Prof. Muhongo kama ni speed basi anatumia mtandao wa 4G

Prof. Muhongo kama ni speed basi anatumia mtandao wa 4G

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
17,080
Reaction score
12,300
Huyu jamaa ana pumzi kinoma, baada tu ya kuapishwa break ya kwanza kwa MD wa tanesco huyo siku hiyo hiyo alifika kituo cha umeme cha Hale na Pangani akayaona ya kuonekana, mvua zinanyesha mgao uko pale pale kumbe mashine moja mbovu na TANESCO hawana hela ndio wanahangaikia mkopo kutoka Sweden. Lipo pia tatizo la walima nyanya na kabeji wanayachepusha maji.

Leo atakuwa Mtera akachungulie kabisa mwenyewe aone kama kweli wanayafunguliaga maji au mashine ni mbovu kama za hale. bravo prof wa ukweli.
 
Prof Muhongo anajua Watanzania tunataka nini na yupo tayari kufikia matarajio yetu kwa serikali. Hivyo hana muda wa mzaha. Kwake ni kazi tu.
 
Hizo habari asingeweza kuzipata kwa kupiga simu tu?
 
Hata afanyeje iyo wizara kamshikia tu naibu wake kwa sasa....
 
angeanza na service charge kuitoa tungemuelewa, kwa nini ulipie huduma ya mhudumu kukuletea chakula hotelin wakat ndo kazi yake?
 
Humjui prof. Muhongo wewe acha kubwabwaja...... Subiri akupige kazi ama bado una amini kua nae alikula hela za Escrow... hahahaha

Haijalishi hata afanye kazi vipi

uliza naibu wake ni mbunge wa wapi...ndo utaelewa
 
Prof Muhongo ana uchungu na nchi hii. Pia ni mtu ambaye anatumia vema taaluma yake. Pia ni mtu ambaye ana akili sana. Sema tu Mafisadi wakiongozwa na dalali mkuu, Reginald Mengi walitaka kuturudisha nyuma
 
Binafsi nilikia nasubir Magufuli amchague huyu jamaa kwenye uwaziri ili nianze kufanya nae kazi effectively shida yangu awe waziri mkuu ila haikuwa basi nashukuru hata hapo alipo hatatuangusha watanzania
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom