run CMD
JF-Expert Member
- May 31, 2015
- 2,825
- 3,133
Prof. Lipumba akiongea na waandishi wa Habari kwenye Hoteli ya Peacock
Prof. Ibrahim Lipumba ametangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti kwenye chama chake cha Wananchi CUF.
Ametangaza kuachia ngazi uenyekiti wa chama hicho mapema leo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Peacok.
Amesema amechukua uamuzi huo kutokana na UKAWA kushindwa kusimamia makubaliano yao.
Chanzo: Nipo kwenye kikao
=======
Prof Lipumba akitaja sababu za kujiuzulu nafasi ya uenyekiti CUF
Sentensi za Prof. Lipumba akiwa na waandishi wa habari
'Nawaomba radhi sana Wanachama na Wananchi walioniamini na kuonesha mapenzi makubwa ktk Uongozi wangu'
'Najua hili litawashtusha, litawakasirisha, litawafadhaisha. Ndani ya Chama mimi naonekana ni kikwazo'
Naonekana siwezi kuwa na mchango kama Kiongozi ktk Mapambano ya kudai haki sawa'
Nimeona niachie ngazi lakini niendelee kushiriki shughuli nyingine zinazohusu Maendeleo ya Chama Kiuchumi'
'Ninaendelea kuwa Mwanachama wa CUF na nimelipia Kadi ya Uanachama mpaka 2020, sina mpango wa Kujiunga ACT'
Taarifa ya kung'atuka niliitoa August 01 2015, nilisubiri kukamilisha masuala ya UKAWA ndio nitoke'
'Naubariki Umoja wa UKAWA ili tusimamie kupata Katiba iliyopendekezwa na Wananchi'
'Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta'-
'Tumekaribisha watu wa CCM ambao waliipinga Rasimu ya Katiba, najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA'
'Nimeona nijikite kwenye kufanya Utafiti wa Ushauri wa masuala ya Uchumi ili kuinua Uchumi wa nchi'
Sijashawishiwa na mtu yoyote kuachia ngazi,ni dhamira na nafsi yangu.. asisingiziwe mtu kwamba amenishauri'
'CUF bado imo ndani ya UKAWA, nitashiriki Kampeni za Uchaguzi kama mwanachama wa kawaida wa CUF'
Last edited by a moderator: