Prince Bagenda ashambulia vikali M4C ya CHADEMA

Prince Bagenda ashambulia vikali M4C ya CHADEMA

Kumbe nae Bangenda yupo!! Sijasahau uvurugaji walioufanya kwenye chama cha Nccr kumbe walikuwa hata hawaamini walichokuwa wanasema wakati ule na asome alama za nyakati huyo mzee sasa.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kwamba maudhui ya kile kitabu chake cha mwaka 2006 ''Tumaini Lilillorejea'' yaliegemea katika itikadi gani?Yafaa pia atueleze sasa tuzingatie nini hasa kama udhihirisho ama hakikisho la Tumaini hilo ambalo wengine hatulioni hadi leo.Halafu NCCR-Mageuzi aliyopata kuiongoza ilipata kuwa na itikadi?Wananchi walikiunga mkono chama hicho ,mwaka 1995, kwa sababu kilikuwa na itikadi iliyokuwa wazi na yenye kueleweka?Hapana.Wananchi walikuwa wanataka mageuzi na mabadiliko.Walichoshwa na hali iliyokuwepo,basi!Je,kuondoka kwake NCCR kulichangiwa na kubadilika kwa itikadi yake ama kuna kingine?Kama hakuondoka kwa sababu za kiitikadi pekee,kwa nini, sasa ,uchambuzi wake uegemee katika itikadi pekee?
Atambue kuwa,hata sasa, wananchi wanaosaka mabadiliko hawataki kujua sana misamiati ya ''itakadi'' , ''falsafa'', ''mwelekeo'' ama ''Imani''!!Wao wanataka mabadiliko..Kama hajaiona ''itikadi'' ,tumwache aendelee kuitafuta anaweza kuiona ADC ama DP ama CHAUSTA! ikiwa baadhi ya wahafidhina wanadhani hatuna itikadi hilo litatatuliwa mbele ya safari...
Mwisho,baadhi yetu tunamtazama Bagenda kama msaliti na kama mtu aliyekosa msimamo.
Baadhi yetu tulikuwa wasomaji wa makala zake wakati huo RAI ikiiunguruma kweli kweli..Alitujengea roho za upinzani tungali wadogo kabisa -tukisoma gazeti la ''RAI'' lililokuwa likiletwa nyumbani na wazazi wetu- .Tukajenga,hatimaye, mashaka dhidi ya watawala.Sasa tumeota sugu kweli kweli ..Baadhi yetu tumweka nadhiri kuwa kamwe hatuwezi kukana dhamira zetu. Hakuna kurudi nyuma.Yeye aendelee kulingoja ''Tumaini Lililokuwa lireje''!!
 
Sasa wewe ndie unaharibu.

Hoja huangaliwa na ikionekana ina kasoro si anaangaliwa anaeleta hio hoja ama vipi?.

Prince Bagenda ameleta hoja mbovu na haileweki si inabidi kumwangalia mtu mwenyewe au wewe umeonaje hoja yake?

Ikiwa unaungana nae basi usijibu swali langu bali chambua hoja yake, na kama unaona hoja yake ina mapungufu basi wewe ongezea mapungufu hayo.

Prince Bagenda hajaleta issue hapa ameleta calculated propaganda, na mtu wa mithili yake(kwa maana ya heshima ya namna anavyoandika na kuchambua mambo) kuleta hayo watu hawezi kujizuia kwenda personal and physical if needs be. It is intended distortion at its best. Ndio maana watu wanaangalia his track record ili kuunganisha na upuuzi aloandika
 
Tusome nyakati. Tupo wengi tunaotetea chama chetu, ingawa sasa ni vigumu kukitangaza mbele ya umma ukapigiwa makofi. Wakati ukifika, namshauri tuhamie huko kabla mlango haujafungwa, kwani wakati utafika tutakapo omba mlango ufunguliwe tuingie, wakati huo mlango utakuwa umekwisha fungwa. Hatuna jinsi, wala hatuwezi kupingana na wakati. Wimbi la wananchi, linaonesha wazi kuwa chama chetu kinaelekea kufa. "NAWASHAURI TUHAME KABLA MLANGO HAUJAFUNGWA" wala huu si wakati wa kupinga nguvu ya umma. tutajiletea matatizo bure.
 
Kada wa chama cha mapinduzi na mwanasiasa mkongwe nchini Prince Bagenda amekishambulia chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kwa operesheni yake ya M4C inayotishia uhai wa CCM.
Katika makala yake ndani ya gazeti la RAI Prince Bagenda amedai M4C ni chama kipya cha siasa ndani ya CDM na kusema hali hiyo ni hatari kubwa kwa ukuaji wa chama hicho na amesema utatokea mvutano mkubwa kati ya wafuasi wa CDM na wafuasi wa itikadi ya M4C.
Bagenda pia amesema kampeni ya M4C wanayoongoza nchi nzima inatangaza sera za shari na chuki.Pia amesema CDM walipata kura nyingi uchaguzi mkuu uliopita kutokana na vita ya makundi ndani ya CCM na kamwe si kutokana na chama hicho kuwa na sera nzuri.Amesema CDM hawana Itikadi inayoeleweka hadi sasa ndiyo maana mpaka sasa wajanja kama yeye wako CCM.

Source:RAI Alhamisi

My Take:
Prince Bagenda alishiriki kusambaratisha chama cha NCCR Mageuzi baada ya kuongoza mgogoro mkubwa huku akikimega chama vipande viwili na yeye akiwa Katibu Mkuu kambi ya Mrema.Baada ya kufanikisha kusambaratisha NCCR,Prince Bagenda alihamia CCM ambapo hadi leo yeye ni kada mwaminifu wa CCM.

TISS huyo tuendelee.....
 
Huyu Bagenda na akina Salva ni jamii moja. Njaa iliwafanya wakane weledi wao. Sisi tuliowafahamu hakika twawaita "marehemu"


Huyu jamaa ni jamii ya wale wanyama ambao wanakula na kushiba na kutapika. Lakini wakishatapika wanachangamkia matapishi yao. Alikuwa Fisi Wenu akaenda NCCR na baadaye akayarudia matapishi yake huko Fisi Wenu.
Mnyama anayerudia matapishi (ambaye ni maarufu) hawezi kuelewa itikadi, vyama vya siasa wala siasa yenyewe. Ni wa kuhurumiwa na kuachwa aendelee kufaidi matapishi yake. Mnyama huyo anaitwa ...
 
Hivi huyu si ndiyo yule mtu aliyeandika kitabu kinachoitwa Tumaini lililorejea alimsifu sana JK. Vipi bado anaimani ileile kwamba JK Ni tumaini lililorejea.Naomba Ndugu Bagenda unijibu la sivyo nitaona kila unachoandika ni upuuzi.
 
PRINCE, tehe tehe, Bagenda, NGOMA YA UKAE, tehe tehe tehe teheee teeee teehee heheee!!
 
Shauri yenu msiemjua vema li- Prinsi la Baghenda!!!

M4C na muziki wake kila kona ya nchi ndani ya CHADEMA hakika CCMU chaivulia kofia hata kabla hatujaingia robo ngwe.

Someni vizuri hiyo namba enyi wakuu wa ufisadi nchini.!
 
Prince Bagenda hajaleta issue hapa ameleta calculated propaganda, na mtu wa mithili yake(kwa maana ya heshima ya namna anavyoandika na kuchambua mambo) kuleta hayo watu hawezi kujizuia kwenda personal and physical if needs be. It is intended distortion at its best. Ndio maana watu wanaangalia his track record ili kuunganisha na upuuzi aloandika

Absolutely YES
 
Kada wa chama cha mapinduzi na mwanasiasa mkongwe nchini Prince Bagenda amekishambulia chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kwa operesheni yake ya M4C inayotishia uhai wa CCM.
Katika makala yake ndani ya gazeti la RAI Prince Bagenda amedai M4C ni chama kipya cha siasa ndani ya CDM na kusema hali hiyo ni hatari kubwa kwa ukuaji wa chama hicho na amesema utatokea mvutano mkubwa kati ya wafuasi wa CDM na wafuasi wa itikadi ya M4C.
Bagenda pia amesema kampeni ya M4C wanayoongoza nchi nzima inatangaza sera za shari na chuki.Pia amesema CDM walipata kura nyingi uchaguzi mkuu uliopita kutokana na vita ya makundi ndani ya CCM na kamwe si kutokana na chama hicho kuwa na sera nzuri.Amesema CDM hawana Itikadi inayoeleweka hadi sasa ndiyo maana mpaka sasa wajanja kama yeye wako CCM.

Source:RAI Alhamisi

My Take:
Prince Bagenda alishiriki kusambaratisha chama cha NCCR Mageuzi baada ya kuongoza mgogoro mkubwa huku akikimega chama vipande viwili na yeye akiwa Katibu Mkuu kambi ya Mrema.Baada ya kufanikisha kusambaratisha NCCR,Prince Bagenda alihamia CCM ambapo hadi leo yeye ni kada mwaminifu wa CCM.

Hahahahahaha, CCM ina itikadi gani? Kweli ujinga ni mzigo mzito saaaana!!!!!! Hivi kipindi chote kile alipokuwa NCCR MAGEUZI kumbe lengo lilikuwa kujaza tumbo tu? sasa yupo na akina tumbo tumbo akili haifikiri tena. Hivi hakuna mwenye busara katika CCM nyakati hizi? Akisimama Mukama utumbo, akisimama Nape uozo mtupu, Wasira akisimama upuuzi tu, akisimama Pinda liwalo na liwe (huku akilia), akisimama Bagenda naye kumbe ndio matope matupu. Sipati jibu tulifikiaje kunaongozwa na watu hawa.
 
Bagenda ni wa kuhurumia..tunaomfahamu vzr wala hatusemi bore tumuombee japo apate mkate wa siku...
 
Hana jipya huyu! Anatumiwa na mafisadi kuganga njaa! alikuwa mhariri mkuu wa kijigazeti cha yule jamaa aliwahi kuwa waziri wa tanesco na migodi (Anatokea Kagera); kigazeti kikafa na sasa kahamia kwa fisadi mwingine (aliyetwaa magazeti yaliyoheshimika zamani - RAI) na kupewa uhariri wa kigazeti kingine cha ung'eng'e. KWELI anajua jinsi ya kupata hela ya kula! Ila kwa M4C, kapotea njia.
 
Ameanza kuhaha huyo maana mwisho wa wanaomshibisha umefika? and kwa taarifa yenu M4C ni vuguvugu na wala si chama kama anavyodai yeye. Hata TANU wakati wa kudai uhuru wakoloni walikiona kinaleta siasa za chuki lakini uhuru ukafika 1961, Uhuru halisi unarudi tena 2015, kwa heri Bagenda na ccm
 
Back
Top Bottom