Precision Air versus FastJet, Nani zaidi

Huwezi kuoperate airbus kwa nauli ya 32k kwenda Mwanza!!!

I guess hiyo 32k ni offer ya ticket chache lets say 10% ya tickets for every flight, Marketing strategy

Tatizo tulilonalo Tanzania ni ukosefu wa waandishi wazuri wa mambo ya biashara. Ukisoma comments za watu wengi hapa ni wazi bado hawaelewi business model ya FastJet. Hii ni low-carrier/no-frills.

Kwa wale wanaolinganisha FastJet na Community air- sio sahihi kabisa. Anthony Diallo didn't do his homework properly kabla ya kuanza hiyo biashara and most crucially, hakuwa na experience kwenye aviation industry.

Founder wa FastJest - Sir Stelios- ni guru wa hizi low carrier. Yeye mwenyewe (Sir Stelios) ameenda shule - ya kueleweka. He is very good kwenye Finance na ana experience sana kwenye aviation industry. Tukumbuke huyu bwana ndiye alianzisha Easyjet. Sasa hivi Easyjest wana wanaenda zaidi ya nchi 30! Kwa mwaka mmoja tu EasyJet anasafirisha si chini ya 50 million passengers!

Pia Easyjet wako listed kwenye London Stock Exchange. Hana magumashi huyu bwana. FastJet itatumia business model hiyo hiyo ya EasyJet - no frills. Hakuna mambo ya juice -juice na vimikate au sijui vikorosho vya bure, kama unataka kula unalipa! Na pia ana very 'lean' administration. Wateja wanakuwa encouraged ku-book flight kupitia website au hata simu. Hii inapunguza gharama za uendeshaji - ambazo mwisho wa siku zinaishia kwa mteja!

Jambo jingine, FastJet kama ilivyo EasyJet, mteja anapata unafuu kwenye bei kama uta-book mapema. Kuna peak & off-peak prices. Mfano mtu anayesafiri saa 4 asubuhi anaweza kulipa zaidi kuliko anayesafiri saa 12 jioni, hata kama watasafiri siku hiyo hiyo. Uzuri ukifanya booking kupitia website yao unapata options nyingi (including bei/time dates). Pengine hii itatusaidia sisi Watanzania kuwa more organised - kupanga ratiba mapema badala ya kuishi kwa mtindo wa zima moto!

Kwa wale wanaosubiri FastJet wafe kifo cha Community air, waandike maamuvu. Kwanza tuone jinsi huyu Sir Stelios alivyoingia kwenye soko. Ameanza East Africa - specifically Tanzania - kwa kununua shares zote za 540. That means amenunua routes/customer base yote ya 540! (market entry). Badala ya kuweka base Nairobi - yeye kaja moja kwa moja Dar. why? Kwa sababu Bongo ndio kuna UKAME zaidi wa usafiri wa anga. Kenya wana Kenya Airways. Hapa bongo ni Prescion na mdundiko wake wa delays!

Kenya Airways waliposikia huyu FastJest inakuja (na wanajua fujo za Sir Stelios) walianza low-cost service - haraka. Leseni ya low-cost ilitoka kama miezi 2 hivi iliyopita. Hawakukaa chini na kuongea kama 'Tomaso', badala yake walianza kujiandaa kwa mazingira ya ushindani.

Jambo jingine, FastJet inaonekana ku-concentrate kwenye routes za kwenye natural resources. Mipango iliyopo ni kwamba, ataanza na Tanzania, Kenya & Ugana, lakini baadae ataongeza routes Angola, Ghana etc. Sijui Community air alikuwa na mipango gani?

How about Air Tanzania.

Sasa hivi Tanzania imeshaingia kwenye ukurasa wa nchi zenye gas, uranium na madini mengine. Big boys wako mjini. Serikali kuendelea kufanya biashara itatugharimu. Air Tanzania bado inaendeshwa na wanasiasa! Mkurugenzi anateuliwa na rais, tena bila interview yoyote! So far hakuna la maana linaloendelea na ujio wa wazee wa kazi kama FastJet unahitaji new thinking toka serikalini.

Kwa mtazamo wangu, Air Tanzania ivunjwe (kabisa), na kuundwa shirika jipya. Serikali iwe ni shareholder lakini wawepo wanahisa wengine. Mambo ya presidential appintee yaishe. Mkurugenzi/wakurugenzi wapatikane kupitia njia za ushindani. Tofauti na hapo, Dr Mwakyembe afunge office za ATCL, na aelekeze hela kuboresha viwanja vya ndege ili wazee wa kazi warushe ndege, na kama kuna change aboreshe usafiri wa Train.

And to the old bag - Precision air

Your time is up, review your business model -haraka. Bad mouthing is not a business model! Mtindo wa kuacha wateja airport wakipiga miayo siku nzima ukome. Even as we speak fungua websites za Precision na FastJet and you will see the difference! FastJet, naweza ku-book flight sasa hivi na nikapata jibu including muda wa kulipia. Lakini Precision website, hata kufunguka ni shida tupu!

Karibuni sana FastJet.
 
Siku ambayo umechelewa ku-check in airport ndio watu watajua umuhimu wa low cost airline hivyo unapofanya booking jitahidi kusoma terms and condition sio unafurahia kulipa nauli ya 43100
 
Jamani me mwenyewe nimetoka kukata tiketi sasa hivi, kwa jinsi walivyonielezea ni kwamba kuna class 3 na nauli ya kuanzia ni 32 elfu na ni class ya chini kabisaa, lipo daraja la kati ambalo nauli yake ni 75000(1way) na class ya juu kabisaa ni laki 1 na 17(1 way) so usije ukashangaa unaenda kufanya booking unaambiwa daraja la nauli ya 32 limejaaa! Nimeshuhudia watu wanaambiwa hivyo pale ofisini kwao airport leo!!

Nauli hizo zipo mie nimebook jumatatu iliyopita kuondoka tarehe 7 dec na kurudi tarehe 14 nimelipa 86,100 (go and return), kila kitu kipo kwenye mtandao na inategeme umefanya booking lini, ndege unapofanya booking leo kuondoka kesho bei huwa juu sana kuliko anaefanya booking leo alafu akaondoka baada ya wiki 2. Ikumbukwe hiki ni kipindi cha sikukuu na wao wana ujanja wa kibiashara

Ukitaka kupata ticket tujifunze kufanya booking online maana kuna option kibao na unaweza kubadilisha hata siku ya safari kama unaweza maana ticket ya kesho yake unaweza gundua ni ya chini zaidi kuliko uliyopanga wewe, kikubwa ni kujifunza kupanga safari mapema
 
  • Thanks
Reactions: FJM
What about kuongeza kodi kwenye mafuta ya taa ili kucurb uchakachuaji wa petrol na diesel? What percentage of Tanzanians uses kerosene? The tax collected from kerosene how does it help the poor who are the majority users of kerosene? So ukisema kuwa serikali haiwezi kupunguza kodi kwenje jet fuel is wrong.


Hilo la kuongeza kodi kwenye mafuta ya taa kia mtu anajua kuwa serikali walichemka! Haina manufaa kwa yeyote. Kama umesoma uchumi, wanaitabzero sum game.
 
Pole kaka,nahisi watumia physiological marketing pricing strategies kuingia sokoni,You think it is cheaper but in reality very Expensive!!!!!!!!
Sasa wewe huoni hiyo ni nafuu wakati one way Precission wanatoza 175,000 kwenda Mwanza,tatizo mumezoea kubeba matenga ya samaki bure huko kwenye ndege nyingine
 
Wanachosema hawa jamaa ni kuwa katika kila abiria 200 wanaosafiri kwa mara moja, kunakuwa na tiketi 50 za nauli ya 43,000 (32,000 bila kodi), na mafungu mengine ya sh. 59,000/, 75,000/, 96,000/ hadi 291,000/. So price inategemea availability ya hizo chances. Mie nimepata ya 59,000/ kwa tarehe15 Dec Mwanza - Dar.
 
FastJet inaleta changamoto kubwa kwa Precision air na hii ni nzuri lakini ni hatari sana kwa usafiri wa anga Tanzania kwa sababu FastJet hawawezi kwenda routes nyinginezo ukiacha ya Dar-Mwz na Dar-KIA. Dege lao kubwa vile kwanza haliwezi kutua mfano Mtwara na hakuna abiria wa kutosha kwenda kwenye destinations nyingine zaidi ya Mwz na KIA. Sasa kama Precision air ikifa hii fastjet itaweza kutoa huduma mikoa mingi kama precision wafanyavyo kwa sasa? kwa maneno hayo nisingependa Precision air ife!!

Precision air wajifunze kwamba competition is stiff and many more new entrants in the market are there to come. Waboreshe huduma ili abiria wasiwakimbie. Kuna watu kulipa laki 4 sio tatizo kwao bora tu huduma iwe nzuri. All in all competition in the service industry is a good thing. So Viva FastJet

Biashara ushindani...,
FasJet ni changamoto kwa Precision air kibiashara.
Ni vizuri Precision wakajitathimini vinginevyo wanaweza angukia pua..., Ile mambo ya monopolism kwenye biashara na kufanya upendavyo sasa imepitwa na wakati.
 
Huo ni mchezo wa kawaida wa kuteka soko! ni moja ya njia tano ktk mbinu za ushindani wa biashara za Pof. Porter....
A cost leadership strategy is based on a marketing strategy in which price is the main strategic tool and where the business objective is market share leadership.In order for this strategy to be successful, your business will need to become the lowest-cost producer in its industry. That means managing costs in marketing and non-marketing functions such as production, supply, etc.- "Porter's generic Strategies"
 
Fair Competition Commission wanatakiwa watupe jibu kama ni halali kutoza chini ya kiwango cha matumizi (below cost) ili kuua ushindani......sidhani kama inakubalika Lamchina
Unauhakika gani hicho kiwango ni chini ya kiwango cha matumizi? Tayari umepewa gharama za kodi na nauli bila kodi sasa unataka nini zaidi? Na pia ukumbuke usafiri huo pia una gharama za juu kulingana na muda wa kukata tiketi yako kwa hiyo profit margin yao imepangwa kulingana na category ya tiketi yako.
 
quote_icon.png
By Lamchina

Pole kaka,nahisi watumia physiological marketing pricing strategies kuingia sokoni,You think it is cheaper but in reality very Expensive!!!!!!!!
Labda ufafanue hiyo reality maana nimesafiri KIA to JKNIA kwa sh 59000 badala ya 180000 halafu wewe unasema in reality ni expensive hebu fafanua tukuelewe.
 
wakuu sijasoma post zote,ila airport tax ni shs 70,000,kwa hiyo kama jamaa watatoza buku 32,plus vat inakua kama 42,000,uki add airport tax unapata 112,000 hv!hii ndio bongo!
 
wakuu sijasoma post zote,ila airport tax ni shs 70,000,kwa hiyo kama jamaa watatoza buku 32,plus vat inakua kama 42,000,uki add airport tax unapata 112,000 hv!hii ndio bongo!

Wacha u mbwiga wewe! Watu wameainisha costs zote hapo juu, wewe unaleta mambo ya kufikirika na kuishangaa bongo! Yaani hukutaka hata kujishughulisha kusoma posts za wenzio kabla ya kuandika blah blah zako hapa? Ninyi ndio mnao sign documents nyeti bila hata ya kuzipitia
 
last wk nillikuwa natuma mizigo mwanza kwa basi pale ubungo, yaani wafanyakazi wa kwenye mabasi wanalalamika balaa eti ajira zetu itakuwaje tena na hii fast jet! yaani sie huku tunafurahia ila jamaa pale wameind saaana, wanasema inabidi serikali iipige marufuku, mi nikawambia nanyie mtafute strategy ya kufanya watu wapande mabasi eti mafuta bei juu jamani, mi nikawambia ni kama vile ilivyo kwa daladalaz versus train ya mwakyembe..ushindani lazima sokoni
 
wakuu sijasoma post zote,ila airport tax ni shs 70,000,kwa hiyo kama jamaa watatoza buku 32,plus vat inakua kama 42,000,uki add airport tax unapata 112,000 hv!hii ndio bongo!

Hujapanda ndege wewe.
Airport tax kwa local bound planes ni 10,000!
 
FastJet inaleta changamoto kubwa kwa Precision air na hii ni nzuri lakini ni hatari sana kwa usafiri wa anga Tanzania kwa sababu FastJet hawawezi kwenda routes nyinginezo ukiacha ya Dar-Mwz na Dar-KIA. Dege lao kubwa vile kwanza haliwezi kutua mfano Mtwara na hakuna abiria wa kutosha kwenda kwenye destinations nyingine zaidi ya Mwz na KIA. Sasa kama Precision air ikifa hii fastjet itaweza kutoa huduma mikoa mingi kama precision wafanyavyo kwa sasa? kwa maneno hayo nisingependa Precision air ife!!

Precision air wajifunze kwamba competition is stiff and many more new entrants in the market are there to come. Waboreshe huduma ili abiria wasiwakimbie. Kuna watu kulipa laki 4 sio tatizo kwao bora tu huduma iwe nzuri. All in all competition in the service industry is a good thing. So Viva FastJet

Precision Air wanaweza kuacha safari za Mwanza na Kia waweke nguvu zaidi mikoa ambayo FastJet hawezi kwenda.
 
Nilikuwa nafanya booking ya kwenda Bukoba Precision Air wananimbia return ticket Tsh 587,000!!!!

Kweli Precision wanatukomoa kama mazezeta. Hiyo Tsh 587,000 inazidi nauli ya kutoka London kwenda New York. Hivi hawa precsion air ndege zao zinatumia mafuta tofauti na wengine au? Kutoka London kwenda Barcelona ni £89, kwenda Cairo £112, Kwenda Roma £60, Kwenda Amsterdam £45. Kutoka DAR kwenda BK £230??? This is too much.
 
Tatizo watu humu ndani wanaleta ushabiki, matokeo yake wanaleta habari za uwongo kuhusu Fast jet.
I just paid for a return ticket for 2 persons na ime cost less than 500,000 pamoja na mzigo mmoja wa 20kg.
Nawashaurini mkakate fast jet ticket za Dec bado zipo. jinsi unavyochelewa ndio unapata bei kubwa.
 
Kiuchumi, serikali makini haiwezi kufanya hivyo. Wanaopanda ndege ni asilimia ndogo sana ya watanzania. Kodi inayokusanywa kwenye mafuta ya ndege ikitumika vizuri inafaidisha watanzania wengi zaidi kuliko hawa wanaotumia usafiri wa ndege. Kuondoa kodi kwenye mafuta ya ndege ni sawa na kuondoa ziwa mdomoni mwa kichanga na kumpa baba yake.

Hehehe hii nimeipenda!
 
Kweli Precision wanatukomoa kama mazezeta. Hiyo Tsh 587,000 inazidi nauli ya kutoka London kwenda New York. Hivi hawa precsion air ndege zao zinatumia mafuta tofauti na wengine au? Kutoka London kwenda Barcelona ni £89, kwenda Cairo £112, Kwenda Roma £60, Kwenda Amsterdam £45. Kutoka DAR kwenda BK £230??? This is too much.

Pengine Size ya ndege zao? (ndogo ndogo)

Au kwetu kodi za mafuta mzigo zinapandisha gharama? au gharamz a uwanja wa ndege?
 
Back
Top Bottom