tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,862
- 25,171
- Thread starter
- #41
Longo longo pro muhongo siyo asili yake. kumshauri aende kivukoni kusoma siasa ni kumwambia aende kusoma longo longo. Mzee huyu haangalii sura wala chama. Ulivyokuja ndivyo atakavyokujibu. Kutaka kuonyesha matokeo ya mh Sendeka nayo ni sawa maana alitaka kuonyosha uelewa wa mtu huyo. tuwe wakweli hivi hatuoni mabadiliko ktk sekta ya umeme tangu pro muhongo awe waziri? kwa nn tusione kwamba huyu pro ameziba liziki za watu ndiyo maana anasakamwa? Hatukumbuki dili la mafuta mazito? Nani asiyeelewa Dr mengi anavyopenda kuabudiwa lkn pro hamuabudu na ndiyo chanzo cha wawili hawa kutoelewana? Mnataka serikali iwekwe mfukoni na watu wa aina ya Dr mengi? Watz bw angekuwa mpole mngemsodoa!! Anaonyesha makucha mnalalamika! kwani amezuia asichunguzwe km kuna tuhuma za kweli dhidi yake? Bila aibu unashauri wizara iongozwe na vihiyo mikataba ya kimataifa wataipambanuaje. Unasemaje matokeo ya mtu ni siri wakati hubandikwa ktk mbao za matangazo na sasa unayaona kiganjani? Huyu ni mzee wa makavu kavu. SHIKAMOO PRO MUHONGO.
Mkuu, tafakari kabla ya kuandika. Matokeo ya Ole Sendeka yatasaidiaje kutatua ufisadi na mgawo wa umeme unaoikumba nchi hii? Hivi unakumbuka kwamba Profesa huyu huyu naliwahi kusema umeme hautapanda bei lakini mwezi huo huo umeme ukapanda bei? Wewe unaishi nchi gani? Unajua jinsi bei ya juu ya umeme inavyotuumiza? Inaonekana wew huishi Tanzania--ungekuwa hapa nchini ungegundua madudu yaliyopo kwenye Wizara hii ya Umeme.
Hlafu naomba nikukumbushe kwamba Prof alimshambulia Ole Sendseka--hajamuongelea Dr Mengi hata kidogo. kama hujui jambo ni bora ukauliza watu waliopo Tanzania. Sio unajichimbia huko nchi za watu halafu hujui shida tunayopata kwa kukosa umeme wa uhakika ktk nchi hii. Na fedha za umeme zimeliwa na mafisadi, watu tunalalamika wewe unaleta masikhara. You can't be serious!
cc:[MENTION]msalani[/MENTION] lusungo Simiyu Yetu mwa 4 T2015CCM FaizaFoxy Mchambuzi Ritz [MENTION]lizabon[/MENTION] siafu dume
Last edited by a moderator: