Kama CHADEMA itakufa au viongozi wakabadilishwa, siyo ACT inayoweza kusababisha hayo.
Katika hatua za awali ili chama kiweze kuaminika ni lazima waanzilishi wake wawe na haiba na wawe wanaaminika kwa jamii angalao kwa wakati huo.
NCCR ilipata wanachama wengi sana na kuungwa mkono kutokana na vigogo wa mageuzi waliokutana na kukianzisha, na baadaye hamasa ikaja kuongezwa na Lyatongo ambaye wakati huo alikuwa mtu mashuhuri sana katika serikali ya CCM.
CHADEMA ilianzishwa na akina MTEI, watu ambao walikuwa na rekodi zao za utumishi na siasa za kiwango cha juu.
Vyama vyote vya siasa vilivyoanzishwa na watu wasioeleweka au kuaminika, au vigeugeu vilikufa kabla havijasimama, vimebakia tu kwenye daftari la msajili.
Huyu mwenyekiti wa muda, ni mtu ambaye hana mbele wala nyuma, juzi CUF, jana ADC, leo ACT, kesho na keshokutwa hatujui atakuwa nani! NI MWENDAWAZIMU GANI ATAMWAMINI MTU KAMA HUYO? Zitto naye kwa sasa haaminiki kabisa, wengi tunamwona ni popo, si ndege si mnyama, NANI MWENYE HEKIMA ATAMFUATA ZITO. Kwa vyovyote ACT itawapata baadhi ya Watanzania lakini kwa kiasi kikubwa watakuwa wa namna ya akina Zitto, watu wasioaminika katika jamii, kukipambazuka wanapiga vita rushwa, likizama wanapokea hongo toka CCM.
Mbowe ajiandae kurudi kwenye bashara zake za kilaghai chadema lazima ipotezwe kwenye siasa za tanzania tuliwambia wamuombe msamaha zitto wakajifanya wajanja sasa fimbo wanazo.