Katika hotuba yake ya kwanza amezungumzia Kilimo cha umwagiliaji kama ndio kipaumbele chake katika kutimiza majukumu yake katika wizara ya maji.
Swali langu, toka lini kipaumbele cha wizara ya maji ni kilimo cha umwagiliaji? Kilimo cha umwagiliaji ni kipaumbele cha wizara ya kilimo kimkakati.
Wizara ya maji tunahitaji utwambie tutapataje maji safi na salama . Kwani hujui ni kiwango gani cha wanchi hawana maji salama?
Hicho sio cheo cha kisiasa.
Dr. Mkumbo inawezekana amechemka kukubali kufanya kazi katika serikali kinyumena maneno yake ya awali.
Lakini Wizara ya Maji kuweka kipaumbele cha kwanza kuwa kilimo cha umwagiliaji katika taifa linalotegemea kilimo si kuchemka.
Wizara za Kilimo na Maji zinatakiwa kushirikiana kuhakikisha wakulima wanapata maji kuendesha kilimo cha umwagiliaji.
Ili kuweza kusambaza maji nchi nzima, serikali inahitaji fedha.
Kilimo ni biashara. Kimsingi, serikali inaweza kutumia kodi inayopata katika kilimo kusaidia kusambaza maji kwa wakulima.
Maji haya yakitumika vizuri na kuzalisha, uchumi utapanda na fedha za kusambaza maji zaidi zitapatikana.
Dr. Mkumbo kuna mengi amekosea na atakosea.Msemeni kwa hayo.
Mkitaka kumsemahata kwa yasiyostahili, hata mtakapomsema kwa yanayostahili mtaonekana ni kawaida yenu kumpinga mtu anayefanya kazi na serikali katika yote.
Zaidi,inabidi watu waelewe kwamba kilimo cha umwagiliaji hakihitaji gharamakubwa ya kusafisha maji (treatment plants). Kimsingi unawezakutafuta mito na kuvuna maji ambayo hayajasafishwa kwa ajili ya kilimo.
Maji safina salama ninavyoelewa mimi -ondoa habari za visima visivyo na uhakika wa usafi wa water table- ni lazima yawe treated, kitu ambacho nchi yetu kufanya priority kwa watu ni habari ya kinyumenyume.