei)
3. Vipi kuhusu sakata la marehemu Chacha (naye aliwahi kuyatamka haya akiwa mbunge kupitia CDM)
4. Vipi kuhusu uteuzi uliofanyika mgombea EALA Mr Anthony Komu
etc
Wajisafishe kwanza.
 
Hadithi hadithi hadithi njoo ,Chadema iwe ya kikanda leo hii labda mtu awe hana macho kuamini hayo watu kila kona wanatamani viongozi wakitaifa wafike kwenye maeneo yao ili wakapata upako wa ukombozi halafu mtu aseme ni chama cha kikanda wamechukua majiji yote kasoro tanga jamani hizo propaganda zimepitwa na wakati

Chadema wasiingie kwenye propaganda waendelee na principle yao ya ukweli manake ndio hali iliyowapa heshima kwa jamii
CCM wameshakufa kufufuka kunahitajika nguvu ya ziada,lakini Chadema pia waendelee kuimarisha chama kila kona ya nchi
 
CDM wanatakiwa kutuaminisha kuwa sio chama cha kikanda kwa vitendo na si kwa maneno kama unavyojaribu kufanya. Mfano:-
1. Kwa nini Kafulila aliondoka CDM
2. Kwa nini Zitto alilazimishwa kuondoa jina kugombea umwenyekiti (shinikizo kubwa lilitoka kwa Mtei)
3. Vipi kuhusu sakata la marehemu Chacha (naye aliwahi kuyatamka haya akiwa mbunge kupitia CDM)
4. Vipi kuhusu uteuzi uliofanyika mgombea EALA Mr Anthony Komu
etc
Wajisafishe kwanza.

ukifuatilia historia ya hii nchi utagundua mambo haya yalishaikuta hata TANU ...wakati tanu inataka kuikomboa nchi hii ilionekana kama ina mtazamo fulani wa kidini zaidi hasa katika idadi ya wajumbe wake na mahali vikao vya chama vilipokua vinafanyikia..lakini ilibdi mwalimu atumie nguvu sana katika kuleta usawaziko ndani ya chama na hata inaaminika kuna baadhi ya mbinu chafu alizitumia kuballance mambo..kama ni mfuatiliaji wa mambo ulishawai kusikia hili...lakini kimsingi hakuna chama kinachoweza kuanza bila kuwa na mtazamo fulani wa kiitikadi toka kwa wananchi wa kawaida japo mingi ya mitazamo hii huwa si ya ukweli... CHADEMA bado ina safari ndefu sana ya kwenda na mengi ya kufanya hasa katika mambo ya ndani ya chama na itikadi zake..cha msingi ni kujipanga kwanza kuchukua nchi halafu marekebisho ya ndani mabyo huwa hayaishi yafuate kama alivyofanya nyerere enzi za tanu
 
Labda sijui kwa watanzania wengine na hasa wasofanyia uchunguzi kauli za haina hii za kina nape, natumai izo kauli anazotoa nape ni za mfa maji, pia nape si smart kihivyo na masuala ya propaganda na ccm kwa sasa viongozi wake hawana uwezo wa kutoa shutuma zenye mashiko hata nape uyu dhaifu akuonekana bora na ata akapewa wadhifa huo, na ndo hata ccm imekuwa ikipuuzwa na watanzania wengi
pia nahamini kwa sasa watanzania wengi wameamka, enzi za ccm kuwa na nguvu zinaisha, ata ngome zao za vijijini kama wanavyokalili zinaangukia upinzani ususani mikononi mwa chadema.
Nina imani kubwa kuwa ccm imeweza kusurvive madarakani hasa 2015 kwa vitendo vyao vya wizi wa kura, hili halina ubishi kuwa wabunge wengi wa ccm wamepata ubunge kwa kuchakachua matokeo pia kwa msaada wa tume hii mbovu ya uchaguzi, mwisho hii ni changamoto pekee ilobaki na kama tutazilinda kura zetu si ajabu tukaamka asubuhi moja ccm akiwa ameshindwa vibaya na kupoteza dola.
 
Mtakumbuka azimo ya UVCCM pwani na azimio lao la kutenga watu kwa misingi ya ukanda, akina Riz 1. Sasa laana ile ile ndo kina Nape wanaendelea nayo.sasa wanafanikiwa kumnunua shibuda ili aendeleze huo ubaguzi.
 
cdm wanatakiwa kutuaminisha kuwa sio chama cha kikanda kwa vitendo na si kwa maneno kama unavyojaribu kufanya. Mfano:-
1. Kwa nini kafulila aliondoka cdm
2. Kwa nini zitto alilazimishwa kuondoa jina kugombea umwenyekiti (shinikizo kubwa lilitoka kwa mtei)
3. Vipi kuhusu sakata la marehemu chacha (naye aliwahi kuyatamka haya akiwa mbunge kupitia cdm)
4. Vipi kuhusu uteuzi uliofanyika mgombea eala mr anthony komu
etc
wajisafishe kwanza.

sijui una maanisha nini kwa item 1 - 4?
Kwani hujui kuwa most wanasiasa wa upinzani asili yao walitokea ccm? Mtu kuama chama c hajabu asa akiona imani yake iko tofauti na chama icho, sasa uyo kafulila unaemsema katoswa tena nccr, uoni apo kuwa yeye pia anamatatizo, au nako kuna ukaskazini?
Zito hakulazimishwa bali alishauriwa, kwani kuondoa jina na hii ilikuja baada ya busara kuonyesha kuwa mpansuko ungekuwa bayana kama jina lake lingeendelea kuwa kama contestant, sasa mpasuko ungekijenga au kukibomoa chama? Hizi ni busara tu zilipelekea uko, kumbuka ata mwalimu alivyo discard jina la malechele n.k.
Pia mkuu lazima hujue kuwa baadhi ya watu ndani ya chadema ni mapandikizi ya ccm, mfano shibuda wadhani action against him itakuwa ni mambo ya ukaskazini?? Let us offer support to movement for change m4c o/w tunaingia kt mtego wa mafisadi pia nape, maneno ya nape ni uzushi pia propaganda zisizokuwa na mashiko
 
Nimekuwa nikifuatilia maneno na matamshi ya viogozi wa CCM kuhusu CDM. Nimeona kuwa sasa CCM inajaribu kuwaadaa wananchi waweze kuamini kuwa CDM ni ya watu wa Kaskazini na inaendekeza Ukabila. Maneno haya yamesemwa na Nauye katika matukio tofouti. Na hata wanajaribu kumtumia Shibuda aweze kuingiza Mgogoro ndani ya CDM ili CDM ishindwe kutawalika. Hivi karibuni Shibuda alitoa kauli hiyo hiyo ya Ukanda na Ukabila kama ambavyo viongozi wa CCM wanavyofanya. Maneno hayo ya Shibuda yanadhihirisha kuwa Shibuda sio mpambanaji na anikitumikia CCM kijahja ndani ya CDM.
Miaka kati ya 1995-2005 CCM iliweza kufanikiwa kukiuwa CUF kwa kutumia propaganda kuwa CUF ni chama cha Waislamu na Chimbuko lake ni huko Pemba. Pia iliweza pia kuwataja waanzilishi wa CUF ambao walioonishwa na Uislam wenye msimiamo mikali. Propaganda hii iliweza kuwaingia watanzania enzi hizo ambao bado walikuwa hawajakuwa na muamko wa mabadiliko na kweli watu wakaichukia CUF kama Chama Cha Uislamu. Kitendo hiki kilichafua sana CUF hasa maeneo ya TZ-Bara.Bahati mbaya sana CUF walishindwa kuua hii propaganda.
Ushauri wangu kwa wananchi na wanachama wa CDM ni kuwa macho na CCM kwa kuwa wanawatalaam wa propaganda na wanaweza kufanya lolote. Wengi wao walisomeshwa China na Urusi enzi za Chama kimoja ili waweze kukiongoza CCM kwa kutumia propaganda.
Wapenzi wa CDM sasa kaeni macho na kauli zozote za Viongozi wa CCM hasa Nauye kwa kuwa zinaweza kuwakatisha Tamaa ya M4C. Nchi yetu inahitaji mabadiliko hata iweje maana CCM sasa wameshafanya Tanzania mali yao. Wanauza kila kitu. Sasa Hivi kuna Tajiri Mmoja wa Marekani(Mwenye asili ya Ukraine) ameshaanza kuchimba dhahabu kule Majimoto maeneo ya Ring'wani wilaya ya Serengeti. Huyu Mzungu ni tajiri sana na anamiliki kampuni moja inayoitwa MPG Global. Huyu ni rafiki yake kikwete na eneo hilo ameuziwa kinyamela.Someni hapa mjue MPG Global ni ya akina nani: MPG Global - Board of Directors
Nawasilisha.
ulimwengu wa leo si wa propaganda. tazama CCM walivyoadhirika Arumeru kwa wapigakura kupuuza propaganda zao za Nasari kutooa na zile za washiri. Kwa upande wa CUF, kuna makosa waliyafanya ikawa kama wao wenyewe wanathibitisha kile walichokuwa wanatuhumiwa. Nimeshuhudia swala zikienddeshwa kabla ya mikutano yao. Strategically, that was wrong.
Hii ya Dalali Kafumu kwenye board imeniacha hoi. Wamegeuka madalali wa kuuza mali zetu, hakika lazima siku moja tupate majibu.
 
Watanzania akili zetu sijui ni vipi, hata propaganda zinatushinda hivi kweli chama kinaweza kuwa cha kidini, kikabila na kikanda kwa wakati mmoja. Yaani mwanachama awe mchaga, mkristo na mtoka kaskazini, wachaga ambao sio wakristo sio wanachama1? Pia wakristo wasiotoka kaskazini sio wanachama!?. Ingekuwa hivyo sugu asingekuwa mwanachama na watu wa mbeya wasingempa kura kwa kujua chama ni cha kanda ya kaskazini pia tusingemuona zitto. Mi nawashauri ccm wachague moja kati ya haya matatu ndio walikomalie ila kwa akili ya kawaida chama hakiwezi kikawa cha kidini, kikabila na kikanda halafu kiwe na nguvu kama chadema
 
Haya Mnaishambulia CHADEMA kuhusu UDINI; Huko Zanzibar Mtasema ni nini? Mmeona na Ushahidi upo kuwa Chuki ipo dhidi ya Dini fulani

Lakini Mnakimbilia tu kwa CHADEMA; Nnaiona bado ni CHAMA kinachokuwa na kupendwa woga wenu Mnakishambulia na
Unafiki wa Udini na Ukabila - IT IS A SHAME
 
Back
Top Bottom