Rais Dr. Magufuli, utakumbukwa kwa mengi mazuri sana unayoyatenda kwa nchi yetu Tanzania.
Kwanza, ni kuwapa nafasi wasomi yaani wahadhiri nafasi ila Wengi wao wameonesha usomi wa makaratasi na siyo utendaji.
Pili, rais umekuwa na uzalendo wa dhati kwa nchi hii na watu wake.
Ombi na pendekezo langu, awamu ya pili ya uongozi wako hapo 2020, napendekeza tuondolee wahadhiri wote kwenye Baraza lako la mawaziri, na kwenye wizara zote maana wameonesha udhaifu mkubwa sana.
Maana hii awamu ya tano, imewavua nguo wasomi Wengi sana hasa wahadhiri wenye elimu ya ngazi ya uzamivu /PhD na maprofessa kwa utendaji uchwara na ubabaishaji mwingi.
Wahadhiri waendelee kufundisha vyuoni ila watumike Kama washauri na watafiti wa mambo mbalimbali.
Vinginevyo, wawe wanafanyiwa usahili kabla ya kupewa nafasi hizo ili kujihakikishia kuwa wanauwezo wa Kiutendaji.
Maana, sisi tusiofanya kazi kwenye tasinia ya vyuoni tunashangaa maajabu na madudu ya hao wasomi mfano wa akina Muhongo.
Kila la kheri JPM, together we shall win the battle!!