TheDreamer Thebeliever
JF-Expert Member
- Feb 26, 2018
- 2,490
- 3,534
Habari wadau!
Leo nimecheka sana baada ya Kabudi kupewa nafasi ya kujibu hoja ya mbunge mmoja aliyeuliza kwamba kwa nini mikataba ya madini isiwekwe wazi kama ilivyoanishwa katika sheria ambayo alinukuu mpaka kifungu cha sheria kinachoitaka serikali kuchapisha mikataba ili watu waisome.
Nilistaajabu kusikia prof akisema hilo swala haliwezekani, dada alipoanza kunukuu tu kifungu cha sheria ndipo professor akamkatisha na kusema kwamba ana first class ya sheria yaani kama kumwambie vile utanambia nini .
Proffesor ameshindwa kujibu hoja na kujivunia first class yake na kusahau hizo first class kama zake tunazo nyingi tu huku mtaani zimejaa zinaendesha bodaboda.
Kitu alichopaswa kufanya Prof ni kujibu hoja ya mbunge mwenzake sio kumtambia kwamba ana first class,first class yake imetusaidia nini watanzania katika kutatua changamoto zetu? Leo migodi mingi inafungwa mfano Williamson Diamond ,Buzwagi yamebaki makombo tu ,wazama wa maeneo ya migodi wana maisha duni balaa.
wananchi wanataka kujua uwazi wa mikataba ila unapotaka kugusia swala la kuweka wazi mikataba utashangaa watu macho yanawatoka kama nini.
Binafsi sidhani kama Kabudi ni mtu sahihi kwenye nafasi ya uwaziri anaoutumikia kwa sasa ,mama anahitaji kupata mtu sahihi wa kufanya majukumu nyeti kama haya.
Leo nimecheka sana baada ya Kabudi kupewa nafasi ya kujibu hoja ya mbunge mmoja aliyeuliza kwamba kwa nini mikataba ya madini isiwekwe wazi kama ilivyoanishwa katika sheria ambayo alinukuu mpaka kifungu cha sheria kinachoitaka serikali kuchapisha mikataba ili watu waisome.
Nilistaajabu kusikia prof akisema hilo swala haliwezekani, dada alipoanza kunukuu tu kifungu cha sheria ndipo professor akamkatisha na kusema kwamba ana first class ya sheria yaani kama kumwambie vile utanambia nini .
Proffesor ameshindwa kujibu hoja na kujivunia first class yake na kusahau hizo first class kama zake tunazo nyingi tu huku mtaani zimejaa zinaendesha bodaboda.
Kitu alichopaswa kufanya Prof ni kujibu hoja ya mbunge mwenzake sio kumtambia kwamba ana first class,first class yake imetusaidia nini watanzania katika kutatua changamoto zetu? Leo migodi mingi inafungwa mfano Williamson Diamond ,Buzwagi yamebaki makombo tu ,wazama wa maeneo ya migodi wana maisha duni balaa.
wananchi wanataka kujua uwazi wa mikataba ila unapotaka kugusia swala la kuweka wazi mikataba utashangaa watu macho yanawatoka kama nini.
Binafsi sidhani kama Kabudi ni mtu sahihi kwenye nafasi ya uwaziri anaoutumikia kwa sasa ,mama anahitaji kupata mtu sahihi wa kufanya majukumu nyeti kama haya.