Sasa nyie kina
eddy koyola MOTOCHINI Lizaboni HAMY-D Godie mcubic monges Mwishowao Brightman Jr haa mym mnamsifiia Muhongo kwa lipi hasa aliloliafanya hapo? Yaani kutembelea shughuli zilizo chini ya wizara yake ndiyo hiyo mnayoiita "kasi"? Ukisoma hilo bandiko lako eddy utagundua kwamba kumbe tatizo hilo la mitambo ya Hale na Pangani Tannesco tayari walishaanza kulishughulikia kwa kuomba Mkopo toka Sweden, ingawa hujaweka wazi kama ni kwa serikali au mabenki ya huko sweden. sasa hapo mnamsifia Muhongo kwa lipi?
Ndiyo maana sisi wengine tunasema kwamba Magufuli hakujitayarisha kuwa Rais. Wewe unataka muelekeo wa nchi uwe wa uwekezaji kwenye viwanda, na roho ya uendeshaji wa kiwanda chochote kile duniani ni nishati ya umeme. Sasa nchi nzima ina mgao wa umeme kumbe kuna mashine mbovu inataka hela za kuikarabati, lakini Maguuli "anaokoa" hela kwenye sherehe za kupongezana wabunge na sherehe za Uhuru wa Tanganyika badala ya kuzipeleka Hale na Pangani yeye anazipeleka zikaanzishe upanuzi wa Bara bara ya Morocco! Aliposema "Tanzania ya Magufuli itakuwa ya viwanda" alimaanisha nini?
Wata wa CCM wanamwita Lowassa fisadi eti kwa kuhusika kwake kwenye Kashfa ya Richmond, hivi Serikali ilipoteza shilingi ngapi kwenye sakata la Richmond na kiasi gani kimechotwa kwenye sakata la Tegeta Escrow? Hivi mtu anayemuita mtanzania mwenzake tumbili bado tu anastahili kuwemo kwenye baraza la mawaziri la nchi yetu? Ni wangapi leo hii watavumilia Lissu akaimuita Magufuli tumbili? Kweli CCM ni ile ile!!