Prof. Muhongo ampiga dongo Zitto Kabwe(?)

Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Mhongo amesema kamwe hatafuata ushauri unaohusu gas kwa watu ambao wamehudhuria mafunzo ya wiki moja ya gas na kupata cheti cha mahudhurio 'certificate of attendance' na amekemea tabia ya watu hao kujifanya wanajua sana masuala ya gas kuliko wataalam wenyewe.

This guy is exremely naïve and paranoid! Si kweli kwama ushauri mzuri unapatikana kwa wataalamu tu.
 
Tuwe wakweli. Muhongo hajamtaja mtu. Hivyo ni hisia tu kusema amemlenga ZZK. Amlenge kwa lipi iwapo wote wanatumia nafasi zao kufukuzia dili huku wengine wakiwadanganya wananchi kuwa lao si moja?
 
So long as huu mgao ambao sio mgao lakini ni mgao ukiisha na mimi kupata umeme wa kumwaga.., I wont have problem na huyu Muheshimiwa.., as of now nina hasira sana za kuwa gizani na kutumia hiki kibatari changu ambacho na mafuta karibia yanakwisha...
 
Huyu waziri anafanya kazi akikumbana na vikwazo kila kona maana naona kila kukicha wakosoaji wake wanaongezeka. Inaonyesha ameziba mirija mingi sana ya vigogo na sasa wanatafuta namna ya kumkwamisha. Mungu amlinde dhidi ya wote wanaotaka kumkwamisha ktk juhudi zake za kutuondolea migao ya umeme isiyoisha.
 
Hivi ukitaka kumuuliza maswali huyu waziri unafanyeje ,kipindi chenyewe recoded and edited
 
kapotolo

Uko sawa kabisaaa lakini haileti maana kwa kitu usichokijua kujifunza kwa kukosoa na pili kodi katika madini haiimaninishi kuyajua madini na kimsingi ni vitu viwili tofauti ni vizuri tukaheshimu wataalam kwanza, mfano kumejengeka tabia ya wajuaji wa jinsi kama hii anayoisemea prof kuingilia hata majukumu ya kidaktari kama kutangaza kwa kusisitiza mtu kafa wakati yeye siyo daktari ama mtu fulanin kaiba wakati yeye siyo auditor, na mambo mengine mengi. wabunge wetu wetu kwa idadi kubwa hupenda sana wasikike kuliko maslahi yataifa letu nawaomba waache.
 
Last edited by a moderator:
Pia usikose kuangalia sTAR TV jumapili saa moja unusu atakuwepo Freeman mbowe na mtu mwenye hadhi yake toka ccm kuongelea Rushwa kwenye vyama vya siasa ,kipindi kinaratibiwa na YAHAYA M.
Hiyo itakuwa live!

hili neno linatumika vibaya na visivyo.
 
Tatizo la mzee nae ana dharau sana,ushauri asipokee kwa sababu hauna tija lakini sio kwa vile umetolewa na mtu ambae hajasoma petroleum geology
 
Kumbe Hakijarushwa bado. Jamani mnaoshika ITV huko mtujuze hapa waziri kasema nini?

Pamoja na mambo mengine, ametahadharisha waTZ kuhusu watu wanaojifanya wataalmu wa Gesi na Uranium kwa kuwa tu wamehudhuria kozi za mambo hayo za wiki tatu na kupata "CERTIFICATE OF ATTENDANCE", ila hawajui lolote juu ya mambo hayo!
Pia hakuna kitu kinachoitwa Mgao wa umeme (Power rationing) kwa kuwa uwezo wa kuzalisha umeme ni mkubwa kuliko hata mahitaji ya siku! hitaji la juu kabisa ni Megawati 850 lakini wanazalisha MEGAWATI 1000+, kwa hiyo kwa hali hiyo hakuna mgao!
Pia kasema EWURA na TANESCO walikuwa na mpango wa kupandisha gharama za umeme January mwakani, amewapiga STOP! kwa kuwa hawana sababu kwani hata madeni ya TANESCO serikali inawalipia!!!!!

Kasema pia ili kuondoa hiyo sura ya "mgao", inatakiwa viongozi wa TANESCO mahali mahali wawe na utaratibu wa kutoa taarifa umeme ukatikapo ama kabla ya kukatika, na kueleza sababu za kukatika! Hii kitu kweli hawa jamaa huwa hawafanyi!

La mwisho nililopata ni kwamba, haka ka sura ka "mgao" kanaonekana kuna watu wanakafurahia kwa sababu za kisiasa, kiuchumi(wana maslahi yao- business), ama chuki binafsi! yaani wanakalazimishia kaonekane kapo kumbe maskini hata hakuna mgao wa ukweli!!!!

Yangu ni hayo tu mkuu
 
pamoja na mambo mengine, ametahadharisha watz kuhusu watu wanaojifanya wataalmu wa gesi na uranium kwa kuwa tu wamehudhuria kozi za mambo hayo za wiki tatu na kupata "certificate of attendance", ila hawajui lolote juu ya mambo hayo!
Pia hakuna kitu kinachoitwa mgao wa umeme (power rationing) kwa kuwa uwezo wa kuzalisha umeme ni mkubwa kuliko hata mahitaji ya siku! Hitaji la juu kabisa ni megawati 850 lakini wanazalisha megawati 1000+, kwa hiyo kwa hali hiyo hakuna mgao!
Pia kasema ewura na tanesco walikuwa na mpango wa kupandisha gharama za umeme january mwakani, amewapiga stop! Kwa kuwa hawana sababu kwani hata madeni ya tanesco serikali inawalipia!!!!!

Kasema pia ili kuondoa hiyo sura ya "mgao", inatakiwa viongozi wa tanesco mahali mahali wawe na utaratibu wa kutoa taarifa umeme ukatikapo ama kabla ya kukatika, na kueleza sababu za kukatika! Hii kitu kweli hawa jamaa huwa hawafanyi!

La mwisho nililopata ni kwamba, haka ka sura ka "mgao" kanaonekana kuna watu wanakafurahia kwa sababu za kisiasa, kiuchumi(wana maslahi yao- business), ama chuki binafsi! Yaani wanakalazimishia kaonekane kapo kumbe maskini hata hakuna mgao wa ukweli!!!!

Yangu ni hayo tu mkuu
Muhongo 2015!
 
Kwa kweli Prof hana mfano hapa TZ. Tanesco ilikuwa imeshakuwa ni mzigo usiobebeka. Tangu enzi ya mwinyi mpaka wakati huu wa huyu jamaa anaeishi Airport mgao wa umeme na miradi ya umeme wa dharula vilishakuwa vitu visivyoepukika. Leo Prof anasema mgao haupaswi kuwepo. Hii ni ajabu kweli!!!!!!!!!!!!

Prof, as the scriptures say, you are the salt of the earth and the light of the world. Acha wahalifu na magenge yao ya kihalifu wazidi kuwa wahalifu, lakini wewe endelea kubaki nuru ya Tanzania. kama tunavyojifunza habari za akina Socretes na Pilato na wewe tutajifunza kutoka kwako tu. Mungu mbariki Prof, Mungu ibariki Tanzania
 
Prof Muhongo ameziba mianya mingi hivyo wahusika wanafanya waliwezalo aonekane hafai, nampongeza kwa kutoyumbishwa na mafisadi.
 
Tusipojenga taifa la kuheshimu taaluma za watu tutaishia kuwapeleka Mabwepande....

Asante sana Ben:

1. Tumemsikiliza Prof. na hakutaja jina la mtu endapo Zitto na yeyote kwa sababu za upambe au binafsi au kuchonganisha watu atafikiria hivyo basi ni wao ndio wenye hayo matatizo tena watakuwa wamethibitika kuwa ndio wanaosemwa maana duniani wapotoshaji wapo kila mahala. Mimi nikisema hapa kuwa kuna wapotoshaji wanasema kuwa JF ni mtandao wa usalama wa Taifa Tanzania. Halafu wewe kati ya watu zaidi ya milioni 45 (Watanzania) ukafikiria kuwa nakusema wewe basi itakuwa ni kweli kuwa wewe ndiye unayesema hayo!!Nitakuwa sina cha kukusaidia zaidi ya kuendelea kukufuatilia miendo yako ili nijue unachotafuta ni nini zaidi?




2. Prof. Sospeter amefafanua vyema alipoulizwa kuwa je, sasa tusiosoma tusitoe mawazo au tusisikilizwe; alisema la hasha, wananchi wote watoe mawazo yao kwenye kuchangia sera nzuri ya gesi lakini alisema anawazungumzia WAPOTOSHAJI tena wenye elimu ndogo ya certificates of attendance ambao amewapa onyo.

Naumuunga sana mkono huyu Waziri. Kwanza lazima taaluma za watu ziheshimiwe maana hata yeye mwenyewe hajifanyi kujua mambo ya mafuta maana hiyo si taaluma yake ambayo alibobae ndio maana anawaheshimu wataalamu wa eneo uzalishaji wa gesi na amesema watahusishwa sana. Pili kuna watu wenye elimu ndogo katika jambo hujifanya wajuaji na kupotosha ukweli ni lazima tuwamulike na kuwaseme maana ni wa hatari sana! Hii si ajabu kukuta hata form two students wakawa wasumbufu (kiujuaji)kuliko a form four or six student, au Private akawa mkali na mwenye majingambo (Kijeshi)kuliko Luteni au Captain wa jeshi ndivyo ilivyo watu wachache wenye vyeti vya chini wanaweza kujifanya kuwa wajuzi wa kila kitu na kudharau kazi anayoifanya Prof. Sospeter eti kwa vile tu wamepata mafunzo fulani ya muda mfupi au kaenda ziara mahala na kuuliza kuhusu Uranium au natural gas exploration.

Nimemsikiliza huyu mtu, nampa muda atekeleze anachosema na kuamini na nitamuhukumu baada ya kupima alipofikia katika yale anayoahidi lakini si upuuzi wa kupotosha. Mfano watu walisema kuwa alitaka tu bajeti ipite baada ya hapo nchi yote ingeingia gizani!! Upuuzi mtupu!! maana tunajua kuwa kuna utofauti kati ya umeme kukatika kwa sababu za uchakavu wa mitambo na miundombinu kwa ujumla na mgawo wa umeme kwa sababu za uchache wa umeme (megawatts) zinazozalishwa!! Na hili pia amelifafanua leo- well done!

Huyu jamaa kweli si mwanasiasa hata utamsikia utofauti wake na mtu anayetaka kujiingiza katika malumbano yasiyo na tija. Nilifurahia jibu alilotoa kuwa hawana mkakati wa kuwadhibiti wapotoshwaji bali wao wataendelea kuhakikisha kuwa wananchi wanapata umeme wa uhakika na hayo ndiyo tunayatafuta ukiongezea kuwa uwe ambao tunaweza kumudu gharama zake.
 
Back
Top Bottom