Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,875
Anaandika Prof.Wajiri Sanganyi(US).
Nina wasalimia kutoka huku kwa bwana Trump ambapo tupo huku kimajukumu,Ila tukiendelea kufuatilia yote ambayo yanaendelea nyumbani huko Tanzania.
Nimeshiriki siasa za upinzani huko Tanzania miaka ya 1991 nikiwa na akina Juliasy Miselye ,Prosper Rwegoshora,Peter Golugwe,akina Thao,Mgeta, Leo Lwekamwa. Leo Lwekamwa sasa hivi yeye yupo huku US, wakati huo tukiwa TLP.
Leo ninataka nitoe ujumbe huu kwa viongozi na wanachama wa vyama pinzani.Nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa siasa zinazoendelea sasa hivi nchini kwetu Tanzania.Hasa upande wa CCM , vyama pinzani, chadema na ACT-mzalendo.Mnapitia changamoto kadhaa poleni.Ni changamoto ambazo hata sisi tulipitia huko nyuma wakati wa Nyerere,Mwinyi na Mkapa.
Naomba leo nizungumzie kuhusu upinzani tuu.Kwa namna ninavyoamini vyama vikubwa vya upinzani Tanzania kwa sasa ni vyama viwili tuu, Chadema na ACT mzalendo mnikosoe nikikosea.
Ninataka kuwaambia viongozi wa vyama pinzani nchini Tanzania hasa Chadema chini ya mtoto wangu Mbowe na ACT mzalendo chini ya mtoto wangu Zitto.
Lazima mfahamu kwanza vyama huwa havidumu milele bali vinazakiwa,vinakuwa na hufikia muda vinakufa au vinakosa nguvu kabisa.Hii sio hiari ni kanuni (Party is formed,grow and witheraway).
Siasa za vyama hivi viwili kati ya Chadema na ACT mzalendo ni siasa za kugombea kuishi (Survival for the fittest).Chadema wapo katika kilele cha ukuaji(Grey step/Peak step),Act mzalendo ndio wanaanza ukuaji hasa baada ya kumpokea Maalimu Seif hivyo wanapambana kukuwa.
Nina rafiki zangu wapo Chadema mara zote huwa wakiniambia kwamba Chadema haiwezi kuunganisha nguvu na ACT mzalendo kwani ACT mzalendo ni chama kidogo sana.Mimi huwa nina washauri Chadema kama wanahitaji waendelee kuwepo katika midani ya siasa ni lazima waunde umoja na ACT mzalendo pia na vyama vingine pinzani katika chaguzi.
Huwa nina ambia rafiki zangu huko Chadema kwamba wasitiwe upofu na wingi wa wabunge walio nao ,hao walipatikana mwaka 2015 tuu sio guarantee ya kuendelea kuwapata katika chaguzi zijazo bila nguvu ya umoja.Hivyo kudharau vyama vingine wanavyoita vidogo sio vyema hata kidogo .Sisi tulio watangulia tunajua hayo.Nina wapa mifano kuanzia uchaguzi wa 1995 , 2000,2005,2010,2015
Mwaka 1995,NCCR ilikuwa chama pinzani kikuu chenye nguvu kipindi hicho chini ya Mbatia , Anthony Komu,Masumbuko Lamwai,Ringo Tenga,Mvungi na Mrema.
Uchaguzi wa 1995 ,Mkapa wa CCM alipata kura 4026422 sawa na asilimia 61.82 akifuatiwa na Mrema akiwa Chama kikuu cha upinzani NCCR alipata kura 1,808,616 sawa na asilimia 27.77,vikifuatiwa vyama vingine vya upinzani .Nakumbuka Mkoa wa Dar es salaam wakati ule Mrema alipata kura nyingi sana hatimaye uchaguzi ule mkoa wa Dar ulifutwa .
Miaka mitano kupita ulikuwa uchaguzi wa 2000 ,awamu ya pili ya Mkapa.Matokeo Mkapa kura 5,863,201 asilimia 71.74 ,Sasa hivi karata ilibadilika sio NCCR tena ilikuwa CUF chini ya lipumba akipata kura 1,329,077 asilimia 16, akifuatiwa na TLP baada ya Mrema kuhamia TLP kutoka NCCR ,NCCR ikawa ya Mwisho hata wabunge ikashindwa na TLP.Nakumbuka TLP waliopata wabunge 16 pia kuongoza Halmashauri ya Moshi, nakumbuka kipindi hicho msajili George Liundi alitaka kukifuta chama cha TLP kabla ya uchaguzi wa 2000 ,baada ya uchaguzi wa 2000 TLP chini ya Leo Lwekamwa na akina Thao ,Mselya,Mgeta ikawa ponapona yao.
Chama cha NCCR kilipotelea mbali naambiwa sasa hivi kina Mbunge mmoja James Mbatia.
Uchaguzi wa 2005 , Kikwete wa CCM alipata kura 9,123,952 sawa na asilimia 80.28 , akifuatiwa na CUF ya Lipumba wakati huo kura 1327125 , akifuatiwa Mbowe wa Chadema kura 668,756 asilimia 5.88
Hapo ndipo ilikuwa mwisho wa Chama cha NCCR,TLP na CUF kama vyama vikuu vya upinzani nchini Tanzania.
Uchaguzi 2010 Kikwete wa CCM alipata asilimia 62.83 na chama pinzani kilichoongoza ni Chadema mgombea wake Dr.Slaa asilimia 27.05 akifuatiwa na Lipumba CUF asilimia 8.28
Na 2015 aliongoza Magufuli wa CCM na upinzani ni ukawa Lowasa.
Hii ni mifano dhahiri ili Chadema wajue kwamba ponapona yao kama chama kikuu cha upinzani ni Umoja miongoni mwa vyama pinzani.Ndio nafasi yao ya kuendelea kuishi bila njia hiyo ni rahisi chama hicho kufa mapema kama vyama vingine namna vilivyokufa.
Wafuasi mara zote hubadilika baada ya kuona chama kimepoteza mvuto au kuzeeeka,wafuasi waliacha NCCR 2000 waka Support CUF na TLP ,waliacha TLP 2005 waka Support CUF na Chadema,2010 wafuasi waliacha CUF waka Support Chadema ,2015 ilikuwa ukawa ndio Chadema ikapata wabunge wengi wanaoringia sasa bila umoja tena wa vyama pinzani chadema mtaongea habari nyingine mara nyingi huwa nina waambia .
Hivyo kwa aina ya Siasa za sasa Chadema haipaswi kudharau kabisa chama cha ACT mzalendo kwa kutamka hawawezi kuungana.ACT mzalendo naambiwa kimeenea Zanzibar kote , bila kusahau lazima tufahamu kwamba siasa za Zanzibar ni za tofauti na bara.Zanzibari hata wasipoungana ikisimama ACT tuu uwezo wa kupambana na CCM upo mkubwa na kupata viti hata kura nyingi.
Ila huko bara Chadema na ACT mkusimama pekeenu,mtafanywa kama kwenye chaguzi za marudio (Wabunge na Madiwani) , pia serikali za mitaa.
Kwa mfano Chadema na ACT mzalendo huko bara mkikosa jimbo hata moja bila kuungana , Zanzibar ACT mzalendo itapata viti hivyo na ACT kuwa chama kikuu cha upinzani kupitia Zanzibar sababu siasa zao ni tofauti na huko bara.
Mimi nina jua kuwa Chadema kinachukia sana kukuwa kwa ACT mzalendo hasa baada ya Maalim Seif kuhamia ACT mzalendo,chuki za namna hiyo zipo sana katika siasa za upinzani .Kuhama kwa Maalim Seif kwenda ACT mzalendo ilikuwa ni sawa na kuhama kwa Mrema kutoka CCM kwenda NCCR.
Mrema akiwa CCM alikuwa na cheo cha Naibu waziri Mkuu na waziri wa wizara nchini.Wakati huo Mrema alikuwa Mrema ,Mrema kweli .Alipo hama kutoka CCM alitakiwa kwenda TLP kwa akina Leo Lwekamwa na ikatakiwa awe mwenyekiti wa TLP ,akina Leo Lwekamwa akakubali kujiuzulu na wakaenda badili jina la mwenyekiti kwa msajili wakati huo ni George Liundi hivyo kujiandaa kumpokea Mrema ili aingie TLP,wakafunga Safari hadi Moshi kumchukua Mrema.Walipofika wakapata taarifa kwamba Mrema ameshawishiwa na NCCR hivyo amejiunga na NCCR.
Akina Leo Lwekamwa waliishiwa nguvu hivyo kuanzia 1995 hadi 2000 TLP walikuwa na chuki kubwa dhidi ya NCCR ,hii ndivyo ilivyo sasa kwa Chadema dhidi ya ACT mzalendo hasa baada ya Maalim Seif kuhamia chama hicho ikiwa cha ACT mzalendo wakati Chadema wakati huo waliniambia walikuwa tayari wamerekebisha ofisi yao kubwa Makao makuu Chadema Zanzibar ipo Kikwajuni.Chadema walikasirishwa kwa kwa hoja ya kwamba Maalim kwenda katika chama kidogo ACT mzalendo ni kuvunja nguvu ya upinzani alipaswa kuja katika chama kikuu cha upinzani bara ili kiwe tena nguvu Zanzibar ,hii ni chuki kubwa dhidi ya ACT mzalendo .
Ndio maana , uchaguzi serikali za mitaa hawakuungana na kwa taarifa nilizopewa uchaguzi mnafanya mwaka huu CHADEMA hawataki kuungana.
Ukweli ni kwamba mtu mwenye umri wa miaka 60 huwezi kumpa umri wa kuishi (Life expectancy) ya miaka 50 ijayo huwa ni vigumu atakuwa aidha mzee sana hajiwezi au kufa huo ndio mfano wa Chadema kwa sasa, Chadema hakina miaka 10 mbele nipo mtaniambia.Ila ni rahisi kwa mtoto wa miaka 15 kumtabiria kuishi (life expectancy) miaka 50 ijayo,mfano huu ni sawa na ACT wazalendo .
Lazima tuelewe kwamba Chadema umri wake sasa upo kileleni ,hakuna Chadema zaidi ya ile ya 2005,2006,2008,2009,2010,2011,2012,2013,2014,2015 no more Chadema badala yake kuna rise up ya chama kingine cha upinzani hii ndio principle hata ACT wazalendo itakufa tuu.
Hivyo Raia yangu ili huko Tanzania kuendelee kuwa na mfumo wa vyama vingi imara kuunganisha nguvu ni jambo lisilo kwepeka , watoto zangu Mbowe na Zitto Kabwe zingatieni hayo.
Good Day ,Tanzanians.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nina wasalimia kutoka huku kwa bwana Trump ambapo tupo huku kimajukumu,Ila tukiendelea kufuatilia yote ambayo yanaendelea nyumbani huko Tanzania.
Nimeshiriki siasa za upinzani huko Tanzania miaka ya 1991 nikiwa na akina Juliasy Miselye ,Prosper Rwegoshora,Peter Golugwe,akina Thao,Mgeta, Leo Lwekamwa. Leo Lwekamwa sasa hivi yeye yupo huku US, wakati huo tukiwa TLP.
Leo ninataka nitoe ujumbe huu kwa viongozi na wanachama wa vyama pinzani.Nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa siasa zinazoendelea sasa hivi nchini kwetu Tanzania.Hasa upande wa CCM , vyama pinzani, chadema na ACT-mzalendo.Mnapitia changamoto kadhaa poleni.Ni changamoto ambazo hata sisi tulipitia huko nyuma wakati wa Nyerere,Mwinyi na Mkapa.
Naomba leo nizungumzie kuhusu upinzani tuu.Kwa namna ninavyoamini vyama vikubwa vya upinzani Tanzania kwa sasa ni vyama viwili tuu, Chadema na ACT mzalendo mnikosoe nikikosea.
Ninataka kuwaambia viongozi wa vyama pinzani nchini Tanzania hasa Chadema chini ya mtoto wangu Mbowe na ACT mzalendo chini ya mtoto wangu Zitto.
Lazima mfahamu kwanza vyama huwa havidumu milele bali vinazakiwa,vinakuwa na hufikia muda vinakufa au vinakosa nguvu kabisa.Hii sio hiari ni kanuni (Party is formed,grow and witheraway).
Siasa za vyama hivi viwili kati ya Chadema na ACT mzalendo ni siasa za kugombea kuishi (Survival for the fittest).Chadema wapo katika kilele cha ukuaji(Grey step/Peak step),Act mzalendo ndio wanaanza ukuaji hasa baada ya kumpokea Maalimu Seif hivyo wanapambana kukuwa.
Nina rafiki zangu wapo Chadema mara zote huwa wakiniambia kwamba Chadema haiwezi kuunganisha nguvu na ACT mzalendo kwani ACT mzalendo ni chama kidogo sana.Mimi huwa nina washauri Chadema kama wanahitaji waendelee kuwepo katika midani ya siasa ni lazima waunde umoja na ACT mzalendo pia na vyama vingine pinzani katika chaguzi.
Huwa nina ambia rafiki zangu huko Chadema kwamba wasitiwe upofu na wingi wa wabunge walio nao ,hao walipatikana mwaka 2015 tuu sio guarantee ya kuendelea kuwapata katika chaguzi zijazo bila nguvu ya umoja.Hivyo kudharau vyama vingine wanavyoita vidogo sio vyema hata kidogo .Sisi tulio watangulia tunajua hayo.Nina wapa mifano kuanzia uchaguzi wa 1995 , 2000,2005,2010,2015
Mwaka 1995,NCCR ilikuwa chama pinzani kikuu chenye nguvu kipindi hicho chini ya Mbatia , Anthony Komu,Masumbuko Lamwai,Ringo Tenga,Mvungi na Mrema.
Uchaguzi wa 1995 ,Mkapa wa CCM alipata kura 4026422 sawa na asilimia 61.82 akifuatiwa na Mrema akiwa Chama kikuu cha upinzani NCCR alipata kura 1,808,616 sawa na asilimia 27.77,vikifuatiwa vyama vingine vya upinzani .Nakumbuka Mkoa wa Dar es salaam wakati ule Mrema alipata kura nyingi sana hatimaye uchaguzi ule mkoa wa Dar ulifutwa .
Miaka mitano kupita ulikuwa uchaguzi wa 2000 ,awamu ya pili ya Mkapa.Matokeo Mkapa kura 5,863,201 asilimia 71.74 ,Sasa hivi karata ilibadilika sio NCCR tena ilikuwa CUF chini ya lipumba akipata kura 1,329,077 asilimia 16, akifuatiwa na TLP baada ya Mrema kuhamia TLP kutoka NCCR ,NCCR ikawa ya Mwisho hata wabunge ikashindwa na TLP.Nakumbuka TLP waliopata wabunge 16 pia kuongoza Halmashauri ya Moshi, nakumbuka kipindi hicho msajili George Liundi alitaka kukifuta chama cha TLP kabla ya uchaguzi wa 2000 ,baada ya uchaguzi wa 2000 TLP chini ya Leo Lwekamwa na akina Thao ,Mselya,Mgeta ikawa ponapona yao.
Chama cha NCCR kilipotelea mbali naambiwa sasa hivi kina Mbunge mmoja James Mbatia.
Uchaguzi wa 2005 , Kikwete wa CCM alipata kura 9,123,952 sawa na asilimia 80.28 , akifuatiwa na CUF ya Lipumba wakati huo kura 1327125 , akifuatiwa Mbowe wa Chadema kura 668,756 asilimia 5.88
Hapo ndipo ilikuwa mwisho wa Chama cha NCCR,TLP na CUF kama vyama vikuu vya upinzani nchini Tanzania.
Uchaguzi 2010 Kikwete wa CCM alipata asilimia 62.83 na chama pinzani kilichoongoza ni Chadema mgombea wake Dr.Slaa asilimia 27.05 akifuatiwa na Lipumba CUF asilimia 8.28
Na 2015 aliongoza Magufuli wa CCM na upinzani ni ukawa Lowasa.
Hii ni mifano dhahiri ili Chadema wajue kwamba ponapona yao kama chama kikuu cha upinzani ni Umoja miongoni mwa vyama pinzani.Ndio nafasi yao ya kuendelea kuishi bila njia hiyo ni rahisi chama hicho kufa mapema kama vyama vingine namna vilivyokufa.
Wafuasi mara zote hubadilika baada ya kuona chama kimepoteza mvuto au kuzeeeka,wafuasi waliacha NCCR 2000 waka Support CUF na TLP ,waliacha TLP 2005 waka Support CUF na Chadema,2010 wafuasi waliacha CUF waka Support Chadema ,2015 ilikuwa ukawa ndio Chadema ikapata wabunge wengi wanaoringia sasa bila umoja tena wa vyama pinzani chadema mtaongea habari nyingine mara nyingi huwa nina waambia .
Hivyo kwa aina ya Siasa za sasa Chadema haipaswi kudharau kabisa chama cha ACT mzalendo kwa kutamka hawawezi kuungana.ACT mzalendo naambiwa kimeenea Zanzibar kote , bila kusahau lazima tufahamu kwamba siasa za Zanzibar ni za tofauti na bara.Zanzibari hata wasipoungana ikisimama ACT tuu uwezo wa kupambana na CCM upo mkubwa na kupata viti hata kura nyingi.
Ila huko bara Chadema na ACT mkusimama pekeenu,mtafanywa kama kwenye chaguzi za marudio (Wabunge na Madiwani) , pia serikali za mitaa.
Kwa mfano Chadema na ACT mzalendo huko bara mkikosa jimbo hata moja bila kuungana , Zanzibar ACT mzalendo itapata viti hivyo na ACT kuwa chama kikuu cha upinzani kupitia Zanzibar sababu siasa zao ni tofauti na huko bara.
Mimi nina jua kuwa Chadema kinachukia sana kukuwa kwa ACT mzalendo hasa baada ya Maalim Seif kuhamia ACT mzalendo,chuki za namna hiyo zipo sana katika siasa za upinzani .Kuhama kwa Maalim Seif kwenda ACT mzalendo ilikuwa ni sawa na kuhama kwa Mrema kutoka CCM kwenda NCCR.
Mrema akiwa CCM alikuwa na cheo cha Naibu waziri Mkuu na waziri wa wizara nchini.Wakati huo Mrema alikuwa Mrema ,Mrema kweli .Alipo hama kutoka CCM alitakiwa kwenda TLP kwa akina Leo Lwekamwa na ikatakiwa awe mwenyekiti wa TLP ,akina Leo Lwekamwa akakubali kujiuzulu na wakaenda badili jina la mwenyekiti kwa msajili wakati huo ni George Liundi hivyo kujiandaa kumpokea Mrema ili aingie TLP,wakafunga Safari hadi Moshi kumchukua Mrema.Walipofika wakapata taarifa kwamba Mrema ameshawishiwa na NCCR hivyo amejiunga na NCCR.
Akina Leo Lwekamwa waliishiwa nguvu hivyo kuanzia 1995 hadi 2000 TLP walikuwa na chuki kubwa dhidi ya NCCR ,hii ndivyo ilivyo sasa kwa Chadema dhidi ya ACT mzalendo hasa baada ya Maalim Seif kuhamia chama hicho ikiwa cha ACT mzalendo wakati Chadema wakati huo waliniambia walikuwa tayari wamerekebisha ofisi yao kubwa Makao makuu Chadema Zanzibar ipo Kikwajuni.Chadema walikasirishwa kwa kwa hoja ya kwamba Maalim kwenda katika chama kidogo ACT mzalendo ni kuvunja nguvu ya upinzani alipaswa kuja katika chama kikuu cha upinzani bara ili kiwe tena nguvu Zanzibar ,hii ni chuki kubwa dhidi ya ACT mzalendo .
Ndio maana , uchaguzi serikali za mitaa hawakuungana na kwa taarifa nilizopewa uchaguzi mnafanya mwaka huu CHADEMA hawataki kuungana.
Ukweli ni kwamba mtu mwenye umri wa miaka 60 huwezi kumpa umri wa kuishi (Life expectancy) ya miaka 50 ijayo huwa ni vigumu atakuwa aidha mzee sana hajiwezi au kufa huo ndio mfano wa Chadema kwa sasa, Chadema hakina miaka 10 mbele nipo mtaniambia.Ila ni rahisi kwa mtoto wa miaka 15 kumtabiria kuishi (life expectancy) miaka 50 ijayo,mfano huu ni sawa na ACT wazalendo .
Lazima tuelewe kwamba Chadema umri wake sasa upo kileleni ,hakuna Chadema zaidi ya ile ya 2005,2006,2008,2009,2010,2011,2012,2013,2014,2015 no more Chadema badala yake kuna rise up ya chama kingine cha upinzani hii ndio principle hata ACT wazalendo itakufa tuu.
Hivyo Raia yangu ili huko Tanzania kuendelee kuwa na mfumo wa vyama vingi imara kuunganisha nguvu ni jambo lisilo kwepeka , watoto zangu Mbowe na Zitto Kabwe zingatieni hayo.
Good Day ,Tanzanians.
Sent using Jamii Forums mobile app