Prof. Maghembe amekalia kuti kavu

Katika siku zote leo ndio nimekuona kichwa! hongera sana mkuu

hata mimi nimeshangaa ile taarifa ya kuachiwa kwa mifugo bila masharti yoyote
 
Mkuu wangu umesema nilichokuwa nataka kusema...huh ulikuwa ni mzigo toka enzi na enzi...na kama mukulu alipitia majina ya mawaziri wote na rekodi zao za utendaji wa Kazi...Basi kwa Magembe inawezekana alipigwa kipapai akampa tu Kazi bila kujijua.

Bwana yule ni mzigo na utaendelea kuwa mzigo popote pale atakapopelekwa.

Kila mtu ana jinsi Mungu wake alivomuumba ila ikifika mtu unakuwa hata mvivu kuongea tena waziri...inatia kinyaa



Magu hayuko makini katika uteuzi wake na haya ndio matokeo yake.

Historia ya Maghembe alikuwa haijui?Huyu si alikuwa mmoja wa mawaziri mizigo enzi za Kikwete?Haya alikuwa hayajui wakati anampa uwaziri?

Magu nae ni tatizo tena kubwa tu
 
Na
nashauri huyu akitumbuliwa basi wizara achiwe katibu mkuu, mawaziri hawana tija tena kila siku wanaboronga.
 
Pia Mwambie Jpm Wakati Analishughulikia Hili Asilahau Na Issue Ya Yule Alieuza Twiga Wetu.
 
Tatizo ni chama cha ccm wala sio Maghembe, Magufuri atapata shida sana kwenye haya mapambano atajikuta anapambana na chama chake
Yaan ni shida akitumbuliwa maghembe anakimbilia kwa kinana Lumumba
 
Hatua ya proff maghembe inashangaza. Eneo hilo linafahamika kuvamiwa na wafugaji wanyarwanda wa jamii ya kitutsi. Wanatoa rushwa kwa vigogo na huwafanyia wenyeji vitendo vya kinyama ikiwa ni pamoja na kufanya mauaji ya wale wenye ujasiri kuwapinga. Uamuzi wa proff yafaa kuchunguzwa kama ni kwa manufaa ya nani.
 

Yule jamaa ni zigo hasa sijui kwa nin rais alimteua
 
Sijawai kukuunga mkoni lakini kwa ili nakunga magembe hafai kwenye sekta ya Utali... kuna sakata linafukuta lingine la wadau wa UTALI KANDA YA KASKAZINI.. taarifa zimenifikia mezani kwangu hapa kwenye chumba cha habari nazifwatilia kwa ukaribu
 
Ni aibu sana kwa wote waliotaka kuikwamisha operesheni ya kuwadaka maharamia wa meno ya tembo....

Binafsi napendekeza hii wizara wawape watu wa maliasili wenyewe,watafute mhifadhi mmoja ambaye ni mwaminifu apewe hii wizara,mambo ya ujangili yataisha endapo wakiwezeshwa.
Mfano mmoja kuna mhifadhi alikuwa ANAPA akahamishwa kwenda TARANGIRE baadae KINAPA,akiwa TARANGIRE alifanya mambo makubwa sana hadi kuchukua chuma na kuingia doria mwenyewe na majangiri akayakamata.
Huyu ni mfano mmoja wapo na huwa hana mzaa.
 
Maghembe Alikuwa Katavi Wiki Iliyopita Kwenye Deals
Deal gani mkuu, inaonekana mzee anakula migao kutoka kwa matajiri ila najiuliza wale wanyarwanda tulioambiwa na Manyerere Jackton kwamba ndio waliingiza mifugo yao hifadhini kutokea rwanda walimpa nini Waziri hadi akamfuta kazi mwenzake?
 
Magu hayuko makini katika uteuzi wake na haya ndio matokeo yake.

Historia ya Maghembe alikuwa haijui?Huyu si alikuwa mmoja wa mawaziri mizigo enzi za Kikwete?Haya alikuwa hayajui wakati anampa uwaziri?

Magu nae ni tatizo tena kubwa tu

Tatizo asingemteua. Mungesema kanda ya kaskazini ameisusa. Huyo ndiye alionekana anauafadhari. Waliobaki makanjanja chagadema fullstop
 
Wahuni na majizi kama hao wahamie kwa watetea mafisadi chadema
 
Huyo mtu kafukuzwa lini? Unaonekana mbulumundu kukimbilia kuandika usichokijua.... huyo amesimamishwa kazi.....

Naona safari hii ampe Leonidas Gama au siyo?
Hivi n8 kwamba kwa vile tu upo chadema ama nini?
 
Tatizo asingemteua. Mungesema kanda ya kaskazini ameisusa. Huyo ndiye alionekana anauafadhari. Waliobaki makanjanja chagadema fullstop
Sio kweli kaskazini hakukuwa namna ya kumkwepa kwa kuwa CCM alibaki yeye tu majimbo mengne yakienda upinzani,kingne naona mkulu alikuwa anabalance angalau dini kulikuwa hakuna namna ya kumkwepa. Unapozungumzia kaskazini hasa kisiasa sanasana tunaongelea Arusha, Kilinjaro na Manyara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…