Kajunjumele BA
JF-Expert Member
- Jan 3, 2012
- 673
- 351
wananchi msiumize vichwa vyenu... Binafsi naweza kusema sumaye anazosifa za kushika nafasi kuu. Akiwa w/mkuu miaka miwili ya mwisho ya mzee rukhsa na baadae kuendelea na mzee mkapa tumeweza kuona juhudi zake na mapungufu yake kiasi lkn amethubutu chini ya uongozi wa mkapa kuifanya nchi kuheshimika kwa wananchi na nje ya nchi kwa kudhibiti mifumuko ya bei ambayo mpaka leo hii ambacho siwezi kusahau ni nauli ya daladala aliipokea kutoka kwa mzee mwinyi ikiwa ni sh 150/= na tukamaliza nayo katika utawala wake mpaka alipo mkabidhi kanali jakaya ambaye binafsi nasema ameliyumbisha taifa kupitia kwa msaidizi wake mr lowassa aka msanii nimuite hivyo.
Kinacho shangaza mr lowassa amekuwa na juhudi nyingi za kujifanya anauchungu wa nchi hii wakati si kweli.
Nisiseme mengi juu ya huyu mr lowassa kwani anajulikana ndani ya miaka mi2 tu ameharibu na kufikia kutimuliwa hii ni kutokana na kukosa uadilifu katika madaraka aliyokabidhiwa.
Hivyo basi nahitimisha kusema kwamba wananchi tusihadaike na mh. Huyu msanii maana hana jipya.
Kama tunataka kweli maendeleo basi bw. Sumaye anaweza kutokana na historia yake na pia la muhimu zaidi ni yuko fiti kiafya na anajiamini hana kashfa, na mtu wa watu maana nilishawahi kukutana nae duka moja mitaa ya samora sikuweza kuamini waziri mkuu aliyekaa madarakani kwa kipindi kirefu kupita wote walio pita awe hana ulinzi wa kutisha kama anavofanya bwana msanii maana nae nilikutana nae mitaa yake ya obay akiwa na jopo la ulinzi nilishangaa mbona sumaye waziri mstaafu hana ulinzi kama huu?? Wakati huyu msanii kakaa miaka 2 tu mjengoni na kutimuliwa alafu ulinzi mkubwa loh??? Haya ni majanga
kiukweli kama wananchi tunataka maendeleo ya nchi hii basi nafasi iwe wazi kwa bw sumaye maana rekodi yake inajulikana. Tusifate ushabiki na njaa ya vijipesa mnavyohongwa makanisani na misikitini na sasa hivi kaingia mashuleni ili awakamate wazazi.
Kazi kwenu wananchi.
1. Mkuu kimsingi na kubaliana nawe kwa sehemu kwani Kashfa nyingi za Sumaye zilikuwa za kutungwa na ndo maan aliporudi kutoka masomoni Harvard alivitahadharisha vyombo vilivyokuwa vikimchafua kwamba kwa sasa vikiendelea viwe tayari kuakabiliana na mkondo wa Sheria kwani awali aliwavumilia kwakuwa alikuwa Kiongozi lakini kwa sasa hata sita kusafisha jina lake kisheria...na Kuthibitisha kwamba vyombo vile vilikuwa vikitoa habari za uzushi baada ya mkwara huo vilinyamaza.
2. Sehemu ya Pili kuhusu kufaa kwa Sumaye kugombea Urais sina Pingamizi iwapo ataomba kupitia vyama vya "watanzania" Hapa na maanisha vyama vinavyoongea lugha ya watanzania lakini iwapo ni kupitia CCM ni BIG NO CCM imeharibika beyond repair Kaka.