Wakuu,
Kuna sekeseke linaendelea chini kwa chini ambalo likifumuka linaweza kupelekea Prof. Muhongo kuhamishwa Wizara au kupoteza nafasi yake.
Kifupi ni kuwa jamaa kaingilia maslahi ya wakubwa na kwa sasa mambo si mambo. Tutayasikia ya kusikika muda si mrefu.
Nimeandika ili wajue tayari tumejua, tuna taarifa za ndani zaidi na tunafahamu kinachoendelea kati yetu na wamarekani.
mkuu toa taarifa kamili tena kwa uthibitisho, tunashindwa kuelewa na itachukuliwa kama umbea na porojo za kijiweni.
Njia mojawapo inayotumiwa na CIA kujipenyeza katika nchi ni kupitia miundombinu. Hawa wenzetu wana ujanja kutuzidi.SYMBION powered by CIA na project za umeme wa vijijini wapi na wapi?. Hilo ni changa la macho, tutasubiri mpaka dakika ya mwisho. Viongozi wa Tanzania wengi mbumbumbu, someni CIA proposed world order after cold war.Hali tuliyonayo Tanzania ni mbaya kuliko tunavyoifilia, nchi imefika hatua haijui hata adui wake halisi ni nani, maadui wanakumbatiwa na viongozi wenye nyadhifa nyeti kabisa, lazima tuvune mabua
hivi lini hii CCM tutairestisha ini pisi wawanawani 2015 mbali sana.
inakera sana kuona CCM kutwa kucha ni kutetea matumbo yao na sio maslahi ya wananchi
Prof Muhogo nakushauri wakikutisha itisha press conference sema kila kitu
halafu jiuzulu, hapo hapo andaa barua kabisa na itume after conference achia ngazi rudi kafundishe
CV yako inatisha huna haja kuinyenyekea CCM isiokuwa na lengo la kumkomboa Mtanzania.
Yaani Wamarekani ni majangili wa kutupwa. Si watu wazuri hata kidogo. Ukiacha barabara waliyojengwa huko kusini kwa ajili ya kurahisisha kuiba uranium yetu, miradi yao mingi ndani ya TZ iko kwenye kutusambazia virusi vya ukimwi na viwanda vyao vya kutengeneza vyandarua huko Arusha. They are evil people....
duh...pole mkuu?......
Sielewi kitu.