Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Nampa hongera ndugu yangu na mtani wangu Sospeter Mhongo nikimtaadharisha kutokuishi kwakuwafokea wananchi, kutokuishi kwa kujikweza kwa elimu yake, kutokuishi kama wasiosoma si watu wanaofaa kutoa maoni na ushauri.
Ni muda wakuishi na Watanzania wote bila ubaguzi ukimwomba Mwenyenzi Mungu akupe hekima na busara pamoja na moyo wa upendo kwa wa chama chako, wa upinzani na wasio na chama.
Futa moyoni mwako waliokunyanyasa kifikra na waliokupokonya madaraka, yamkini neema ya uongozi iliyopo mbele yako inatokana na kukataliwa kwako kulikopelekea watu waone umuhimu wako.
Nikutakie kila la heri katika harakati za kisiasa na kulijenga Taifa.
Ni muda wakuishi na Watanzania wote bila ubaguzi ukimwomba Mwenyenzi Mungu akupe hekima na busara pamoja na moyo wa upendo kwa wa chama chako, wa upinzani na wasio na chama.
Futa moyoni mwako waliokunyanyasa kifikra na waliokupokonya madaraka, yamkini neema ya uongozi iliyopo mbele yako inatokana na kukataliwa kwako kulikopelekea watu waone umuhimu wako.
Nikutakie kila la heri katika harakati za kisiasa na kulijenga Taifa.