Profesa Anna chupuchupu kukamatwa na PCCB

Profesa Anna chupuchupu kukamatwa na PCCB

Mwakani naenda kupambana nae kupitia chama cha kidemokrasia tuone kama mdomo ataurefusha tena labda wanipambanishe na Alfred Tibaigana nasikia nae yumo hapo patachimbika.

Nakuhakikisha hayumo Huyu A. Tibaigana niliongea naye anasema siasa sasa basi, yeye anapambana na kilimo na miti aina ya karibea, yaani huyu mstaafu namkubali sana, ameajiri vijana kibao kwenye shamba jipya , na amenunua sehemu ambayo ni vigumu kustawisha kitu, lakini yeye limemfaa zaidi, kuna ndizi za kufa mtu.
Mama la prosesali huko ana kitu, kama anataka sifa aziweke kwenye kiimo sio kutafuta umaarufu kifisadi. Shule yenyewe Kajumulo iko taabani sijui hizo hela zinasaidia kitu gani ati!!!
Kama unataka kugombea ni-pm nikupe data jinsi ya kuwapiku vigogo hawa, hawana jipya.
 
Mapovu ya nini Dada? Umewahi kumsikia Halima Mdee akimchana chana huyu Jambazi wa ESCROW kiasi cha kumfanya aachie ushuzi mwembamba? Unafikiri wote tunalishwa na huyo mamako aliekoswakoswa kunaswa na PCCB jana? Mradi wa kigamboni na hisa zake za ESCROW unafikiri hazijulikani?... Tuepushie mashuzi hapa jamvini ...

Hayo matusi yako si ya bure kwani inaelekea ujumbe wangu umefika kwako barabara! Maana hapa unajaribu kuonyesha CHUKI ZAKO BINAFSI! Na hii haisaidii kwani ukweli unajulikana hata wewe unajua kuwa hao ndugu zako ndiyo wezi. Wewe ni kati ya wale walio ajiriwa hapa JF kwa kazi hii. Wakati mwingine ninakuelewa kwani bila kuandika chochote mtandaoni si ajabu mtoto wako hatapata hata chai ya hasubuhi.
 
Naomba nijuzwe kwanza , Hongo nini? Kinyume na hapo hii taarifa haijakamilika.
 
Katika hali isiyo ya kawaida leo aliyekuwa waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka ameponea chupuchupu baada ya vijana wa PCCB Wilayani Muleba kuvamia nyumbani kwakwe ghafla baada ya kupata tetesi kuwa alikuwa akigawa hongo kwa vijana wa mjini hasa wachuuzi wa ndizi ambao walikuwa wamejumuika kwake baada ya kuwaarika.

Alibainika mapema leo asubuhi kuwa profesa Anna anakikao na vijana hao na mwaliko wao uliambatana na ahadi ya pesa. Baada ya vijana wa PCCB kujulishwa kuhusu mchezo huo walijipanga kuhakikisha wanafanya kazi yao lakini taarifa za PCCB kujipanga zilimfikia Profesa kabla hajaanza kutoa rushwa.

PCCB walipovamia nyumbani kwake Kagabiro walikuta kundi la vijana na walipowapekua vijana hao hawakuweza kupata pesa hizo maana profesa alikuwa keshatonywa mapema kuhusu mtego wa PCCB.

Toka waziri huyo atemeshwe kibarua chake amekuwa kijijini kwao akifanya kila liwezekanalo kuwashawishi wananchi wa kada mbali mbali kwamba yeye ameonewa na kila baada ya vikao amekuwa na kawaida ya kutoa pesa kuanzia tsh 5000 hadi 25000 kulingana na hadhi ya mtu.

Juzi alifanya mkutano na watendaji, wenyeviti wa matawi wa CCM na makatibu wao ambapo baada ya kikao kwasababu walikuwa wengi waliambulia shs5000 na wengine 6000.

Watu wanajuuliza kweli na profesa anatimza ahadi zake kwa wananchi kupitia hongo kwa viongozi au ndo mambo ya ESCROW yameanza kufanya kazi?

Muleba tumebaki midomo wazi.

Prof. mbona tangu juzi yuko mwanza au wapikaji wa uongo ndo mko kazini?
 
Back
Top Bottom