Prof. Ibrahim Lipumba atangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti wa CUF Taifa

run CMD

JF-Expert Member
May 31, 2015
2,825
3,133
Lupumba.jpg
Prof. Lipumba akiongea na waandishi wa Habari kwenye Hoteli ya Peacock

Prof. Ibrahim Lipumba ametangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti kwenye chama chake cha Wananchi CUF.

Ametangaza kuachia ngazi uenyekiti wa chama hicho mapema leo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Peacok.

Amesema amechukua uamuzi huo kutokana na UKAWA kushindwa kusimamia makubaliano yao.

Chanzo: Nipo kwenye kikao

=======

Prof Lipumba akitaja sababu za kujiuzulu nafasi ya uenyekiti CUF


Sentensi za Prof. Lipumba akiwa na waandishi wa habari
'Nawaomba radhi sana Wanachama na Wananchi walioniamini na kuonesha mapenzi makubwa ktk Uongozi wangu'

'Najua hili litawashtusha, litawakasirisha, litawafadhaisha. Ndani ya Chama mimi naonekana ni kikwazo'

Naonekana siwezi kuwa na mchango kama Kiongozi ktk Mapambano ya kudai haki sawa'

Nimeona niachie ngazi lakini niendelee kushiriki shughuli nyingine zinazohusu Maendeleo ya Chama Kiuchumi'

'Ninaendelea kuwa Mwanachama wa CUF na nimelipia Kadi ya Uanachama mpaka 2020, sina mpango wa Kujiunga ACT'

Taarifa ya kung'atuka niliitoa August 01 2015, nilisubiri kukamilisha masuala ya UKAWA ndio nitoke'

'Naubariki Umoja wa UKAWA ili tusimamie kupata Katiba iliyopendekezwa na Wananchi'

'Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta'-

'Tumekaribisha watu wa CCM ambao waliipinga Rasimu ya Katiba, najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA'

'Nimeona nijikite kwenye kufanya Utafiti wa Ushauri wa masuala ya Uchumi ili kuinua Uchumi wa nchi'

Sijashawishiwa na mtu yoyote kuachia ngazi,ni dhamira na nafsi yangu.. asisingiziwe mtu kwamba amenishauri'

'CUF bado imo ndani ya UKAWA, nitashiriki Kampeni za Uchaguzi kama mwanachama wa kawaida wa CUF'

 
Last edited by a moderator:
Taarifa ya lini hii, jana si alizuiliwa na Wazee asubiri mpaka uchaguzi upite.
 
Habari wakuu,
Baada ya sintofahamu ya jana, leo mwenyekiti wa CUF ameamua kujiuzulu nafasi yake kama mwenyekiti wa chama cha CUF, Prof Lipumba atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CUF. Ameita waandishi wa habari na kuongea baada ya jana kuzuiwa na wazee.

Sababu ni kutokwenda sawa na wenyekiti wenza wa UKAWA kuhusu kumuunga mkono mtu na kuwapokea watu ambao wamehusika na kutengeneza rasimu ya katiba mpya ambayo yeye hakubuliani nayo na yeye anaunga mkono rasimu ya katiba ya jaji Warioba.

Atashiriki kupigia kampeni wagombea ukiacha Urais na alipoulizwa kuhusu kuhusu kuchukua uamuzi huu sasa kasema dhamira yake inamsuta na walipomuuliza kuhusu pesa kasema hata kumuita mgombea ambae atagombea kupitia UKAWA wanashutumiwa wamepokea pesa hivyo hilo halimsumbui bali dhamira yake na nia ya kuungana kuitetea rasimu iliyopigwa teke na CCM.
 
Baada ya hapo jana kuhairisha mkutano na waandishi,leo trh 06/08/2015 Ndugu Lipumba ametangaza kujiuzulu rasmi katika nafasi hiyo ya Mwenyekiti.
Live from Peacock Hotel.
 
Mwenye kujia hasa nini kimesababisha Prof. kujiuzuru katika kipindi hiki tafadhali atujuze zaidi.
 
Back
Top Bottom