Profesa Muhongo: Sitaomba radhi kwa wezi

Hana uzalendo wowote huyu. Uzalendo wa kweli ilitakiwa kuuonyesha siku ile ile wakati anasoma budget yake bungeni kwa kumwaga kila kitu hadharani sio kutufichaficha baadhi ya mafuta yake.[/QUO

Wewe bunge si kijiwe cha kubishana simba na yanga. Lazima uwe na data zote ndipo uwataje watu.
Mimi namuunga mkono Prof huyu mahiri. Ana msimamo na alisimama kidete kuwakatalia makampuni ya kihuni yaliyotaka kununua mafuta kwa bei ndogo Puma kisha kuuzia serikali kwa bei kubwa. Mimi wasiwasi wangu ni kuwa atahimili hayo maadili yake kwa muda gani kabla hajaingizwa kwenye fisadi strong room ya JK na CCM.
Simama kidete Prof. Najisikia fahari kubwa kwa watu wa mkoa wangu wanapkuwa weledi na kukataa kuperekeshwa na mafisadi. Wewe ni mtoto wa Mara anakotoka mwalimu JK. Tafsdhali rudisha heshima ya mkoa wetu unaochafuliwa kila siku na wanasiasa tumbo kama Wasira na wengine.
 
*Mimi simuungi mkono huyu Professor Muhongo kwa sababu ni mnafiki sana. Hana tofauti na kina Sitta, Mwakyembe, Kilango na Ole Sendeka kwenye issue ya Richmond, ukweli wote wanaujua halafu wanatuonjesha tu, mwingine wanabaki nao mioyoni mwao na kuuzika chini halafu wanataka sisi raia tuwaunge mkono!!

*Wakati anatoa hoja hii bungeni watu wengi tulimtaka ataje majina ya wabunge waliohusika na namna wanavyohujumu TANESCO ila yeye akakataa katakata akidai suala hilo anamwachia Spika Makinda na kamati ya wabunge wa CCM.

*Tumuache akaangwe na mafuta yake mwenyewe, hii ndio dawa ya mnafiki kama huyu, na sasa nawasiliana na mbunge wangu kumtaka apeleke hoja binafsi bungeni kushinikiza kujiuzuru kwa huyu waziri kutokana na kitendo chake cha kulidanganya bunge.

Mzee Concrete!
Amedanganya wapi? Kutokutaja majina ndiyo huko unakokusema kuwa n ni kudanganya? Kwako wewe kipi kinaonekana kuleta uzito zaidi na tija, kutotajwa majina na Waziri au Waziri kutangaza kuwa hapatakuwepo na mgawo wa umeme tena katika nchi yetu? Anyway sisi wengine wapitaji tu,...., mwenye nguvu mpishe,..., nchi yenu hii, wengine tupo hapa kama observers, hatuna letu,...., mnachoamua nyie wengine hatuna hata chembe ya nguvu ya kukizuia, WASILIANA NAYE MH. MBUNGE WAKO APELEKE HIYO HOJA, ili ufurahi na roho yako!
 
Ajiangalie sana na kauli zake
awakunbuke kina rutihinda na kibona misimamo iliwaponza ohoo
 
Napenda viongozi wazalendo kama hawa wakikukaba sana piga chini ka kazi kao mkuu!
Kwanini ajiuzulu. Msimamo wangu asiombe radhi na wala asijiuzulu. Kujiuzulu ni kusalimu amri ya mafisadi na hiyo ndio strategy yao. Chonde chonde Prof. never surrender
 
Profffffff Kaza buti kipimo kwa kuelimika ni pale umapoweza kusimamia Maamuzi yako, ukiamini kuwa uko sahihi.
 
Kwanini wengi hatutofautishi maana ya mgawo(power rationing) na ubovu katika mfumo wa umeme(faults).Mfano kuna tofauti kubwa kati ya kukosa maji kutokana na mgao wa maji na kukosa maji kutokana na kupasuka kwa bomba la maji.
 
Huko zamani za kale Wayahudi walikuwa wanaamini kwamba "Hakuna jambo jema litatoka Galilaya" lakini baadaye ikagundulika kwamba ni imani ya kipuuzi kuamini hakuna hakuna jambo jema linaloweza kutoka Galilaya. Leo hii kuna watu wanataka tuamini watu kama kina Prof: Mhongo hawawezi kuwa safi eti kwa sababu tu aliyewateua ni Mwana CCM!!
 
CCM siipendi lakini baadhi ya watu wake nawakubali sana. Profesa muhongo, mama Tibaijuka, Magufuli. HAWA ni watu wenye akili, uadilifu na uzalendo kwa nchi yao. Profesa muhongo achana na wapuuzi wanaojifanya wao ndio kila kitu nchini. ACHANA NA WEZI NA MAFISADI HAO. BANA KILA KONA SISI TUKO PAMOJA NA WEWE. NA UZURI NI KWAMBA HUKUOMBA HIYO KAZI NA HUNA NJAA. WAKIPITA MBELE YAKO WACHANE VIBAYA WASIKUZOEE KABISA. TENGENEZA HISTORIA YAKO KWA NCHI YAKO. TATIZO LA UMEME LIMEKUWEPO KWA MIAKA ZAIDI YA 15. LIMALIZE NA SISI TUTASEMA MUHONGO NDIYE ALIYETATUA TATIZO LA UMEME NCHINI. REKODI ZITAWEKWA. ACHANA NA MAFISADI
 
*Mimi simuungi mkono huyu Professor Muhongo kwa sababu ni mnafiki sana. Hana tofauti na kina Sitta, Mwakyembe, Kilango na Ole Sendeka kwenye issue ya Richmond, ukweli wote wanaujua halafu wanatuonjesha tu, mwingine wanabaki nao mioyoni mwao na kuuzika chini halafu wanataka sisi raia tuwaunge mkono!!

*Wakati anatoa hoja hii bungeni watu wengi tulimtaka ataje majina ya wabunge waliohusika na namna wanavyohujumu TANESCO ila yeye akakataa katakata akidai suala hilo anamwachia Spika Makinda na kamati ya wabunge wa CCM.

*Tumuache akaangwe na mafuta yake mwenyewe, hii ndio dawa ya mnafiki kama huyu, na sasa nawasiliana na mbunge wangu kumtaka apeleke hoja binafsi bungeni kushinikiza kujiuzuru kwa huyu waziri kutokana na kitendo chake cha kulidanganya bunge.
EL kakulipa nini? Au na wewe utsema ni mwanaume wa shoka?
 
What is this Country, mtu ukiwa mkweli people they don't like you, ukiwa mwizi people they do say huyu jamaa ni mjanja sana, what Tanzanians want?

Huyu Muhongo ni mtu mwadilifu sana, amefanya kazi kwenye instutition kubwa za sayansi hapa duniani bila kasha yoyote. Watanzania wanapenda sana bla bla, mtu anayeongea sana halafu hakuna positive outcome.

Wanapenda sana mtu anayedanganya Kila siku, wanapenda mtu ukiwa mwizi, na ndo maana wezi wote huwaita wajanja. Who is doubting Muhongo's credentials? He/she must be out of normal mind set. Tuache malumbano tujenge nchi yetu. Tuko um Ana sana wezi hupata nafasi ya kuiba.

Prof. We support you and will always support you, your cv profile is itself your leadership to Tanzanians.
 
anyway, ni hatua tusonge mbele...

mara profesa alipoweka mikakati yake pale bungeni.....kwa mara ya kwanza....wabunge wa CCM waliafiki kuna haja ya kukubali kuwa mawaziri wasiwe wabunge.... wakaahidi kuwa watajitahidi kulisemelea hili kwenye kutoa maoni ya katiba mpya........

tunaona jinsi gani prof muhong'o anavyokitetea cheti chake...akipotray picha ya msomi halisi......probably...similar to mwakyembe...and magufuli??? mawazo tu.....
 
Tunahitaji viongozi wa design hiyo ili tuendelee, huwezi kumuomba radhi mwizi aliyekuibia! Very stupid hiyo tume, mnafikiria kwa masaburi na kazi yenu kulindana washenzi sana hamna hata haya! Mkishapata madaraka mnajisahau kila nyiye ndo mnatufanya hii ngozi nyeusi ionekane ni ya wajinga, watu wanajishughulisha nyiye viongozi mnaweka mipango ya kuwakwamisha kisa mfaidike nyiye wachache. Masaburi yenu.
 
*Mimi simuungi mkono huyu Professor Muhongo kwa sababu ni mnafiki sana. Hana tofauti na kina Sitta, Mwakyembe, Kilango na Ole Sendeka kwenye issue ya Richmond, ukweli wote wanaujua halafu wanatuonjesha tu, mwingine wanabaki nao mioyoni mwao na kuuzika chini halafu wanataka sisi raia tuwaunge mkono!!

*Wakati anatoa hoja hii bungeni watu wengi tulimtaka ataje majina ya wabunge waliohusika na namna wanavyohujumu TANESCO ila yeye akakataa katakata akidai suala hilo anamwachia Spika Makinda na kamati ya wabunge wa CCM.

*Tumuache akaangwe na mafuta yake mwenyewe, hii ndio dawa ya mnafiki kama huyu, na sasa nawasiliana na mbunge wangu kumtaka apeleke hoja binafsi bungeni kushinikiza kujiuzuru kwa huyu waziri kutokana na kitendo chake cha kulidanganya bunge.

Mwanaume unapokuwa na haraka, wanawake wanapunjika sana wanaishia kukudharau halafu mnawalaumu.
Do you think retreats is surrendering? or do you think buying time is equal to not knowing what to do? never!!!!
 
Kwa Prof kuomba radhi haina tofauti na mwanaume kumfumania mkeo kisha ukamwambia 'sorry for disturbing you'. Upuuzi mtupu.
 
Ajitahidi akaze uzi tuendelee maana CCM tena ikishinda 2015 watamuondoa anawazibia kuiba
 
Ma prof. wa vitendo kama nyie mko wachache sana so please usikubali kuomba radhi wezi kwa ajili ya siasa.
 
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ameapa kuwa kamwe hataomba radhi bunge kwa madai aliyotoa dhidi ya watu aliowatuhumu kulihujumu Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambao amewafananisha na wezi.

Akizungumza kwenye mahojiano maalumu na Mwananchi juzi, Profesa Muhongo alisema yote aliyoyasema kwenye kikao cha Bunge la Bajeti kilichopita ni sahihi na ana ushahidi wa kutosha kuthibitisha tuhuma hizo.
“Kamwe sitaomba radhi kwa wezi. Subirini muone na kusikiliza kwenye kikao kijacho cha Bunge nitakachoongea kwa muda wa hizo dakika tano wanazotaka kunipa niombe radhi,” alisema Profesa Muhongo.

Alitoa kauli hiyo alipotakiwa kuzungumzia kuvuja kwa ripoti ya Kamati ya Brigedia Jenerali Mstaafu, Hassan Ngwilizi iliyoundwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda kuchunguza tuhuma za rushwa kwa wabunge zilizosababisha Kamati ya Nishati na Madini kuvunjwa.

Taarifa hizo za kuvuja kwa ripoti hiyo zinaeleza kuwa, Kamati ya Ngwilizi imependekeza Waziri aombe radhi na Katibu Mkuu wa wizara yake, Eliakim Maswi achukuliwe hatua za nidhami na mamlaka zilizo juu yake.
“Yaani watu waibie taifa, tuwagundue na kuwasema, halafu nisimame kuowaomba radhi? Sitafanya hivyo. Sitaki kuzungumza mengi, lakini Watanzania wasubiri kauli yangu siku jambo hilo litakapowekwa hadharani,” alisisitiza Profesa Muhongo.

Awali, akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu kikao cha Mawaziri wa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kuhusu mkakati wa kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme nafuu katika nchi hizo, Profesa Muhongo alisema hakuna na kamwe hautatokea tena mgawo wa umeme nchini.

Aliwataka wenye kuombea mgawo wa umeme utokee nchini kubadilisha maombi yao, kwani jambo hilo halitatokea tena kutokana na mikakati iliyowekwa na serikali kuongeza uzalishaji kupitia gesi asilia, mafuta na maji.

Alitaja vyanzo vingine vya uzalishaji umeme vinavyoendelea kufanyiwa kazi hivi sasa, kuwa ni makaa ya mawe, umeme jua, joto ardhi na mabaki ya mimea kama miwa ambayo imegundulika kuzalisha umeme.

Akitoa takwimu za uzalishaji umeme alizopokea juzi asubuhi katika utaratibu wake wa kupokea taarifa ya uzalishaji mara tatu kwa kutwa, Waziri huyo alisema zilizalishwa megawati 355.40 kwa kutumia gesi, 170
kwa mafuta na 110 kwa maji.

Alisema hadi sasa uwezo wa juu wa uzalishaji umeme nchini ni megawati 1,348 kwa siku wakati mahitaji ya ni megawati 830.

Waziri huyo alienda mbali kwa kuwataka wanaokwenda Makanisani, Misikitini au sehemu yoyote ya Ibada kuomba mgawo wa umeme utokee nchini wabadilishe maombi yao kwa sababu hayatasikilizwa.

Alitaja tatizo na changamoto pekee inayoikabili Wizara yake na Tanesco kuwa ni miundombinu ya kusambaza umeme unaozalishwa ndiyo maana nguvu kubwa sasa imeelekezwa kwenye uboreshaji wa miundombinu ili kila
Mtanzania mwenye kuhitaji umeme mijini na vijijini apate huduma hiyo.

Hivi sasa wanaopata huduma ya umeme nchini ni zaidi ya asilimia 18 ya Watanzania wanaokadiriwa kufikia zaidi ya 40 milioni.

Waziri Profesa Muhongo alisema idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka mara dufu kati ya sasa hadi 2017 baada ya miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia, jua, mabaki ya mimea na joto ardhi itakapokamilika.

Alisema Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuzindua mradi mkubwa wa kujenga bomba la kusafirisha gesi kutoka Mnazi Bay-Dar es Salaam.
hili ndiyo bunge linaloongozwa na magamba,ni kawaida yao wamefanya mwa Msigwa,Mnyika,waziri kivuli wa sheria,Lema,sasa wao kwa wao kwa kuwa anataka kuwaharibia ulaji wao.kazi kwenu watanzania muwachague tena hao wabunge wa magamba ambao wanaweka mbele maslahi yao
 
Muhimu atoe ushahidi. Kama hana itabidi aombe radhi au awajibike. Kama ushahidi anao kweli itabidi kamati iwajibike kwa nini hawakuutumia huo ushahidi. Sound bites peke yake hazitatosha. Credible evidence is needed and the professor knows the importance of evidence in making such huge attributions.
 
Back
Top Bottom