Possibles
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 1,898
- 2,335
Tangu lini chama kikaongoza bunge?Kigwangala hajui kuwa Bunge ni muhimili wa nchi?Kigwangala hajui kuwa hoja ya posho ilipitia katika vikao vyote halali vya bunge?Kigwangala hajui kuwa Bunge na wabunge wamewekwa na wanawajibika kwa wananchi?Kigwangala haelewi kuwa vikao halali vya bunge vikishahalalisha jambo la kidhalimu kama hilo na mbunge akaona hajapendezewa basi uamuzi mzuri ni kuwapeleka hoja yake kwa wananchi? Ina maana Kigwangala anafikiri NEC ina uwezo wa kubadili kilichoauliwa na Bunge?Sasa naanza kuamini kumbe hata mjadala wa katiba pia waliupitisha huku hawajui kuwa Bunge linapaswa kuwa kwa ajili ya kupitisha wanayoyataka wananchi. Nawaonea huruma wananchi wanaoongozwa na Kigwangala.