Possible Intelligent Life out there

Haina shida. Nikipata nafasi nitatupia hapa hiyo kitu tuichambue.

Shukrani sana mkuu Mkuu Monstgala/Mgalanjuka
Kabla hatujaenda mbali ningependa nijue je tunapaswa kuiamini DRAKE'S EQUATION kwa 100%

.made in mby city.
 
Haina shida. Nikipata nafasi nitatupia hapa hiyo kitu tuichambue.

Shukrani sana mkuu Mkuu Monstgala/Mgalanjuka
Kabla hatujaenda mbali ningependa nijue je tunapaswa kuiamini DRAKE'S EQUATION kwa 100%

.made in mby city.
 
Mkuu Monstgala/Mgalanjuka nipo interested sana na hii elimu ya anga, kiufupi naipenda sana tangu nipo mdogo
Mkuu je naweza kusoma bachelor ya hii mambo?
Je ntasomea wapi?
Je ina dili kweli hii kitu au ndo nijiandae kuisoma kama hobie tu?
Kwasasa mimi ni mwanafunzi kidato cha sita PCM taker
Nategemea sana ushirikiano wako mkuu

.made in mby city.
 
Shukrani sana mkuu Mkuu Monstgala/Mgalanjuka
Kabla hatujaenda mbali ningependa nijue je tunapaswa kuiamini DRAKE'S EQUATION kwa 100%

.made in mby city.

Mkuu NICOLAX nasikikiaga sana hii kitu inaitwa DRAKE'S EQUATION hebu nipeni maujuzi kidogo na mm kabla hatujaenda mbali sana
Mkuu MONSTGALA uko wapi Mkuu?
 
Shukrani sana mkuu Mkuu Monstgala/Mgalanjuka
Kabla hatujaenda mbali ningependa nijue je tunapaswa kuiamini DRAKE'S EQUATION kwa 100%

.made in mby city.

100%? Aisee one thing you should know 100% is something that is not likely to be used in many scientific experiments as a result. Ni unrealistic, 100% ni kwamba katika hali yoyote matokeo yanayotarajiwa yatakuwa sawawasa bila kuwa na punje ya kasoro kitu ambacho ni rare.

Tukirudi kwenye Drake's equation sijui unajua kiasi gani lakini Drake equation ni hoja yenye probabilities. Katika parameters zinazounda equation hii, Drake ameweka makadirio mengi ambayo value zake hazina namba kamili bali range tu kutoka kiasi fulani mpaka kiasi fulani. Kwa hali hii huwezi kupata jibu ambalo litakuwa ni kamili bali litakuwa ni uwezekano tu na majibu mengi sana yanaweza pia kuwa matokeo ya kukokotoa equation hiyo. Hilo moja lakini pia equation yenyewe haikokotoleki kirahisi kwa maana parameters nyingi bado hazina majibu wala si rahisi kukadiria. Utaona bado hatujui kuna nyota ngapi zenye sayari katika Milkyway galaxy, hata average ya sayari zilinazoweza kusupport life katika galaxy yetu bado ni changamoto kujua kwa hakika lakini hata tukipata average na makadirio mengine ya parameters zote katika equation bado jibu la equation litakuwa too vague lakini at least liwe juu ya moja na si chini ya moja. Mfano kama N ambayo ni number of civilizations katika galaxy hii ni zaidi ya moja (+1), hii ina maana hatuko peke yetu. Lakini kama N ikiwa ni ndogo kuliko moja(-1) hii ina maana hakuna uwezekano wa kuwepo extra life katika galaxi hii, hivyo katika Milkyway lote na majinyota bilioni mia mbili kuna uhai katika Dunia tu.

Mfano rahisi kusaidia kumeza: Mtu mmoja mwanakijiji ana kuku wa blue peke yake anajaribu kujua kama kuna kuku wengine wa blue duniani. Parameters anazotumia ni kama ili kujua idadi ya kuku wa blue lazima ajue average ya wafugaji wote duniani, average wafugaji wenye kuku, sehemu ya kuku wenye uwezekano wa kutaga mayai yenye vifaranga wa blue, sehemu ya mazingira yanayopelekea kifaranga awe wa blue na labda muda wa unaotokana na yeye kupata habari hiyo kabla kuku hajachinjwa. Si mfano unaolingana lakini unaweza kupata picha ya equation hiyo ilivyo ngumu. Akiweka values ndogo za makadirio kwenye parameters zake atapata jibu negative kwamba chance za kuku wengine wa blue duniani hamna. Akiweka value kubwa kwenye makadirio yake katika parameter za equation atapata jibu kwamba kwamba kuna zaidi ya kuku mmoja wa blue. Jibu lolote linategemea values za parameters, bahati mbaya hana values hizo na ni mwanakijiji hana reseources za kufanya sensa ya wafugaji dunia nzima ili kupata angalau makadirio ya parameters zake. Kwa sasa kaangalia pale kijijini (Solar system) kaona hamna kuku wa blue wala mfugaji.

Ngumu zaidi ni kwamba Drake equation inaangazia intelligent life na sio just life maana inatakiwa viumbe wawe na uwezo wa kutuma signals au kufanya activity fulani ambayo vifaa vyetu vitaweza kudetect. Katika mifano hapo juu nimerahisisha tu lakini in reality life inayoangaliwa ni ile inayoweza kutuma ishara fulani ili sisi nasi tuzione tujue kuna wenzetu. Hapo utakutana na mambo magumu sana katika parameter za equation hii maana kuna suala la muda na uwezo wa kuwasiliana wa viumbe hao kama wapo. Lakini sio uwezo tu je wana interest ya kuwasiliana nasisi? Je kama mawasiliano yao ni tofauti sana na radio signals au any of which we have, how can we detect them? Au vipi kama ni mijidudu yenye kuwinda uhai mwingine katika galaxi hii na kuutokomeza alafu sisi hatujui tunatuma signals tu! Kwa hiyo hizo parameters nyingine mbili ambazo kwenye mfano wa kuku wa blue hazifit. Ni ngumu kuzikadiria lakini zipo na zinakadiriwa na tunakwenda mbele. SETI walichofanya na kuona uwezekano upo, kwa njia fulani lakini msingi ukiwa ni Drake's equation wakaona hebu tutume signals huko angani tusubiri majibu.

Drake equation haipo kutoa jibu lakini inajenga msingi na inafaa katika utafutaji wa maisha mengine katika galaxi, at least pa kuanzia. Kuna marekebisho pia maana wataalam wengine hawaoni baadhi ya vigezo muhimu na inakuwa si budi kuweka sawa au kuongeza baadhi ya parameters. Tunazungumzia galaxi moja tu (Milkyway) kwanza katika Drake kwa sababu ukiingiza next spiral galaxy kama Andromeda ugumu unakuwa maradufu. Ni kama yule mkulima hajafanya utafiti wa kuangalia kuku wa blue Duniani na anapanga kuangalia mwezini au vyote kwa pamoja. Sijui kama unanielewa mkuu, uliza tu kama hunipati.
 
Mkuu NICOLAX nasikikiaga sana hii kitu inaitwa DRAKE'S EQUATION hebu nipeni maujuzi kidogo na mm kabla hatujaenda mbali sana
Mkuu MONSTGALA uko wapi Mkuu?


armi nipo majukumu mengi, Lakini hebu ipitie kidogo hii na uangalie post hiyo nillomjibu Nicolax alafu twende mbele. Pia unaweza angalia vizuri wikipedia.
 
Last edited by a moderator:

Nadhani hailipi kwa Tanzania. Kama unadhani unaweza kujiendeleza katika vyuo vya Marekani, Ulaya au nchi nyingine zenye program hizi unaweza kujaribu. ningekushauri soma bachelor program inayoweza kukukwamua kiuchumi na ukiwa na kipato kizuri unaweza kujiendeleza katika fani hii baadae.
 

Ahsante mkuu kwa ushauri, naomba nikusumbue tena
Je naweza nikapata scholarship kutoka kwa baadhi ya ORGANISATION zinazo husiana na hizi mambo popote duniani ??

.made in mby city.
 
Mkuu Monstgala kuna mada hapa jukwaani ulikuwa unazungumzia kuhusu aliens na category zao!!!..
Kwa Bahati mbaya siioni Ile thread!!,
Vp uliidelete au umeihamisha ukumbi!!,
Kama umedelete naweza pata zile notice make!
Pole Kwa kuchukua muda wako!!!
 
Mkuu naomba unisahihishe!
Ninavyo amini mimi kuna hii kitu inaitwa Godlock zone hapa si ndipo uhai unapopatikana?
Kama ndivyo me nahisi kila sayari itakuja kuwa na uhai.
Kwa kuwa jua lina zivuta sayari zote kuja kuja kwake
Hivyo sayari zote zitapita kwenye Godlock zone.na zitakuwa na uhai.

Evidence
Mars kufanana kwakaribu kabisa na dunia,kwa kua she is next to Godlock zone.

NB:
Watu wengi wanasema mars ilikuwa kama dunia but me ninavyo hisi Mars inaelekea kuwa kama dunia na sio ilikuwa kama dunia.

Mkuu naomba unisahihishe tafadhari.
 
mkuu unaweza ukaniambia uhusiano wa muonekano wa constellation sagittarius na katikati ya milkwaygalaxy(black hole-)
 

Ni biblia au nn?
 
..Mkuu kwanza sio Godlock ni Goldilock,na ni kweli unachokisema kuwa hio zone inasupport Life but concept ya sayari kuvutwa towards the sun haina maana Ya kwamba we are moving miles closer to the sun tupo hapa hapo na tutabak hapa hapa since a GoldiLock zone Ina intervals no more life itakua created popote pale
 
Life ni condition ambayo inatokea pale mazingira fulani yanapokuwepo. Mazingira fulani ya kuruhusu uwepo wa uhai inaweza kuwa ndio chanzo cha uhai wenyewe. Na inafahamika maji na Oxygen zipo hata nje ya sayari yetu na sio elements pekee kwamba zipo duniani tu. Na dunia hapo zamani haikuwa na uhai na ilikuwa sayari isiyoweza kuishi uhai kutokana na mazingira yaliyokwepo then it makes sense.

Kama kuna billions of stars with billions of solar systems it can be possible kuwepo kwa another existence of life supported by its own environment na katika its own evolution depending on its environment and its adaptation.

Its just an assumption, hata anayesema hakuna uhai sehemu nyingine its just an assumption too.
 
mmh mambo makubwa haya.
 
kujiangaisha kote huko kwa wanadamu,na kuishughurisha akili kiasi kikubwa namna hiyo ni kwa7bu ya HOFU YA KIFO TUU...!!!...siachi kusema wanadamu tumepewa akili kwa ajili ya kudadisi na kujipambanulia mambo ktk mazingira tuishiyo......
mungu ni mkubwa.....

Sent from my HUAWEI G750-U10 using JamiiForums mobile app

 
Sory! HV wana anga wanapoenda ktk uchunguzi huko juu! Ndani ya kile chombo wanabeba na Misosi kama ugali,wali au pizza?????
 
Sory! HV wana anga wanapoenda ktk uchunguzi huko juu! Ndani ya kile chombo wanabeba na Misosi kama ugali,wali au pizza?????
Nadhani kutakuwa na vyakula vyao maalum mkuu
Wabebe ugali huo mda wa kwenda toilet kila saa wataupata wapi
 
Mkuu Monsstgala Uko wapi siku hizi, tunamiss sana madini yako.

Mm ni mmoja wa wale tuliokuwa tunakufuatilia tangu enzi hizo.

Rudi mkuu uje kuendelea kutupa madini ya aina hii
 
Mkuu Monsstgala Uko wapi siku hizi, tunamiss sana madini yako.

Mm ni mmoja wa wale tuliokuwa tunakufuatilia tangu enzi hizo.

Rudi mkuu uje kuendelea kutupa madini ya aina hii

Mkuu nimerudi, nashukuru sana. Napitia baadhi ya topics mpya za jukwaa hili nipate kuchangia lolote. Cheers..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ