Prof. Tibaijuka: Watu waliochota fedha za escrow kutoka Stanbic hawatajwi, sisi tulionewa

Hv wamiliki wa STANBIC NI WAKINA NANI....na wamilik wa mkombozi ni wakina nani?
 
Huyu bibie atulie tu, kashakula nyekundu na ndio ajali za kisiasa zilivyo kama alivyojisemea mkwere juu ya mkubwa Lowa...
 
Jinamizi la kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow bado linamsumbua mbunge wa Muleba Kusini (CCM), Profesa Anna Tibaijuka baada ya kuliibua kwenye semina ya mapambano dhidi ya ufisadi, akichongea wabunge ambao hawajaguswa.

Profesa Tibaijuka alipoteza uwaziri wa nyumba, ardhi na makazi kwenye sakata hilo baada ya kubainika kuwa aliingiziwa fedha zinazoonekana zilitoka kwenye akaunti hiyo iliyokuwa inamilikiwa kwa pamoja na Tanesco na kampuni ya kufua umeme ya IPTL.

Profesa Tibaijuka alikuwa mmoja kati ya viongozi wa ngazi ya waziri, mbunge, jaji na viongozi wa dini walioingiziwa fedha ambazo zinatokana na Sh306 bilioni zilizochotwa kwenye akaunti hiyo.

Akichangia katika semina hiyo inayolenga kuwajengea wabunge uwezo wa kupambana na ufisadi na ambayo iliandaliwa na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Ufisadi (ACFE), Profesa Tibaijuka alisema wakazi wa jimbo lake walimchagua kwa mara nyingine licha ya tuhuma za Escrow kwa sababu hawakuziamini.

Alisema fedha hizo za Escrow zilitoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kwenda benki ya Stanbic na Mkombozi, lakini cha ajabu majina ya watu waliopewa fedha kupitia benki moja yalitolewa na yale ya benki nyingine yalifichwa.

Alisema inakuwaje yeye anakuwa katika tuhuma, wakati aliyempa fedha hizo hatuhumiwi.

Watu waliotajwa kwenye sakata hilo ni wale waliopewa fedha zilizopitia benki ya Mkombozi, lakini hadi sasa wale waliopewa fedha zinazodaiwa kuwa ni taslimu kutoka Stanbic hawajatajwa.

Alisema sheria pekee yake haiwezi kufanya lolote katika mapambano dhidi ya ufisadi na hakubaliani na wabunge wanaosema kuwa hata kama mahakama imeshindwa kuthibitisha ufisadi, watuhumiwa wataifishwe mali zao.

“Sisi wabunge hatukuja kufanya kazi hiyo, tumekuja kutunga sheria ili zisaidie katika kutuongoza,” alisema.

“Ni vyema kuzungumzia unyofu wa watu kwa kuanzia katika shule, makanisa, misikiti na wabunge.”

Aliituhumu Takukuru kuwa inakubali kutumiwa kwa kuchagua kesi za kuchunguza.“Tume ya Maadili ndio usiseme,” alisema.

“Mie nimeshawahi kushtakiwa Tume ya Maadili, najua kuwa kuna mbunge mwenzetu hapa alipata fedha za Escrow, lakini kwa sababu hakuwa mzungumzaji ameondoka bungeni wala hakuna mtu anajua kama alipata. Unaona jinsi ambavyo hawa watu hawako makini,”alisema.

Mbunge wa Hanang (CCM), Dk Mary Nagu alilia na watu aliowaita wazushi kwamba wanawazushia wenzao kuchukua rushwa wakati hakuna ukweli.

Huyu mama asizungushe watu kwanza alitakiwa aombe radhi kwa Umma kupokea zile fedha kwa njia za kifisadi lakini pia azirejeshe mana hoja hapa ni kwanini yeye alichukua zile fedha??

kwa sababu hata hao aliowataja kwamba hawajachukuliwa hatua hakubadilishi yeye kutokuwa fisadi. Nafkiri Tibaijuka amesahau kwamba yeye alikuwa waziri na waziri ni kiongozi wa juu serikalini na umma.
 
'what goes around, comes around' ...sijui ndivyo wanasemaga hivyo!?
Ingelikuwa watu walishirikiana kufanya jambo jema basi ingebaki siri lakini katika ufisadi wa kubeba pesa kwenye sandarusi kujumlisha na mtifuano ndani ya chama fisadi ni wazi hawa watu tutawajua siku si nyingi na wataadhibiwa!
 
Huyu mama asizungushe watu kwanza alitakiwa aombe radhi kwa Umma kupokea zile fedha kwa njia za kifisadi lakini pia azirejeshe mana hoja hapa ni kwanini yeye alichukua zile fedha??

kwa sababu hata hao aliowataja kwamba hawajachukuliwa hatua hakubadilishi yeye kutokuwa fisadi.
Nafkiri Tibaijuka amesahau kwamba yeye alikuwa waziri na waziri ni kiongozi wa juu serikalini na umma.
Niliona juzi Temeke dereva aliyekamatwa akisafirisha wahamiaji haramu akikiri kosa mbele ya media, lakini akauliza swali la msingi kuwa aliyemkabidhi hao watu (mmiliki wa mzigo) alipandishwa kwenye gari la polisi lakini walivyofikishwa kituoni hakuonekana. Na ikagundulika kwa polisi wamemwachia kabla hajafika hapo.
Kwa maana hiyo dereve aliamini maelezo hayo yatampunguzia adhabu kama ulivyoandika hapo kwenye red.
 
Yeye anawajua majina hayo wengine waliochukulia Stanbic si awataje tu kuliko kulalamika tu.
Serikali na bunge imewogopa yeye atawaweza wapi. Hajitaki?
Mkuu hajakataa kwamba amepewa anakubali kila kitu lakini anachosema mbona waliotajwa ni wale wa Mkombozi Bank tu vipi wale waliochukua Stanbic mbona hawatajwi?Akina nani?Kama tuna nia kweli kwanini tusiwataje wote na tukawa na fare system?
 
Hivi tutatoboa kweli chini ya ccm maana ni miaka 55 tuko vilevile huduma za maji na dawa hospital vyote shida
 
Awataje yeye maana wote wanafahamiana atakua karahisisha mambo
Yeye hana mamlaka kuwataja ila mpaka hapo ametuonesha kuwavyombo vyetu hakuna lolote vina fanya kazi kwa kutumiwa tu hawafati sheria na utaratibu unavyo wataka kusema,haiwezekani watu wachote pesa huko BOT alafu waje kuwababmbikizia watu huku downstream,kibaya zaidi zilizo gawiwa mkombozi tena kwa kufata utaratibu wote ndio wanao sumbuliwa lakin huyu singa singa ambae hata hakulipa kodi na aligawa pesa nyingi sana huko stanbic hasumbuliwi,watanzania kuna maswali mengi sana ya kujiuliza hapa na kuhoji,kwanini kuna kigugumizi ktk orodha ya stanbic???huyu mama ana hoja ya msingi tusibeze
 
UJUE HAYA YOTE YANATUONESHA JAMBO HAPA,HUYU MAMA NI DHAHIRI HAUSIKI KABISA NA JAMBO HILI,KAMA ANGEKUA MUHUSIKA KAMA HAO WA STANBIC AMABO HATA MAELEZO HAWANA YA WALICHUKUA PESA HIZO KWA KAZI GANI,BASI TUNGE MSIKIA AKIKAA KIMYA LAKINI ANAZIDI KUSISITIZA HILI WA TZ TUONE MCHEZO UNAO ENDELEA

ALAFU WA TANZANIA TUNAFURAHISHA TUHUMA ZISIZO HALALI WALA UKWELI TUNABEBA MABANGO KWELI TENA ZILE ZA UZUSHI ILA AKINA RUGUMI ,STANBIC WA TANZANIA HATUHOJI.

TEAM TUNATSKA LIST YA STANBIC!!!!!!!!!!
 
Huyu mama asizungushe watu kwanza alitakiwa aombe radhi kwa Umma kupokea zile fedha kwa njia za kifisadi lakini pia azirejeshe mana hoja hapa ni kwanini yeye alichukua zile fedha??

kwa sababu hata hao aliowataja kwamba hawajachukuliwa hatua hakubadilishi yeye kutokuwa fisadi. Nafkiri Tibaijuka amesahau kwamba yeye alikuwa waziri na waziri ni kiongozi wa juu serikalini na umma.
Sasa ufisadi wake unaingiaje wakati kesha sema toka mwanzo na ukumbuke alikua mtu wa kwanza KUKUBALI hadharani kuwa kweli alipokea mchango na alipewa mchango kwa ajili ya shule,maelezo gani uliyataka??hao wengine hawana maelezo ndio mana mpaka leo wako kimya kwasababu hawakua na sababu ya kupokea izo pesa,maelezo ya kutoa hakuna
 
Yeye hana mamlaka kuwataja ila mpaka hapo ametuonesha kuwavyombo vyetu hakuna lolote vina fanya kazi kwa kutumiwa tu hawafati sheria na utaratibu unavyo wataka kusema,haiwezekani watu wachote pesa huko BOT alafu waje kuwababmbikizia watu huku downstream,kibaya zaidi zilizo gawiwa mkombozi tena kwa kufata utaratibu wote ndio wanao sumbuliwa lakin huyu singa singa ambae hata hakulipa kodi na aligawa pesa nyingi sana huko stanbic hasumbuliwi,watanzania kuna maswali mengi sana ya kujiuliza hapa na kuhoji,kwanini kuna kigugumizi ktk orodha ya stanbic???huyu mama ana hoja ya msingi tusibeze
Basi na yeye angeenda kuchukulia stanbic
 
Labda za stanbic hazikuwa za escrow ndiyo maana hawakutangazwa
pesa zilizopitia mkombozi bank zilikuwa mgao wa yule mzee wa kihaya,aliyetoa plot yake kusimika mitambo ya umeme,lilikuwa gawio la mbia katika mradi huo,na huyo mzee sijui alitembelewa na roho mtakatifu ama alikuwa hajawahi kushika pesa nyingi kwa ghafla,akaanza kuzigawa kwa ndugu,jamaa,marafiki na maaskofu,
pesa zilizokuwa stanbic nadhani na salio la wawekezaji huyo singer baada ya kuwa wamemkatia mzee wa kihaya pesa yake,
story za lumbesa inaweza kuwa uvumi tu kama ule wa magari ya washawasha 777,
anyway huyo mwekezaji inawezekana nae aliwapa takrima baadhi ya watu waliomfanikishia mambo yake,lakini haiwezekani eti yule mhindi akagawa pesa kama yule mzee wa kihaya ambae investment yake kwenye mradi ilikuwa ni ardhi peke yake
 
Back
Top Bottom