Prof. Ibrahim Lipumba atangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti wa CUF Taifa

:flypig::flypig:

siasa za maji taka ......... ni bora kuwa mgombea binafsiiiii

hivi vyama uchwaraaaaaaaa.............

waongoooooooooo..........

bora kuachanaaaaaaa na ccm.......

si cuf waongoooooooo.........

si ukawaaa waoooongoooooooooooooooooooooooooo....
 
Nyerere alitabiri upinzani wa kweli utatoka CCM . Baada ya Lowassa kutoka CCM na kuhamia upinzani wa kweli wale wapinzani feki kama lipumba na Slaa wamelala mbele kupisha upinzani wa kweli wa CCM

Mafuriko hauwezi kuyazuia kwa mkono
 
Mbowe amewauza wenzake. Lipumba alishiriki kila kitu, lakini hakujua kama wameuzwa. Sasa ameujua mchezo wote, ulitaka aendelee kushiriki dhambi?

Hayo ni matusi kwa CUF na wanachama wao. Wamekuwa wakikaa vikao ndani ya chama kuangalia ushiriki wao kwenye UKAWA uweje. Kama walimwachia Mwenyekiti ndie aangalie maslahi yake kwenye ushiriki basi chama chao ndio cha kulaumiwa sio Mbowe tena
 
Huyo profesa gani asiyeweza kutathmini hali ya siasa ilivyo? Yaani umepigana kutetea katiba ya wananchi, hadi wale walioipinga wamekuelewa na wameamua kurudi upande wako, wewe unawakataa kisa walikupinga hapo awali? Badala ya kujipongeza kwa kugeuza mawazo ya wale waliokupinga awali nasasa ni wenzako na wakotayari kuondoa CCM na ubabe wake wa kulazimisha katiba yao na sasa kuanza mchakato mpya wa katiba ya Warioba wewe unaona bora utoke???? sasa kampeni uliyokuwa unafanya ni ya kuhifadhi waliokuelewa toka mwanzo tu, hukuwa na haja ya kuwabadili wasioelewa toka mwanzo ili waelewe maana na rasimu ya Warioba na kuwashawishi wakuunge mkono???Hiyo siyo sababu unayosema sasa mimi sikubaliani nayo. Mi nahisi sababu inatoka msikitini kwamba huwezi mpigia kampeni mgombe wa dini nyingine! Huo ni udini! sioni sababu nyingine ambayo unashindwa kuwaeleza wafuasi wako! Na kwa udini wako, basi kapumzike!

Hao wamemuelewa au wamefuata madaraka? Mtu aliyeelewa hawezi kujiunga nanyi na masharti ya yeye nduo aongoze.
 
Sentensi za Prof. Lipumba akiwa na
waandishi wa habari
By :
'Nawaomba radhi sana Wanachama na
Wananchi walioniamini na kuonesha
mapenzi makubwa ktk Uongozi wangu'
'Najua hili litawashtusha,
litawakasirisha, litawafadhaisha.
Ndani ya Chama mimi naonekana ni
kikwazo'
Naonekana siwezi kuwa na mchango kama
Kiongozi ktk Mapambano ya kudai haki
sawa'
Nimeona niachie ngazi lakini
niendelee kushiriki shughuli nyingine
zinazohusu Maendeleo ya Chama
Kiuchumi'
'Ninaendelea kuwa Mwanachama wa CUF
na nimelipia Kadi ya Uanachama mpaka
2020, sina mpango wa Kujiunga ACT'
Taarifa ya kung'atuka niliitoa August
01 2015, nilisubiri kukamilisha
masuala ya UKAWA ndio nitoke'
'Naubariki Umoja wa UKAWA ili
tusimamie kupata Katiba
iliyopendekezwa na Wananchi'
'Ni kweli nilishiriki kumkaribisha
Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi
yangu inanisuta'-
'Tumekaribisha watu wa CCM ambao
waliipinga Rasimu ya Katiba,
najiuliza tutaweza kusimamia malengo
ya UKAWA'
'Nimeona nijikite kwenye kufanya
Utafiti wa Ushauri wa masuala ya
Uchumi ili kuinua Uchumi wa nchi'
Sijashawishiwa na mtu yoyote kuachia
ngazi,ni dhamira na nafsi yangu..
asisingiziwe mtu kwamba amenishauri'
'CUF bado imo ndani ya UKAWA,
nitashiriki Kampeni za Uchaguzi kama
mwanachama wa kawaida wa CUF'
 
prof na dr wote ni kundi moja na wote wanaongea lugha moja na wameaga kwa lugha moja hawa ni watu wa hovyo kabisa!!
 
Sijawahifikiria wala kuona katika maisha yangu muumini anaposlimu na kuingia msikitini Sheikh anaacha jukumu lake la kuongoza na kuwa muumini wa kawaida eti kwa sababu huyu muumini alikuwa anaamini Biblia sasa ana mashaka kama ataielewa Qoruan.Ni bora kutoenda shule kabisa kuliko kwenda na ukaelimika ndani ya Tanzania
Sentensi za Prof.Lipumba akiwa na waandishi wa habari leo hii akijiuzuru uwenyekiti wa CUF
"Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta.Tumekaribisha watu wa CCM ambao walipinga Rasimu ya Katiba,najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA?"
. "CUF bado imo ndani ya UKAWA nitashiriki kampeni za uchaguzi kama mwanachama wa kawaida wa CUF"
. Sasa tunamsubiri Dr Slaa kama ataingia kwa njia hiyo ya Lipumba au la!Muda utafika
 
Si hata hilo pia wananchi wanataka kuona kwanza viongozi wanao waamini kuelekea uchaguzi mkuu, hivi unadhani bila ya ushiriki wa Slaa na Lipumba kwenye hizi campaign how many people will be demoralized?

Isitoshe huyu Lipumba alivyo ponda wazi kuhusu msimamo wao wa awali juu ya muungano wa UKAWA ambao chanzo chake ni rasimu, unless labda huyo Lowassa nae aendelee na wimbo wa rasimu lakini huu wimbo wa goli la mkono watu washaushtukia ni sababu za mapema kwenye kujihami ata wakishindwa kialali poor UKAWA.

Hakuna Jinsi....

Lazima tusonge Mbele

This is a battle

Sio wote wanaoweza kufika salama

Unajua mtu kuachia uenyekiti,Ukatibu wa chama kikubwa kabisa sio mchezo.

Lipumba kuponda sio tatizo..Anajianika alivyo mnafiki...Kumbuka yeye ndiye Mwanzilishi wa UKAWA

This tarnishes his image
 
Kwa mara ya kwanza nakubaliana na mzee wa kujificha Mzee Mwanakijiji.

Hili dubwana UKAWA litaleta matatizo makubwa haya maneno yake nayakumbuka.

Mbowe, kazi kwako acha jimbo la Hai zunguka na wagombea wako wa kukodi ukawanadi kwa wananchi.
 
Last edited by a moderator:
sisi tunatafuta mtaji wa kura ili tuitoe ccm madarakani eti yeye Lipumba anasema tunakosea kuwakaribisha waliounga mkono katiba pendekezwa.
Sasa bila kuunganisha nguvu na kuifuta ccm madarakani tutaweza vipi kuipiga chini hiyo katiba pendekezwa??

kwakweli Lipumba ametoa sababu shallow mno.
 
God is on throne.... We shall see whose words count, hakuna fisadi atakanyaga ikulu ya Tanzania, its a decree!

Mafisadi mpaka wakae chini..... Hii move mtacheza mpaka mwisho kwa style ya changing roles bila kujua anayewachezesha ni nani yupo wapi na ana capability na capacity gani!
 
Back
Top Bottom