Profesa Muhongo: Sitaomba radhi kwa wezi

Prof huu mkwara tuu, msamaha
ataomba hata nyuma ya pazia. tangu mwanzo alikua anawafaham wezi lakini hakuwataja kwa sababu ya kuwaogopa. Ile ilikua zamu yake now its their turn akileta ubishi hata amini aise.
Umeona eeeh!!
Ninauhakika lazima tu ataomba msamaha, hii ni mikwara mbuzi tu.

Atakuja kuomba radhi ama hadharani(Bungeni) ama sirini(Kamati ya bunge au ya wabunge wa CCM). Na kuanzia hapo atakuwa mpole na rafiki mwema kwa mafisadi.
 
Nilijua tu hatawezana nao, hongera kwa kujaribu.
Bora rudi mlimani, department imekwisha sasa

kwa hawa wezi ambao ndiyo wenye dhamana ya uongozi ni ukichaa tu kukubali kufanya nao kazi..Lakini nachowaomba hawa wazalendo wasiwaache hao wezi wakatamalaki bila kuwafanyia damage for the sake of the country.....Wito kwa wazalendo wote nchini please mkigeuka nyuma mtakuwa nguzo ya chumvi na katu Mungu hatawasamehe..Ifanyieni nchi yenu jema moja once and for all....Dont you worry everything else is in control....

Hili swali najiuliza sana hivi nini maana ya nchi kutekwa? Je haiwezi kuwa kuna mapinduzi ya amani yamefanyika na tukatekwa na wezi?..Just thinking loudly how comes wezi wamegeuka kuwa heros na uwizi kugeuka kuwa sifa kuu ya viongozi nchini kwetu and nobody is taking action? Rais analia, mawaziri baadhi wanalia, viongozi mbali mbali wanalia lia tu and raia ndiyo usiseme tunalia na kusaga meno and everything is just silent....

Ninashangaa na nitaendelea kushangaa until I get an appropriate answer..Ziko wapi jamani security bodies zetu? Yakowapi majeshi yetu ya ulinzi na usalama? Why all these dirty and evil things in our country? Lakini nikifika hapo badala ya kukata tamaa najua jambo moja Mungu hajawahi shindwa hata kama binadamu wote watageuka na kwenda upande wa uasi bado yeye ni Alpha na Omega; asiyeshindwa vita....

This time I want to demonstrate what is called power the 'dunamis' which will turn the heads of all these evil men and the world where they operate upside down na kufanywa a public spectacles....Shame is upon them in Jesus name of Nazareth and will be exposed to everybody and be disgraced in Jesus name of Nazareth.

I bind the evil spirits in them into chains and command them to be thrown into the everlasting afflictions and toments... If they dont hear this voice and repent Let the water they drink turn into blood cancer in their bodies; let the food they eat turn into intestinal cancer; let the free oxygen they breath turn into pneumonia in their bodies and let the sun which shines into their bodies turn their skin into bowls?! yanayouma..Let their evil thoughts turn into high blood presures and paralysis; They shall never rest until they truly repent of their evils and leave the righteous to govern the country....The only way they can escape these is through true repentance and leave the good governance to prevail!
 
Babykailama:

Hayo yote uliyoeleza ni sawa katika mazungumzo ya kawaida. Lakini ukitaka kumtia mtu hatiani ni lazima upeleka ushahidi wa kushikika. Tume iliyoundwa ni kama mahakama. Huwezi kwenda mahakamani ukatoa maneno ya jumlajumla kama hayo uliyoeleza hapo juu ndiyo yatoshe kumtia mtu hatiani. Kumbuka makosa ambayo Profesa Muhongo amewatuhumu wenzake ni ya kuwafukuzisha ubunge na wakienda mahakama ikathibitika wanafungwa. Katika utawala wa sheria hakuna shortcut. Yeye kama kweli walimwomba rushwa ana ushahidi anao kwa nini asiutoe?

Hata mimi kwa hiyo issue ya Mwigulu ambaye umei-cite hapo juu ipo mahakamani na kesi inaendelea. Na sasa hivi sina sababu ya kujetete kwenye social media kama nilimtukana au ala, kwa sababu sasa tupo katika chombo chenyewe hasa na ukweli utajulikana hukumu itakapotoka. Ni mahakama pekee inayoweza kuthibitisha kama nilimtukana mhe MN au la, hakuna mwingine. Nakualika uendelee kufuatilia hiyo kesi na inaanza kusikilizwa rasmi tarehe 5 Novemba.

Narudia tena katika utawala wa sheria hakuna njia ya mkato ili utende haki. Tatizo letu watanzania sasa hivi tunapenda mno njia ya mkato katika kila jambo, hatutaki kuhangaika. Na kwa kuwa wanasiasa wetu wanapenda sifa za haraka haraka ndiyo hivyo tena wanatumia udhaifu wetu kupiga maneno barabarani ili tuwapigie makofi. Na wala mie sitetei wala rushwa, nawachukia na kuwalaani sana hasa inapokuja swala la viongozi. Lakini vilevile napinga sasa tabia unayoibuka ya kuwatuhumu na kuwahukumu watu barabarani, na kukataa kutumia vyombo halali katika kuthibitisha au kukanusha tuhuma zao. Hatuwezi kujenga nchi ambapo kila mtu ni hakimu, tutakuwa tunaingia kwenye the Republic of the Jungle, na baadhi yetu hatutaki tufike huko!

Naona umejibu either unayoyapenda au unayoyamudu.... does this mean you are out taken by babykailama ?
Kwa mtazamo wangu nilitegemea umtosheleze yeye au wafuatiliaji wengine tunafuatilia mjadala huu kwa kujibu yaliyokuvutia ambayo unahisi kwako yanaweza kuwa ni nguzo ya kuegemea au viganja vya kufichia uso...!!
 
Dr Kitila umechemsha na utajishushia heshima kubwa uliyoanza kujijengea kwa jamii ya wapenda haki wa nchi hii. Bora unyamaze tu maana kwa kuendelea kujitetea unaongeza aibu na uchafu katika jina na heshima yako.
 
1. Juzi na jana Mwenyekiti wa CCM (T) ambaye pia ni Rais wa Tz, katika vikao vya chaguzi za UWT na UVCCM alieleza kuwa, kuna watu wananunua uongozi na kura zinauzwa. Kwamba kuna watu wanatumia rushwa na kuna makundi ya wanaowania Urais ujao; akawaasa wajumbe wasiwapigie kura watu hao. Sasa wewe msomi, Mkumbo kamwambie na Rais Kikwete atoe ushahidi wa rushwa na au hayo makundi vinginevyo aombe msamaha.

2. Baada ya hicho kikao cha Bunge kuahirishwa, katika kipindi cha dakika 45 kwenye ITV, Mh. Job Ndugai (Naibu Spika) alisema waziwazi kuwa kulikuwa na sababu zaidi ya moja zilizosababisha kuvunjwa Kamati ya Bunge inayosimamia Wizara ya Nisahati na Madini. Moja wapo ni kuwa Wabunge wenyewe ndani ya kamati walikuwa wanalalamikiana kwa kuwatuhumu wenzao ndani ya kamati hiyo kuhusika na vitendo vya rushwa. Sasa kawambie na hao Wabunge waombe msamaha, kabla ya kumwambia Mh. Job Ndugai na pia Mh. Anna Makinda naye athibitishe ni akina nani hao waliokuwa wakilalamika la sivyo nao waombe msamaha kwani haiwezekani katika kadamnasi ya waelewa katika Bunge zima la nchi, Waziri mmoja ‘kichaa’ akaibuka na kusema kuna harufu ya rushwa halafu Spika avunje tu Kamati kwa kauli hiyo ya mtu mmoja bila kujiridhisha na yaliyosemwa au kuwepo sababu nyingine za kimazingira au vinginevyo.

3. Julai 14, 2012 saa 10.00 jioni, Dr. Mkumbo ulisema kuwa Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigullu Nchemba ni mzinzi. Je uliweza kupeleka mahakamani ushahidi wa uzinzi? Basi kama hujawahi kutuonesha jinsi ulivyokuwa ukishuhudia kwa kupiga chabo au CCTV footage ulizokuwa umetegesha tendo la uzinzi wa mtu au kuwashawishi Mh. Mwigulu na waliyekuwa wakizini naye wenyewe wakiri kuwa ni wazinzi basi omba msamaha. Wewe Mhadhiri, Mzamivu wa Saikolojia, utajidharirisha sana Dr. Mkumbo kudoubt anachosema msomi mwenzako simply kwa kuwa wewe uko CHADEMA na yeye CCM katika suala zito la rushwa inayoitafuna nchi yetu ambalo kwa ushahidi wa kimazingira vinadhihirisha wazi pasi na shaka kuwa rushwa ipo Tanzania. Waziri Sosper alisema na kuwataka baadhi (sio wabunge wote) wenye migongano ya kimaslahi na TANESCO & Wizara wasifanye hivyo, alisema pia kuwa Mkurugenzi Mhando alikuwa anafanya biashara na mkewe ndani ya TANESCO, alisema pia kuwa kuna waliokuwa wanaiba umeme kupitia vishoka na akataja hata Shule za akina Mchungaji Lwakatare n.k, alisema pia wazi kuwepo kwa hujuma za kutunga migao ya umeme (power rationing) kwa kisingizio cha uhaba wa uzalishaji wa nishati jambo ambalo ni tofauti na kukatwa umeme tokana na uharibifu au ukarabati wa miundombinu katika baadhi za sehemu. Hayo yote hayakusemwa na Mawaziri waliopita wala Viongozi wa kamati za bunge akina Mh. Makamba au rafiki yako Mh. Zitto ambao yeye alibaki kumsifia na kumtetea Mhando kuwa ni msafi na mahesabu ya vitabu vya TANESCO kuwa ni masafi. Nawe unaingia kichwa kichwa unaunga mkono mafisadi eti oh leta ushahidi katika jambo la wazi kama hili?

4. Kwa vile wewe ni mshauri ndani ya CHADEMA, mweleze vile vile Mh. Lissu atoe ushahidi ndipo uamini akiyoyasema ambapo yeye hata aliwataja Wabunge waliohusika katika tuhuma za rushwa na za migongano ya maslahi. Usiniambie kuwa Lissu ni kilaza kiasi kile cha kusikia tu eti Waziri anasema bungeni halafu yeye naye akakimbia faster mbele ya TV na na ‘kucut na kupaste’ tuhuma just kwa sababu zimesemwa na Waziri.

5. Hivi majuzi nilikusifu ukuongoza kongamano zuri UDSM la kumenzi Baba wa Taifa Nyerere. Sasa mbona baba wa Taifa, J. K Nyerere kwa shahidi tu za kimazingira kasema mara kadhaa kuwa nchi yetu inanuka rushwa au kuwa serikali ni corrupt. Na sijawahi kukusikia ukisema kuwa huamini aliyosema Nyerere maana hakutoa ‘hard evidence’ za kuwepo rushwa. Sasa naamini yule kijana aliye kukumbusha kuwa Wahadhiri wengine hamufanyi tafiti na kuandika papers, ni kweli! Nakukumbusha kuwa, Nyerere alieleza kuwa dalili za serikali corrupt, ni kutokusanya kodi; hakusema kuwa ni Mkurugenzi T, tarehe U, saa V aliyeonekana katika surveillance camera W, akipokea Tsh. X, wakiwepo askari Y na Afisa wa Takukuru Z.

Sasa huu ni mfano mzuri sana wa jinsi ambavyo watu wenye maadili na uthubutu wanaweza kuona mbali kwa utafiti wa kimazingira na kusema hapa kuna rushwa kama vile mazingira aliyoyaona huyu Profesa wa ukweli Sospeter lakini akina viegeugeu Zitto wakawa wanazunguka usiku kucha wakizuia Mhando asichukuliwe hatua.


Msomeni kiona mbali, Carl Sagan, Astronomer akitamka, “Absence of evidence is not evidence of absence!"

Waziri Sospeter hakuna kuomba radhi wala hakuna ku regret whatsoever! Mh. Spika unda Kamati nyingine na watuhumiwa wasogezwe kwenye vyama vyao. Mh. Kikwete wale Mawaziri na Watendaji wakuu wengine wanaolala na kuamka business as usual na kukuita tu Dr. Dr. bila mpango fukuza! Wanaochakalika bila uwoga kama huyu Sospeter (ambaye ni wewe ulimleta in the first place) na anaonekana kusimamia maadili na maendeleo wape support ya nguvu, maana hawa ndiwo watakaoiokoa CCM (kama inaokoka) wala sio UVCCM maana hawa Mawaziri na Makatibu wakuu ndio wasimamizi wakubwa wanaoweza kuhakikisha kuwa kero za wananchi zinapungua na viwango vya maisha ya wananchi vinapanda. Wananchi hawajali uprofesa wake wala ustadi wa kuomba miongozo bungeni bali wanataka kuona nguzo na bili za umeme zinapungua kwa mwananchi wa chini, umeme unawaka wakati wote, wachimbaji wadogo wanawezeshwa, mikataba yote inakuwa wazi na iwe ya kumfaidisha Mtanzania zaidi ya mwekezaji. Mambo kama haya ndiyo darubini yetu kwa huyu Profesa. Akianza kukatishwa tamaa tu, mafisadi nao (bila kujali itikadi za vyama) wanaanza kupeperusha bendera zao. Hii ni karne nyingine hatukubali kupotoshwa!
Nimekukubali Mara elfu moja.
 
Mkuu usitake kutupotosha kwa makusudi.
*Hakuna sheria iliyokuwa inamkataza kutaja majina ya wahalifu au kumwaga ushahidi hadharani.
Mbona wahujumu wengine wa TANESCO ambao sio wabunge aliwatajwa kwa majina na uhusika wao? Why double standard?

*Hali ya nchi yetu unaiona jinsi ilivyo sasa, Tume ni kitu cha kuchelewesha, kuficha na kupotosha ukweli. Huwezi kulinganisha na UK, USA.
Kwa tulipofikia ni kumwaga mchele kwenye kuku wengi ndio Protocol zingine zifuate.

*Sasa ushahidi wake huko kwenye tume alikong'ang'ania kuufichia umegonga mwamba, vipi sasa tena anataka kurudi kwenye njia aliyoikataa awali ili tumtetee?

kumwaga mchele ni kazi ya wapinzani siyo kiongozi mwandamizi wa serikali iliyopo madarakani...Muhongo kama waziri ni kiongozi wa wale wezi wa kwa kua TANESCO iko chini yake na alichofanya ni swa kama aliwataja majina na kuwasimamisha na kufukuzwa wengine, lakini wabunge ni huru na wana chombo chao cha kuwachukulia hatua n.k spika na kamati zao wakiunda tume za kijinga kuficha ukweli, unataka waziri aende kwenye media kutaja majina wakati wako cleared na chombo chao? na hii itamsaidia nani si ataonekana ana chuki binafsi na itafika wakati wewe na mimi tutamdharau kwa kuendeleza chuki.

tujaribu tusionee watu wachache angalau wanaojitahidi kufanya kazi ndani ya mfumo mgumu kama ulivyosema TZ siyo Uk wala US kwa hiyo huu tufanye kazi na vile tulivyonavyo wakati tukijaribu kujenga uwezo wetu zaidi wa uongozi. ila vile vile wale wachache wanaotufumbua macho na kutingisha mfumo tusiwatelekeze na kuwaita wanafiki eti kwa kutokutaja majina.
 
1. Juzi na jana Mwenyekiti wa CCM (T) ambaye pia ni Rais wa Tz, katika vikao vya chaguzi za UWT na UVCCM alieleza kuwa, kuna watu wananunua uongozi na kura zinauzwa. Kwamba kuna watu wanatumia rushwa na kuna makundi ya wanaowania Urais ujao; akawaasa wajumbe wasiwapigie kura watu hao. Sasa wewe msomi, Mkumbo kamwambie na Rais Kikwete atoe ushahidi wa rushwa na au hayo makundi vinginevyo aombe msamaha.

2. Baada ya hicho kikao cha Bunge kuahirishwa, katika kipindi cha dakika 45 kwenye ITV, Mh. Job Ndugai (Naibu Spika) alisema waziwazi kuwa kulikuwa na sababu zaidi ya moja zilizosababisha kuvunjwa Kamati ya Bunge inayosimamia Wizara ya Nisahati na Madini. Moja wapo ni kuwa Wabunge wenyewe ndani ya kamati walikuwa wanalalamikiana kwa kuwatuhumu wenzao ndani ya kamati hiyo kuhusika na vitendo vya rushwa. Sasa kawambie na hao Wabunge waombe msamaha, kabla ya kumwambia Mh. Job Ndugai na pia Mh. Anna Makinda naye athibitishe ni akina nani hao waliokuwa wakilalamika la sivyo nao waombe msamaha kwani haiwezekani katika kadamnasi ya waelewa katika Bunge zima la nchi, Waziri mmoja ‘kichaa’ akaibuka na kusema kuna harufu ya rushwa halafu Spika avunje tu Kamati kwa kauli hiyo ya mtu mmoja bila kujiridhisha na yaliyosemwa au kuwepo sababu nyingine za kimazingira au vinginevyo.

3. Julai 14, 2012 saa 10.00 jioni, Dr. Mkumbo ulisema kuwa Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigullu Nchemba ni mzinzi. Je uliweza kupeleka mahakamani ushahidi wa uzinzi? Basi kama hujawahi kutuonesha jinsi ulivyokuwa ukishuhudia kwa kupiga chabo au CCTV footage ulizokuwa umetegesha tendo la uzinzi wa mtu au kuwashawishi Mh. Mwigulu na waliyekuwa wakizini naye wenyewe wakiri kuwa ni wazinzi basi omba msamaha. Wewe Mhadhiri, Mzamivu wa Saikolojia, utajidharirisha sana Dr. Mkumbo kudoubt anachosema msomi mwenzako simply kwa kuwa wewe uko CHADEMA na yeye CCM katika suala zito la rushwa inayoitafuna nchi yetu ambalo kwa ushahidi wa kimazingira vinadhihirisha wazi pasi na shaka kuwa rushwa ipo Tanzania. Waziri Sosper alisema na kuwataka baadhi (sio wabunge wote) wenye migongano ya kimaslahi na TANESCO & Wizara wasifanye hivyo, alisema pia kuwa Mkurugenzi Mhando alikuwa anafanya biashara na mkewe ndani ya TANESCO, alisema pia kuwa kuna waliokuwa wanaiba umeme kupitia vishoka na akataja hata Shule za akina Mchungaji Lwakatare n.k, alisema pia wazi kuwepo kwa hujuma za kutunga migao ya umeme (power rationing) kwa kisingizio cha uhaba wa uzalishaji wa nishati jambo ambalo ni tofauti na kukatwa umeme tokana na uharibifu au ukarabati wa miundombinu katika baadhi za sehemu. Hayo yote hayakusemwa na Mawaziri waliopita wala Viongozi wa kamati za bunge akina Mh. Makamba au rafiki yako Mh. Zitto ambao yeye alibaki kumsifia na kumtetea Mhando kuwa ni msafi na mahesabu ya vitabu vya TANESCO kuwa ni masafi. Nawe unaingia kichwa kichwa unaunga mkono mafisadi eti oh leta ushahidi katika jambo la wazi kama hili?

4. Kwa vile wewe ni mshauri ndani ya CHADEMA, mweleze vile vile Mh. Lissu atoe ushahidi ndipo uamini akiyoyasema ambapo yeye hata aliwataja Wabunge waliohusika katika tuhuma za rushwa na za migongano ya maslahi. Usiniambie kuwa Lissu ni kilaza kiasi kile cha kusikia tu eti Waziri anasema bungeni halafu yeye naye akakimbia faster mbele ya TV na na ‘kucut na kupaste’ tuhuma just kwa sababu zimesemwa na Waziri.

5. Hivi majuzi nilikusifu ukuongoza kongamano zuri UDSM la kumenzi Baba wa Taifa Nyerere. Sasa mbona baba wa Taifa, J. K Nyerere kwa shahidi tu za kimazingira kasema mara kadhaa kuwa nchi yetu inanuka rushwa au kuwa serikali ni corrupt. Na sijawahi kukusikia ukisema kuwa huamini aliyosema Nyerere maana hakutoa ‘hard evidence’ za kuwepo rushwa. Sasa naamini yule kijana aliye kukumbusha kuwa Wahadhiri wengine hamufanyi tafiti na kuandika papers, ni kweli! Nakukumbusha kuwa, Nyerere alieleza kuwa dalili za serikali corrupt, ni kutokusanya kodi; hakusema kuwa ni Mkurugenzi T, tarehe U, saa V aliyeonekana katika surveillance camera W, akipokea Tsh. X, wakiwepo askari Y na Afisa wa Takukuru Z.

Sasa huu ni mfano mzuri sana wa jinsi ambavyo watu wenye maadili na uthubutu wanaweza kuona mbali kwa utafiti wa kimazingira na kusema hapa kuna rushwa kama vile mazingira aliyoyaona huyu Profesa wa ukweli Sospeter lakini akina viegeugeu Zitto wakawa wanazunguka usiku kucha wakizuia Mhando asichukuliwe hatua.


Msomeni kiona mbali, Carl Sagan, Astronomer akitamka, “Absence of evidence is not evidence of absence!"

Waziri Sospeter hakuna kuomba radhi wala hakuna ku regret whatsoever! Mh. Spika unda Kamati nyingine na watuhumiwa wasogezwe kwenye vyama vyao. Mh. Kikwete wale Mawaziri na Watendaji wakuu wengine wanaolala na kuamka business as usual na kukuita tu Dr. Dr. bila mpango fukuza! Wanaochakalika bila uwoga kama huyu Sospeter (ambaye ni wewe ulimleta in the first place) na anaonekana kusimamia maadili na maendeleo wape support ya nguvu, maana hawa ndiwo watakaoiokoa CCM (kama inaokoka) wala sio UVCCM maana hawa Mawaziri na Makatibu wakuu ndio wasimamizi wakubwa wanaoweza kuhakikisha kuwa kero za wananchi zinapungua na viwango vya maisha ya wananchi vinapanda. Wananchi hawajali uprofesa wake wala ustadi wa kuomba miongozo bungeni bali wanataka kuona nguzo na bili za umeme zinapungua kwa mwananchi wa chini, umeme unawaka wakati wote, wachimbaji wadogo wanawezeshwa, mikataba yote inakuwa wazi na iwe ya kumfaidisha Mtanzania zaidi ya mwekezaji. Mambo kama haya ndiyo darubini yetu kwa huyu Profesa. Akianza kukatishwa tamaa tu, mafisadi nao (bila kujali itikadi za vyama) wanaanza kupeperusha bendera zao. Hii ni karne nyingine hatukubali kupotoshwa!


mmm! JF ina watu!! nimesoma nikakubali mtiririko na mantinki yako dada baby!. Ninamueshimu Dr. Mkumbo lakini kwa hili akae tu kimya nadhani hakulichungulia hili suala kwa undani pengine ubize wa shughuli za Chuoni.
 
Nitashangaa muungwana kuomba radhi kwa wezi. Muhongo usije ukajichanga wewe ni prof uombe radhi stand "seven"!
 
kumwaga mchele ni kazi ya wapinzani siyo kiongozi mwandamizi wa serikali iliyopo madarakani...Muhongo kama waziri ni kiongozi wa wale wezi wa kwa kua TANESCO iko chini yake na alichofanya ni swa kama aliwataja majina na kuwasimamisha na kufukuzwa wengine, lakini wabunge ni huru na wana chombo chao cha kuwachukulia hatua n.k spika na kamati zao wakiunda tume za kijinga kuficha ukweli, unataka waziri aende kwenye media kutaja majina wakati wako cleared na chombo chao? na hii itamsaidia nani si ataonekana ana chuki binafsi na itafika wakati wewe na mimi tutamdharau kwa kuendeleza chuki.

tujaribu tusionee watu wachache angalau wanaojitahidi kufanya kazi ndani ya mfumo mgumu kama ulivyosema TZ siyo Uk wala US kwa hiyo huu tufanye kazi na vile tulivyonavyo wakati tukijaribu kujenga uwezo wetu zaidi wa uongozi. ila vile vile wale wachache wanaotufumbua macho na kutingisha mfumo tusiwatelekeze na kuwaita wanafiki eti kwa kutokutaja majina.
*Mkuu nani alisema kazi ya kumwaga mchele kwenye kuku wengi ni kazi ya wapinzani pekee? Mwakyembe amefanya hivyo ATC, TRC, Bandari nk, Magufuri amefanya Tanroad nk.

*Kutaja au kutotaja hayo majina na ufisadi wao ulikuwa ni utashi wake mwenyewe waziri, hivyo vyovyote vile kisheria yuko sahihi, lakini kwa kuwa alidai anauhakika na ushahidi, sisi wapenda HaKi wote tulitaka awaanike hadharani kwanza ili umma tujue na tupime mwenyewe na tuanze kumuunga mkono, lakini yeye akatudharau, sasa leo vipi tena anataka huruma zetu?

*Hatuko hapa kumwonea huruma au kumpendelea waziri Muhongo lakini tuko hapa kuona haki ikitendeka, sasa waziri kalikoroga mwenyewe tumwache alinywe.
 
Nitashangaa muungwana kuomba radhi kwa wezi. Muhongo usije ukajichanga wewe ni prof uombe radhi stand "seven"!
Mkuu acha kuishi kwa hisia jifunze kuishi kwa uhalisia.

Professor alikataaa katakata kututajia majina ya hao wezi, namna walivyoiba, vitu walivyoiba, hatua za kisheria alizowachukulia nk. halafu anataka tumuunge mkono!! how?
 
Dr Kitila umechemsha na utajishushia heshima kubwa uliyoanza kujijengea kwa jamii ya wapenda haki wa nchi hii. Bora unyamaze tu maana kwa kuendelea kujitetea unaongeza aibu na uchafu katika jina na heshima yako.
Dr.Kitila Mkumbo yuko sahihi kabisa, Professor aliamini na kuamua kufuata mfumo wa rasmi wa kisheria kuthibitisha madai yake, sasa vipi tena analalamika kisiasa badala ya kutumia hizo hizo taratibu za kisheria kupinga?
 
Muhongo bwana! Ha-ha-ha-ha-ha!
Imekuwaje ukame huu na el nino iliyopotea tumekosa mgao wa umeme? yaani majenereta yamekosa soko kabisa!
 
Babykailama:

Hayo yote uliyoeleza ni sawa katika mazungumzo ya kawaida. Lakini ukitaka kumtia mtu hatiani ni lazima upeleka ushahidi wa kushikika. Tume iliyoundwa ni kama mahakama. Huwezi kwenda mahakamani ukatoa maneno ya jumlajumla kama hayo uliyoeleza hapo juu ndiyo yatoshe kumtia mtu hatiani. Kumbuka makosa ambayo Profesa Muhongo amewatuhumu wenzake ni ya kuwafukuzisha ubunge na wakienda mahakama ikathibitika wanafungwa. Katika utawala wa sheria hakuna shortcut. Yeye kama kweli walimwomba rushwa ana ushahidi anao kwa nini asiutoe?

Hata mimi kwa hiyo issue ya Mwigulu ambaye umei-cite hapo juu ipo mahakamani na kesi inaendelea. Na sasa hivi sina sababu ya kujetete kwenye social media kama nilimtukana au ala, kwa sababu sasa tupo katika chombo chenyewe hasa na ukweli utajulikana hukumu itakapotoka. Ni mahakama pekee inayoweza kuthibitisha kama nilimtukana mhe MN au la, hakuna mwingine. Nakualika uendelee kufuatilia hiyo kesi na inaanza kusikilizwa rasmi tarehe 5 Novemba.

Narudia tena katika utawala wa sheria hakuna njia ya mkato ili utende haki. Tatizo letu watanzania sasa hivi tunapenda mno njia ya mkato katika kila jambo, hatutaki kuhangaika. Na kwa kuwa wanasiasa wetu wanapenda sifa za haraka haraka ndiyo hivyo tena wanatumia udhaifu wetu kupiga maneno barabarani ili tuwapigie makofi. Na wala mie sitetei wala rushwa, nawachukia na kuwalaani sana hasa inapokuja swala la viongozi. Lakini vilevile napinga sasa tabia unayoibuka ya kuwatuhumu na kuwahukumu watu barabarani, na kukataa kutumia vyombo halali katika kuthibitisha au kukanusha tuhuma zao. Hatuwezi kujenga nchi ambapo kila mtu ni hakimu, tutakuwa tunaingia kwenye the Republic of the Jungle, na baadhi yetu hatutaki tufike huko!

Kitila J. K . Nyerere aliwah kusema ikiwa hakimu atahukumu kesi na wananchi wakalalamika haki haikutendeka nilazima ujuwe ipo harufu ya rushwa. Take from Me yale amesema Prof Mulugo ni kweli kweli mtupu na mahakama, tume wameunda ni kíini macho. Take from me sheria zetu nirahisi sana and that is y mafisadi wanafanya vile wanajisikia. Prof we pray 4u achana na vilaza
 
Mkuu acha kuishi kwa hisia jifunze kuishi kwa uhalisia.

Professor alikataaa katakata kututajia majina ya hao wezi, namna walivyoiba, vitu walivyoiba, hatua za kisheria alizowachukulia nk. halafu anataka tumuunge mkono!! how?

Simple logic ni hivi;
Kwa nini kwazaidi ya miaka 5 iliyopita mgao ulikuwa ni wa lazima kila mwaka? Kwa nini mwaka huu tu ndo basi, tena baada ya Muhongo kuingia. no somo rahisi tu!
 
Profesa yupo sahihi, ila tu hizi ni mbinu za mafisadi.

Tatizo ni kueleza atakayo sema siku ya kikao cha bunge, alistahili kukaa kimya ili awape kwa mshtuko lakini sasa mafisadi wamejua kuwa haogopi na atafanya kweli, watachukua mbinu nyingine kama kuacha upepo upite

Mkumbo, kwa kweli si mwelewi ila sintashangaa kama ni pandikizi la magamba kama Zito.
 
Kitila J. K . Nyerere aliwah kusema ikiwa hakimu atahukumu kesi na wananchi wakalalamika haki haikutendeka nilazima ujuwe ipo harufu ya rushwa. Take from Me yale amesema Prof Mulugo ni kweli kweli mtupu na mahakama, tume wameunda ni kíini macho. Take from me sheria zetu nirahisi sana and that is y mafisadi wanafanya vile wanajisikia. Prof we pray 4u achana na vilaza
Mkuu embu funguka zaidi utueleze ni ukweli upi huo ambao Professor Muhongo aliuzungumza bungeni au kwenye kamati ambao utatushawishi tumwamini?
 
Simple logic ni hivi;
Kwa nini kwazaidi ya miaka 5 iliyopita mgao ulikuwa ni wa lazima kila mwaka? Kwa nini mwaka huu tu ndo basi, tena baada ya Muhongo kuingia. no somo rahisi tu!
*Mkuu swala la mgawo wa umeme(Rationaling) tulishalizungumza humu JF tangu 2008, na majibu yalikuwa ni mpango rasmi wa makusudi ili kuwaneemesha watawala.

*Kama mgawo hakuna kwa sasa ni uthibitisho kuwa Professor Muhongo hana maslahi binafsi Tanesco katika mgawo wa umeme.

*Sioni kitu kingine chochote cha zaidi, kama kipo ni kazi ya Professor Muhongo kutushawishi kwa kumwaga mchele kwenye kuku wengi na sio kuufukia ukweli wake kwa spika Makinda na kamati za bunge.
 
Profesa yupo sahihi, ila tu hizi ni mbinu za mafisadi.

Tatizo ni kueleza atakayo sema siku ya kikao cha bunge, alistahili kukaa kimya ili awape kwa mshtuko lakini sasa mafisadi wamejua kuwa haogopi na atafanya kweli, watachukua mbinu nyingine kama kuacha upepo upite

Mkumbo, kwa kweli si mwelewi ila sintashangaa kama ni pandikizi la magamba kama Zito.

*Professor Muhongo ni Professional katika mambo ya miamba, madini na nishati, lakini kwenye mambo ya kisiasa bado ni mchanga sana!!

*Kama mafisadi hawalali usiku na mchana wanatafuta mbinu za kisiasa kummaliza, Why Professor hajipangi kisiasa kupambana nao?

*Kuhusu Dr. Kitila Mkumbo, mbona wengine tumemwelewa vizuri tu, hakuna issue yoyote ya upandikizi hapa. Dr.Mkumbo kasema Facts na sio kushabikia Myths.
 
bado tunasafari ndefu sana! mpaka tuache ushabiki tuanze kufikiri kwa kina! itatuchukua muda na wala hatuwezi endelea. kalibia wote mliochangia ni wale watu wanomsubiri ipigwe ngoma waanze kutingishika bila hata kutafakari ngoma inahusu nini. kama wabunge tu! nae muhongo anawaweza kwwelikweli yeye ni kupigango ngoma mnacheza tu. hata ukulala kiza akikwambia mgomo ni historia wewe unashangilia. wabunge waliambiwa kuna wizi wote si waupuinzani wala ccm wakapanua midomo ooh!wezitunawajua! wezi tunawajua! basi muhongo akapitisha bajeti yake bila hata kuhojiwa mambo ya msingi. unacheza na profesa! alafu lugha ya kusema yeye si mwana siasa muache! huo ni umbumbumbu wa mambo na kama hujui si lazima uchangie ujinga wako. uwanasiasa si rangi wala umbo bali "to host any political position".
 
Back
Top Bottom