Tangu jana kumekuwa na taarifa za moja kati ya makada maarufu na wenye ushawishi ndani ya CCM Prof.Mark Mwandosya kuhamia upinzani, taarifa hizo zimekuwa zikienea kwa kasi sana na kuchagizwa vilivyo na vibaraka wa propaganda za CHADEMA na UKAWA bwana Yeriko Nyerere na wenzake.
Baada ya kuendelea kuzagaa kwa taarifa hizo nimeamua kufanya uchunguzi wangu binafsi dhidi ya madai hayo lakini nilichoambiwa na mmoja kati ya watu wa karibu sana wa Prof.Mwandosya na familia yake ameniambia kuwa PROFESA mara kadhaa amekuwa akihojiwa na watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari pamoja na baadhi ya wanachama na makada waandamizi wa chama amekuwa akijibu na kusisitiza kuwa HANA MPANGO WA KUHAMA CCM.
Aidha duru za udadisi zinaeleza kuwa PROFESA kwa sasa yupo nchini MAREKANI katika shughuli zake binafsi.
Kwa kuwa wakati ni ukuta nadhani tusubiri tuone ataamua nini, kwenda kujivua nguo upinzani kama SUMAYE na mwizi mwenzie LOWASSA au ataendelea kulinda heshima na utu wake akiwa ndani ya CCM.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU BARIKI UCHAGUZI
MUNGU MUONGEZE PROFESA MWANDOSYA KATIKA KUTOA MAAMUZI YAKE
AMEN.
Andiko hili sijaelewa lina dhumuni gani;
1. Kutujulisha kuwa Mwandosya anahamia upinzani?
2. Kuwasema vibaraka wa Chadema/UKAWA kuwa wanaeneza uongo?
3. Kuonyesha kuwa Mwandosya hana mpango wa kuhamia upinzani na Mungu amtie nguvu asifanye maamuzi hayo?
4. Kumtisha Mwandosya kuwa akihamia upinzani atajidhalilisha kwa sababu ukihamia upinzani unakuwa mpumbavu na lofa?
5. CCM ina wasiwasi kumpoteza kada mwingine maarufu na hivyo kuzuia woga wa kuendelea kuonekana kuwa ni chama kilichochokwa?
Nina maswali mengine mengi najiuliza sijapata jibu, ebu tupe dhumuni hasa ni nini