Monstgala
JF-Expert Member
- Aug 25, 2009
- 1,079
- 1,034
Wakuu,
Nimepata maswali mengi sana kuhusu dhana ya viumbe anga za mbali. Baadhi nitayajibu hapa kadri ya uwezo wangu.
Utata:
Wana-anga na wanasayansi wamekuwa wakiangalia mienendo ya nyota, sayari, miezi na vitu vingine vilivyoko mbali nasi(outer space) na hata jirani na Dunia yetu au katika ya mfumo wa Jua (Solar system) ili kuhakiki kama kuna maisha kwa sasa, au kuliwahi kuwa na maisha kabla. Baadhi, kwa mazingira zilizonayo maisha tuyajuayo hayawezi kutokea, hamna hewa, hamna ardhi , joto ni kubwa sana au dogo kabisa etc. Lakini pia baadhi ya sayari na miezi (moons) zina ardhi, atmosphere, na aina fulani ya kiwango cha hewa ingawa si sawa na uwiano sawia na ule wa Dunia.
Mbali na kuangalia sayari pia kuna utafiti wa ku-trace signals from outer space kama SETI na science institutions nyingine zile za wazi na za siri wanavyofanya na sasa ni muda mrefu utafiti wa aina hii unaendelea. SETI wanabase katika Drake's equation kutambua ni nini kinahitajika katika kujua maisha katika anga za mbali. Mbinu nyinginezo nyingi zinatumika kutafuta alama au ishara fulani ambazo zinaweza kuwa ni either mawasiliano ya viumbe hawa wenyewe kwa wenyewe au labda pia wao kama wanatafuta kujua kama kuna wengineo kama jinsi sisi tunavyodhani.
Msingi
Na kama tujuavyo ni ukweli usio na shaka kwamba kuna nyota nyingi sana zinazofanana na jua letu katika maeneo mengine ya mbali sana kutoka sisi tulipo katika universe. Wanasayansi wanasema nyota zinazofanana na Jua letu ni kati ya asilimia tano hadi ishirini (5% - 20%) ya nyota zote katika Universe tunayoweza kuiona (observable universe). Hili neno la universe tunayoweza kuiona lina maana kwamba pale tusipoona basi kuna uwezekano universe inaendelea au kunavitu vingine tusivyovijua lakini makadirio yanayofanyika ni ya ulimwengu tunaoweza kuuona.
Sasa ukumbuke katika mada ile ya Ukweli wa kustaajabisha kuhusu Nyota, nilisema nyota zinakadiriwa kuwa sextillion 100 au zaidi katika ulimwengu tunaoweza kuuona sasa tukisema mfano tuchukue tu asilimia 5 yake, basi tutakuwa tunaongelea nyota bilioni-bilioni 500 zinafanana kimazingira (joto, ukubwa, umri, aina, uwepo wa sayari) na Jua.
Kwa hiyo basi kama kuna nyota zinazoshabihiana na Jua, na pia zina sayari zinazozizunguka tena baadhi ya sayari zina mazingira kama ya Dunia. Kwa probability na scientific evidence, sayari zinazofanana na jua ni lukuki hii inafanya pia uwezekano wa kuwepo Earth-like planet au sayari zifananazo na Dunia kuwa mkubwa. Kama kuna sayari nyingi zenye ardhi na zenye mazingira yanayofanana na dunia basi inakaribisha zaidi dhana ya kuwepo uhai sehemu nyingine katika ulimwengu.
Cha kushangaza:
Hamna ushahidi uliotangazwa "wazi" kuhusu kuonekana kwa viumbe wengine/uhai so far kutoka kwa institutions hizi, serikali za nchi au mamlaka nyinginezo. Lakini theoretical views, scientific projections, personal claims, and philosophical reviews zinaleta information nyingi tofauti kuhusu possible intelligent beings out there.
Wanaofikiri kuhusu dhana ya viumbe vingine nje ya sayari yetu hawatarajii sana kuwepo na binadamu wanaofanana na sisi, viumbe wa kawaida au uhai kama tunavyoujua. Ingawa hilo linawezekana lakini kumbuka kisayansi mazingira yanachangia sana mwonekano au matokeo ya viumbe. Kama mazingira yakiwa tofauti kidogo basi matokeo ya maisha au viumbe yatafuata mkondo. Hili tunaliona hata katika viumbe wa kawaida wa duniani jinsi wanavyokuwa na vigezo vinavyoendana na wao kumudu mazingira yao. Kwa kuwa hata hizi sayari zinazofanana na dunia haziwezi kuwa na mfanano pacha yani circumstance zile zile basi tusitegemee kukutana na viumbe wanaofanana asilimia mia na sisi. Jinsi kila kitu kinavyoonekana leo hii ni matokeo ya jinsi mazingira yalivyokuwa miaka milioni iliyopita na vivyo hivyo kadri muda unavyoenda.
Kuwa na akili zaidi yetu au kuwa na maendeleo na technology kubwa sana zaidi yetu hili ni wazi na lina sababu zake.
Kwanza kuna uwezekano wa utofauti wa maisha kuanza mapema au baadae hivyo kufanya viumbe wengine kama wapo basi wengine wanaweza kuwa wame-evolve zaidi yetu kwa kuwa na muda mrefu zaidi katika ulimwengu au vice-versa. Kama tukichukua mfano wa dunia yetu (Earth), maisha yanakadiriwa ku-evolve kutoka katika simple form kati ya miaka bilioni 3.5 iliyopita hii ni kutoka kwa evolutionists. Kuna sayari zilizo na muda mrefu zaidi ya dunia na hapa lazima utaona katika hali ya kawaida sisi ndo tunaanza na kuna wengine waliokwisha piga hatua kubwa sana. Na hata tukisema katika sayari nyingine kuna viumbe waliumbwa au walitokea mamilioni ya miaka kabla yetu alafu sasa tujilinganishe nao lazima watakuwa wametuzidi mbali.
Pili, kama kuna viumbe wataweza kufika katika sayari yetu basi hii ina maana technology inayowezesha kusafiri umbali huo si ya kawaida. Kuna umbali mrefu sana kati ya nyota moja na nyingine hasa zile ambazo haziko katika mfumo wa nyota panya au nyota kundi. Hata nyota iliyo jirani yetu si rahisi kuifikia kwa technolojia ya usafiri tuliyonayo sasa.
Kwa kuwa maswali yaliyoulizwa yamekuwa na uwigo tofauti basi ni vyema kuyajibia hapa kwa ujumla wake, pale nipatapo nafasi au mtu mwingine ajuaye achangie.
Karibuni
CC: juve2012 kadoda11 NICOLAX fyddell mtoto wa mjini neo1 Mjuni Lwambo Eiyer CYBERTEQ
Nimepata maswali mengi sana kuhusu dhana ya viumbe anga za mbali. Baadhi nitayajibu hapa kadri ya uwezo wangu.
Utata:
Wana-anga na wanasayansi wamekuwa wakiangalia mienendo ya nyota, sayari, miezi na vitu vingine vilivyoko mbali nasi(outer space) na hata jirani na Dunia yetu au katika ya mfumo wa Jua (Solar system) ili kuhakiki kama kuna maisha kwa sasa, au kuliwahi kuwa na maisha kabla. Baadhi, kwa mazingira zilizonayo maisha tuyajuayo hayawezi kutokea, hamna hewa, hamna ardhi , joto ni kubwa sana au dogo kabisa etc. Lakini pia baadhi ya sayari na miezi (moons) zina ardhi, atmosphere, na aina fulani ya kiwango cha hewa ingawa si sawa na uwiano sawia na ule wa Dunia.
Mbali na kuangalia sayari pia kuna utafiti wa ku-trace signals from outer space kama SETI na science institutions nyingine zile za wazi na za siri wanavyofanya na sasa ni muda mrefu utafiti wa aina hii unaendelea. SETI wanabase katika Drake's equation kutambua ni nini kinahitajika katika kujua maisha katika anga za mbali. Mbinu nyinginezo nyingi zinatumika kutafuta alama au ishara fulani ambazo zinaweza kuwa ni either mawasiliano ya viumbe hawa wenyewe kwa wenyewe au labda pia wao kama wanatafuta kujua kama kuna wengineo kama jinsi sisi tunavyodhani.
Msingi
Na kama tujuavyo ni ukweli usio na shaka kwamba kuna nyota nyingi sana zinazofanana na jua letu katika maeneo mengine ya mbali sana kutoka sisi tulipo katika universe. Wanasayansi wanasema nyota zinazofanana na Jua letu ni kati ya asilimia tano hadi ishirini (5% - 20%) ya nyota zote katika Universe tunayoweza kuiona (observable universe). Hili neno la universe tunayoweza kuiona lina maana kwamba pale tusipoona basi kuna uwezekano universe inaendelea au kunavitu vingine tusivyovijua lakini makadirio yanayofanyika ni ya ulimwengu tunaoweza kuuona.
Sasa ukumbuke katika mada ile ya Ukweli wa kustaajabisha kuhusu Nyota, nilisema nyota zinakadiriwa kuwa sextillion 100 au zaidi katika ulimwengu tunaoweza kuuona sasa tukisema mfano tuchukue tu asilimia 5 yake, basi tutakuwa tunaongelea nyota bilioni-bilioni 500 zinafanana kimazingira (joto, ukubwa, umri, aina, uwepo wa sayari) na Jua.
Kwa hiyo basi kama kuna nyota zinazoshabihiana na Jua, na pia zina sayari zinazozizunguka tena baadhi ya sayari zina mazingira kama ya Dunia. Kwa probability na scientific evidence, sayari zinazofanana na jua ni lukuki hii inafanya pia uwezekano wa kuwepo Earth-like planet au sayari zifananazo na Dunia kuwa mkubwa. Kama kuna sayari nyingi zenye ardhi na zenye mazingira yanayofanana na dunia basi inakaribisha zaidi dhana ya kuwepo uhai sehemu nyingine katika ulimwengu.
Cha kushangaza:
Hamna ushahidi uliotangazwa "wazi" kuhusu kuonekana kwa viumbe wengine/uhai so far kutoka kwa institutions hizi, serikali za nchi au mamlaka nyinginezo. Lakini theoretical views, scientific projections, personal claims, and philosophical reviews zinaleta information nyingi tofauti kuhusu possible intelligent beings out there.
Wanaofikiri kuhusu dhana ya viumbe vingine nje ya sayari yetu hawatarajii sana kuwepo na binadamu wanaofanana na sisi, viumbe wa kawaida au uhai kama tunavyoujua. Ingawa hilo linawezekana lakini kumbuka kisayansi mazingira yanachangia sana mwonekano au matokeo ya viumbe. Kama mazingira yakiwa tofauti kidogo basi matokeo ya maisha au viumbe yatafuata mkondo. Hili tunaliona hata katika viumbe wa kawaida wa duniani jinsi wanavyokuwa na vigezo vinavyoendana na wao kumudu mazingira yao. Kwa kuwa hata hizi sayari zinazofanana na dunia haziwezi kuwa na mfanano pacha yani circumstance zile zile basi tusitegemee kukutana na viumbe wanaofanana asilimia mia na sisi. Jinsi kila kitu kinavyoonekana leo hii ni matokeo ya jinsi mazingira yalivyokuwa miaka milioni iliyopita na vivyo hivyo kadri muda unavyoenda.
Kuwa na akili zaidi yetu au kuwa na maendeleo na technology kubwa sana zaidi yetu hili ni wazi na lina sababu zake.
Kwanza kuna uwezekano wa utofauti wa maisha kuanza mapema au baadae hivyo kufanya viumbe wengine kama wapo basi wengine wanaweza kuwa wame-evolve zaidi yetu kwa kuwa na muda mrefu zaidi katika ulimwengu au vice-versa. Kama tukichukua mfano wa dunia yetu (Earth), maisha yanakadiriwa ku-evolve kutoka katika simple form kati ya miaka bilioni 3.5 iliyopita hii ni kutoka kwa evolutionists. Kuna sayari zilizo na muda mrefu zaidi ya dunia na hapa lazima utaona katika hali ya kawaida sisi ndo tunaanza na kuna wengine waliokwisha piga hatua kubwa sana. Na hata tukisema katika sayari nyingine kuna viumbe waliumbwa au walitokea mamilioni ya miaka kabla yetu alafu sasa tujilinganishe nao lazima watakuwa wametuzidi mbali.
Pili, kama kuna viumbe wataweza kufika katika sayari yetu basi hii ina maana technology inayowezesha kusafiri umbali huo si ya kawaida. Kuna umbali mrefu sana kati ya nyota moja na nyingine hasa zile ambazo haziko katika mfumo wa nyota panya au nyota kundi. Hata nyota iliyo jirani yetu si rahisi kuifikia kwa technolojia ya usafiri tuliyonayo sasa.
Kwa kuwa maswali yaliyoulizwa yamekuwa na uwigo tofauti basi ni vyema kuyajibia hapa kwa ujumla wake, pale nipatapo nafasi au mtu mwingine ajuaye achangie.
Karibuni
CC: juve2012 kadoda11 NICOLAX fyddell mtoto wa mjini neo1 Mjuni Lwambo Eiyer CYBERTEQ