Posho ya madaraka kwa walimu

Posho ya madaraka kwa walimu

Kashi

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2013
Posts
897
Reaction score
747
Mwenye taarifa na hili ninaomba aliweke hapa jukwaani.Nimesikia kuanzia mwakani mwezi Julai Wakuu wa shule watalipwa Tshs 250,000 kwa mwezi kama posho,wakuu wa vyuo 300,000.

Waratibu elimu kata 250,000 na walimu wakuu msingi 200,000.Kama hili lina ukweli basi ni mwanzo mzuri wa kurejesha posho ya kufundishia kwa walimu wote.Tafadhali mwenye taarifa sahihi amwage hapa.
 
ndani ya ccm hakuna kitu kama hicho

Nasikia kuna waraka kabisa wa mwezi Oktoba kutoka Utumishi kuhusiana na hili ila nasikia wameweka vigezo kuwa anayestahili kulipwa ni Mkuu wa chuo mwenye masters au PGD,

Mkuu wa shule mwenye bachelor degree,mratibu elimu pia awe na bachelor degree na mwalimu mkuu awe na diploma.Kama ndio hivyo watakaolipwa ni wachache sana hivyo nadhani itawezekana.Wasiokuwa na sifa hizo kielimu wataendelea kushikilia madaraka bila posho.
 
Mwenye taarifa na hili ninaomba aliweke hapa jukwaani.Nimesikia kuanzia mwakani mwezi Julai Wakuu wa shule watalipwa Tshs 250,000 kwa mwezi kama posho,wakuu wa vyuo 300,000.

Waratibu elimu kata 250,000 na walimu wakuu msingi 200,000.Kama hili lina ukweli basi ni mwanzo mzuri wa kurejesha posho ya kufundishia kwa walimu wote.Tafadhali mwenye taarifa sahihi amwage hapa.

Mkuu walipwe kiwango hicho KILA MWEZI kwani siku hizi Walimu nao wamekuwa @wajumbe wa BUNGE la katiba (BMK)? Sahau....hizo ni ndoto za alinacha./ abunuasi ,

mkuu Kashi nakushauri ukimaliza kuota ndoto hiyo uamke na ukaoshe uso na kuangalia katuni ya "Junor Jumbo" hisabatiii...hisabatiiii.hisabati enheee...haeee..hae......hisabatiiiii.
 
Ndo mana mnaitwa walimu ni watu mliofeli.. Wanasambaza habari hizo ili muwasaidie ktk uchaguzi na nyie mlivo mabwege mshaanza kuamini..
Walimu bwana...........
 
Ni kweli kabisa ila kiwango cha posho hakijaainishwa wala ngazi ya elimu, mimi waraka nimeuona na nimeusoma.

Leo nimefanikiwa kuuona,viwango vya posho na ngazi za elimu vimeainishwa.Labda wewe uliona page moja.Nimeiona full package!
 
Ndo mana mnaitwa walimu ni watu mliofeli..
Wanasambaza habari hizo ili muwasaidie ktk uchaguzi na nyie mlivo mabwege mshaanza kuamini..
Walimu bwana...........

ulifeli wewe na ukoo wako
 
wekeni jamvini basi tuone, ikiwezekana tuanze kurogana mapema
 
Back
Top Bottom