Prof. Muhongo ampiga dongo Zitto Kabwe(?)

Muhongo 2015!


HAKUNA KITU HUYU NI MSOMI MTENDAJI ANAYEPENDA KUONA RESULTS. YEYE MWENYEWE NINA HAKIKA HATAKI KABISA HAYA MAMBO YA SIASA. Ningetamani Semunyu amuulize hilo swali kipindi kijacho tusikie. Sitashangaa akisema kuwa yeye si mwanasiasa. Kweli sasa tunaona umuhimu zaidi wa kutenganisha ubunge na uwaziri kwenye katiba tunayoitengeneza!!!
 
Tatizo la mzee nae ana dharau sana,ushauri asipokee kwa sababu hauna tija lakini sio kwa vile umetolewa na mtu ambae hajasoma petroleum geology

kama ana dharau,asingesema atapeleka rasimu ya sera ya gesi kwa kwa ajili ya kupata maoni kutoka kwa makundi yote ya watumiaji wa gesi bila kujali elimu yao,atapeleka pia kwa vyuo vinavyofanya tafiti,kwa wataalamu mbalimbali,miji mikubwa yote yenye viwanda dar,mwanza na arusha.

kama ana dharau,nahisi itakuwa kwa wale wanaomdhihaki...au walio kwenye payroll ya kumdhihaki...
 
Tusipojenga taifa la kuheshimu taaluma za watu tutaishia kuwapeleka Mabwepande....

Hivi Chenge si mtaalamu, ni lini mlimdharau, nipe matokeo ya kumheshimu.
kwa kuwa huwezi sema, nakwambia amewatia ....
 
kapotolo

Uko sawa kabisaaa lakini haileti maana kwa kitu usichokijua kujifunza kwa kukosoa na pili kodi katika madini haiimaninishi kuyajua madini na kimsingi ni vitu viwili tofauti ni vizuri tukaheshimu wataalam kwanza, mfano kumejengeka tabia ya wajuaji wa jinsi kama hii anayoisemea prof kuingilia hata majukumu ya kidaktari kama kutangaza kwa kusisitiza mtu kafa wakati yeye siyo daktari ama mtu fulanin kaiba wakati yeye siyo auditor, na mambo mengine mengi. wabunge wetu wetu kwa idadi kubwa hupenda sana wasikike kuliko maslahi yataifa letu nawaomba waache.

Pamoja na maelezo marefu naomba nikukumbushe kuwa wanaolalamika kuhusu umeme sio wabunge ni wananchi, wabunge ni vipaza sauti vya wananchi.

Pili naomba ufafanuzi hapa; kama muhongo anasema hawezi kusililiza mawazo ya wenye certificate of participation iweje tena atumbie amepeleka rasimu kwa wananchi ili watoe maoni yao kuhusu sera ya gas kabla haijawa sheria?

Anakataa ushauri wa watu wenye access na information anasubiri maoni ya watu ambao hata umeme hawana. Prove kwamba hii sio contradiction.

Prof. kaniangusha bana, ameulizwa jinsi tanesco ilivyojiandaa kupambana na hujuma akasema wao hawapigi propaganda ni vitendo zaidi, badala ya angalau kutumegea kidogo jinsi walivyojipanga, lakini baadaye akaanza kutaja njia mpya za umeme wanazojenga (kwa maelezo yake). Hili jibu nalo ni la kimkakati kama ambavyo angejibu swali la kwanza. Contradiction nyingine.

Pia amezungumzia huduma za tanesco kwa kusema eti zimekuwa bora zaidi, akatoa mfano kwamba sasa hivi kama umeme utakatika meneja wa eneo husika lazima atangazie eneo lake na kama umeme unakatika ghafla basi lazima awaombe radhi waathirika.

Acha tu prof. Apewe ushauri bana
 
Last edited by a moderator:
U-Prof...haukupewa u deserved to be and i consider u as an ASSET na mwenye utashi wa kusimamia kazi kimisingi yake, tenda kazi achana na midomo ya wapenda short-cut. Mungu akujaze nguvu na hekima.
 
Mikataba mibovu tuliyo nayo kwenye madini ndio 2tegemee mpaka kwenye gas na mafuta! hivi waziri wa nishati na madini kuna umuhimu gani wa kuchimba uranium? wakati hatuwezi kuepuka madhara yake? madini athari 2meshindwa kushughulikia? tafadhari 2naipeleka wapi nchi ye2 yenye resources za kutosha? kuwa makini waziri hiyo secta ni muhimu kwa uchumi wa tanzania!!
 
Huyu mzee anaonekana ni mchapakazi, kwanza siyo mwanasiasa na anaonekana kumtetea mtz wa kawaida!
 
waziri wetu una mpango gani au serikali yako ina mpango gani wa kupeleka umeme kwenye baadhi ya vijiji mikoani ambako hawajawahi kuona umeme unafananaje katika maisha yao? its amazing 2012 kuna watu hawajawahi kuona taa ya umeme maishani mwao
 
Prof. Muhungo amejaribu kuonyesha vision yake kuhusu umeme na gas. Tumpe muda kabla ya kumfanyia evaluation. Kumbukeni siasa zetu zilivyoiharibu TANESCO.
 
Asante sana Ben:

1. Tumemsikiliza Prof. na hakutaja jina la mtu endapo Zitto na yeyote kwa sababu za upambe au binafsi au kuchonganisha watu atafikiria hivyo basi ni wao ndio wenye hayo matatizo tena watakuwa wamethibitika kuwa ndio wanaosemwa maana duniani wapotoshaji wapo kila mahala. Mimi nikisema hapa kuwa kuna wapotoshaji wanasema kuwa JF ni mtandao wa usalama wa Taifa Tanzania. Halafu wewe kati ya watu zaidi ya milioni 45 (Watanzania) ukafikiria kuwa nakusema wewe basi itakuwa ni kweli kuwa wewe ndiye unayesema hayo!!Nitakuwa sina cha kukusaidia zaidi ya kuendelea kukufuatilia miendo yako ili nijue unachotafuta ni nini zaidi?




2. Prof. Sospeter amefafanua vyema alipoulizwa kuwa je, sasa tusiosoma tusitoe mawazo au tusisikilizwe; alisema la hasha, wananchi wote watoe mawazo yao kwenye kuchangia sera nzuri ya gesi lakini alisema anawazungumzia WAPOTOSHAJI tena wenye elimu ndogo ya certificates of attendance ambao amewapa onyo.

Naumuunga sana mkono huyu Waziri. Kwanza lazima taaluma za watu ziheshimiwe maana hata yeye mwenyewe hajifanyi kujua mambo ya mafuta maana hiyo si taaluma yake ambayo alibobae ndio maana anawaheshimu wataalamu wa eneo uzalishaji wa gesi na amesema watahusishwa sana. Pili kuna watu wenye elimu ndogo katika jambo hujifanya wajuaji na kupotosha ukweli ni lazima tuwamulike na kuwaseme maana ni wa hatari sana! Hii si ajabu kukuta hata form two students wakawa wasumbufu (kiujuaji)kuliko a form four or six student, au Private akawa mkali na mwenye majingambo (Kijeshi)kuliko Luteni au Captain wa jeshi ndivyo ilivyo watu wachache wenye vyeti vya chini wanaweza kujifanya kuwa wajuzi wa kila kitu na kudharau kazi anayoifanya Prof. Sospeter eti kwa vile tu wamepata mafunzo fulani ya muda mfupi au kaenda ziara mahala na kuuliza kuhusu Uranium au natural gas exploration.

Nimemsikiliza huyu mtu, nampa muda atekeleze anachosema na kuamini na nitamuhukumu baada ya kupima alipofikia katika yale anayoahidi lakini si upuuzi wa kupotosha. Mfano watu walisema kuwa alitaka tu bajeti ipite baada ya hapo nchi yote ingeingia gizani!! Upuuzi mtupu!! maana tunajua kuwa kuna utofauti kati ya umeme kukatika kwa sababu za uchakavu wa mitambo na miundombinu kwa ujumla na mgawo wa umeme kwa sababu za uchache wa umeme (megawatts) zinazozalishwa!! Na hili pia amelifafanua leo- well done!

Huyu jamaa kweli si mwanasiasa hata utamsikia utofauti wake na mtu anayetaka kujiingiza katika malumbano yasiyo na tija. Nilifurahia jibu alilotoa kuwa hawana mkakati wa kuwadhibiti wapotoshwaji bali wao wataendelea kuhakikisha kuwa wananchi wanapata umeme wa uhakika na hayo ndiyo tunayatafuta ukiongezea kuwa uwe ambao tunaweza kumudu gharama zake.

Mkuu hapa umenyoosha mambo vizuri sana. Na umenikumbusha niliwahi kumsikiliza Jenerali Ulimwengu wakati wa mjadala wa Katiba mpya, uleeee wa wanza kwanza. Alikuwa anashangaa siasa zetu zilivyo za ajabu. Aliuliza inakuwaje wanapokutana wakuu wa Wilaya ambao ni maaskari wastaafu walioteuliwa kuwa Wakuu wa Wilaya wanapokuwa na vikao, maana wengine ni ma-Luteni, wengine ma- Captain wastaafu sijui ma Major wakichanganyika na Raia wengine nk. Sasa heshima inakuwaje humo ndani ya Kikao? (sijamnukuu 100% lakini ndiyo hoja aliyoijenga).
Sasa Prof. Muhongo atachakaa muda si mrefu pale atakapopewa vikwazo na Mkuu mmoja wa Mkoa au Wilaya. Labda awe amewekeana special MoU na Mkuu wa nchi.
Hakuna shaka kabisa kwamba Siasa mbovu ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo. Nchi yoyote duniani ukiona wanasisa wake ndiyo wanaolipwa mishahara minono kuliko watu wa taaluma ujue hiyo nchi haiwezi kuendelea. It simply is practicing silly Politics, which will take the country nowhere! Badala yake uchumi ni lazima udidimie na maisha ya wananchi wake hayataweza kuwa mazuri hata siku moja.
Nchi ya namna hiyo utakachoona ni viongozi kutaka maendeleo ya vitu vichache vya kujiletea sifa binafsi, kujenga barabara, madaraja, majumba makubwa nk. huku wakiua vile vilivyokuwepo kabla hawajaingia madarakani. That is what I call silly politics.
 
Kwa kweli Prof hana mfano hapa TZ. Tanesco ilikuwa imeshakuwa ni mzigo usiobebeka. Tangu enzi ya mwinyi mpaka wakati huu wa huyu jamaa anaeishi Airport mgao wa umeme na miradi ya umeme wa dharula vilishakuwa vitu visivyoepukika. Leo Prof anasema mgao haupaswi kuwepo. Hii ni ajabu kweli!!!!!!!!!!!!

Prof, as the scriptures say, you are the salt of the earth and the light of the world. Acha wahalifu na magenge yao ya kihalifu wazidi kuwa wahalifu, lakini wewe endelea kubaki nuru ya Tanzania. kama tunavyojifunza habari za akina Socretes na Pilato na wewe tutajifunza kutoka kwako tu. Mungu mbariki Prof, Mungu ibariki Tanzania

Nimeona nikuwekee hii kitu ujipime wewe na huyo muhongo mnafiti namna gani.

“A word to the wise ain't necessary, it's the stupid ones who need the advice.” by bill cosby.
 
Ebu badili heading yako mwenzio nikaenda ITV nkakuta mziki umeniboa
Ila nashukuru kwa kunikumbusha icho kipindi maana uyu mheshimiwa huwa namkubali sana he is a professional not a politician
kuwa waziri ni sifa tosha ya kukufanya kuwa mwanasiasa maana cheo chenyewe ni cha kisiasa. i only say, within politicians are professionals.Vilevile muwe makini na huyu profesa asiyependa kushauriwa maana mafuta na gas ni mali ya watanzania na ajue watanzania si wote wamesoma na waliosoma wote hawajasoma kuhusu miamba. lakini wanao uhuru na haki kikatiba kuhoji mambo yanayoendelea. jiulize kama mwili wote ungekuwa jicho sikio lingekuwa wapi? ajue hata aliyemteua si mtaalam wa gesi je nae asihoji?watanzania lini tutaacha kuchukulia mambo kishabiki tukaanza kuhoji?
 
Profesa aelewe kwamba si kila mtu atakuwa mtaalam wa kila kitu. Lakini hali hii haimuondolei yeyote yule haki ya kutoa maoni. Professa elewa kwamba watu wanao uhuru hata chini ya katiba ya sasa ya kutoa maoni kuhusu mambo yaendavyo katika nchi yao. Hii ni "fundamental right" ya kila raia, mtaalam na asiye mtaalam. Ninachokiona kwa profesa ni "intellectual arrogance."

Prof. Muhungo elewa kwamba ni juu yako na "the so called wataalam" kutafsiri na kuweka katika lugha ya kitaalam yale ambayo raia wa kwaida anayatoa kama maoni yake.

Prof. ndio maana kuna hata kura ya maoni ambayo inawahusisha wataalam na hoi hahe kama sisi. Nchi hii na rasilimali zake ni kwa wote na sio kwa wataalam. We are not children ambao wazazi watusemee.

Kiongozi tena mwenye hadhi ya Waziri anatakiwa kuelewa mambo haya na hasa lugha anayotumia kwa umma.

Nampenda Mbunge Msigwa anaposema " Anapozungumza Profesa huoni tofauti na mtoto wa darasa la pili". Tuweke mbali ushabiki wa kisiasa na tukubali "constructive criticism". There is no one with a monopoly of ideas on how to run the national economy. Certainly it cannot be the so called experts who have put this country in a hopeless situation through dubious deals and agreements signed as related to the exploitation of our mineral wealth.

By the way professor where are the Tanzanian experts with the necessary experience in the gas sector, anyway? Book knowledge, oh come on professor, you are not serious! Aren't we sailing in the same boat?

Good luck!
 
Profesa aelewe kwamba si kila mtu atakuwa mtaalam wa kila kitu. Lakini hali hii haimuondolei yeyote yule haki ya kutoa maoni. Professa elewa kwamba watu wanao uhuru hata chini ya katiba ya sasa ya kutoa maoni kuhusu mambo yaendavyo katika nchi yao. Hii ni "fundamental right" ya kila raia, mtaalam na asiye mtaalam. Ninachokiona kwa profesa ni "intellectual arrogance."

Prof. Muhungo elewa kwamba ni juu yako na "the so called wataalam" kutafsiri na kuweka katika lugha ya kitaalam yale ambayo raia wa kwaida anayatoa kama maoni yake.

Prof. ndio maana kuna hata kura ya maoni ambayo inawahusisha wataalam na hoi hahe kama sisi. Nchi hii na rasilimali zake ni kwa wote na sio kwa wataalam. We are not children ambao wazazi watusemee.

Kiongozi tena mwenye hadhi ya Waziri anatakiwa kuelewa mambo haya na hasa lugha anayotumia kwa umma.

Nampenda Mbunge Msigwa anaposema " Anapozungumza Profesa huoni tofauti na mtoto wa darasa la pili". Tuweke mbali ushabiki wa kisiasa na tukubali "constructive criticism". There is no one with a monopoly of ideas on how to run the national economy. Certainly it cannot be the so called experts who have put this country in a hopeless situation through dubious deals and agreements signed as related to the exploitation of our mineral wealth.

By the way professor where are the Tanzanian experts with the necessary experience in the gas sector, anyway? Book knowledge, oh come on professor, you are not serious! Aren't we sailing in the same boat?

Good luck!

prof amesema rasimu ya sera ya gesi wataipeleka kupata maoni kwa wananchi bila kujali elimu na kwa wataalamu pia ,vyuo mbalimbali n.k...sasa hapendi kupata ushauri katika muktadha upi? kama kupiga dongo la cheti cha mahudhurio ya wiki moja,hicho ni kijembe kwa wale wanomdhihaki...kikundi cha wanaomdhihaki(kama ukiwa kwenye nafasi yake ,hata wewe ungefanya hivyo)...na walengwa wa kijembe hicho wanajijua...wewe vipi inakuumizaje? pilipili usiyoitafuna,inakuwasha vipi? kama angesema hatatoa nafasi kwa watanzania kuchangia kuhusu rasimu, ungetakiwa ikuume na si kijembe kidogo alichotoa kwa watu wanaokesha kudhihaki kazi anazofanya kwa kuwa wao wanajiona wamebobea kwenye sekta hii ya madini na wanamwona waziri ni mtu wa kuja...tafuteni darubini muone mbali kama macho hayatoshi....
 
kuwa waziri ni sifa tosha ya kukufanya kuwa mwanasiasa maana cheo chenyewe ni cha kisiasa. i only say, within politicians are professionals.Vilevile muwe makini na huyu profesa asiyependa kushauriwa maana mafuta na gas ni mali ya watanzania na ajue watanzania si wote wamesoma na waliosoma wote hawajasoma kuhusu miamba. lakini wanao uhuru na haki kikatiba kuhoji mambo yanayoendelea. jiulize kama mwili wote ungekuwa jicho sikio lingekuwa wapi? ajue hata aliyemteua si mtaalam wa gesi je nae asihoji?watanzania lini tutaacha kuchukulia mambo kishabiki tukaanza kuhoji?
hapendwi kushauriwa katika lipi ?
prof amesema rasimu ya sera ya gesi wataipeleka kupata maoni kwa wananchi bila kujali elimu na kwa wataalamu pia ,vyuo mbalimbali n.k...sasa hapendi kupata ushauri katika muktadha upi?
kama kupiga dongo la cheti cha mahudhurio ya wiki moja,hicho ni kijembe kwa wale wanomdhihaki...kikundi cha wanaomdhihaki(kama ukiwa kwenye nafasi yake ,hata wewe ungefanya hivyo)...na walengwa wa kijembe hicho wanajijua...wewe vipi inakuumizaje? pilipili usiyoitafuna,inakuwasha vipi? kama angesema hatatoa nafasi kwa watanzania kuchangia kuhusu rasimu, ungetakiwa ikuume na si kijembe kidogo alichotoa kwa watu wanaokesha kudhihaki kazi anazofanya kwa kuwa wao wanajiona wamebobea kwenye sekta hii ya madini na wanamwona waziri ni mtu wa kuja...tafuteni darubini muone mbali kama macho hayatoshi....
 
Zitto tusikilize ushauri wake wa nini wakati alishauri nchi inunue haraka mitambo ya Dowans la sivyo nchi itaingia gizani wengine tulianza kumwamini... Loh: Kumbe mgao ulikuwa wa kutengeneza!

Nani alikuwa nyuma yako Zitto ukatusaliti Watanzania bila hata huruma! Shukuru sana uko Tanzania, watu wa aina yako China ungeshatiwa kitanzi.
 
Anasema hakuna haja ya kuwa na mambo ya umeme wa dharura kwani ndio chanzo cha ufisadi. Asisitiza hakuna na hakutokuwa na mgao wa umeme. Asema kila mtu anaongelea mambo ya gesi,hata wasiokuwa na utaalamu wanaongelea kama wataalamu na hivyo wanapotosha umma. Kwa hayo na mengine mengi angalia ITV saa 3 usiku leo,kipindi cha dakika 45.

Ahadi za umeme.jpg Ahadi za umeme.jpg Ahadi za umeme.jpg Ahadi za umeme.jpg

Ataongea sana huyu mzee lakini udhaifu hupo palepale!
 
Muhongo huwa namkubali but sometimes nakuwa na wasi wasi naye!!! ngoja kwanza ije report ya Ngwiliz may be !!! hiz dauti nilizokuwa nazo kwake zinaweza kuisha
 
Back
Top Bottom