Ningependa kuzungumzia kwa kirefu lengo la kichwa cha mada hii; lakini hiyo siyo dhumuni la haya machache nitakayo yaweka hapa.
Mashujaa, waTanzania wote, hasa vijana mliojitokeza maeneo yote ya nhi yetu kuandamana kupinga uhalifu uliofanyika; na baadhi yenu kupoteza maisha, nawapongeza kwa moyo safi kabisa kwa niaba ya waTanzania wote wapenda haki.
Kazi hii inaendelea, msikate tamaa.
Leo niseme tu kwamba waTanzania tumeipoteza nafasi muhimu kabisa ya kubadilisha hali hii inayo tukabili kwa sababu moja tu; ya kukosa uelewa kwa baadhi ya wengi miongoni mwetu.
Kilichotakiwa kufanyika ni kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano haya ili kazi iwe nyepesi kwa kila mmoja wetu.
Lakini nafasi hiyo tumeipoteza, na sasa italazimu tulipie gharama kubwa sana kwa kupambana na hawa waovu wanaolazimisha kututawala.
WaTanzania, sasa tunao uamzi kati ya mambo mawili:
Mosi, kwa ujumla wetu na umoja kati yetu tuendelee kukataa kwa nguvu zaidi kujisalimisha kwa hawa watu, kwa njia zote hadi wakubali kusalimu amri ili tuwawajibishe kwa maovu yao.
Au, sisi wenyewe kwa kushindwa kupata ushirikiano miongoni mwetu, tujisalimishe kwao, jambo ambalo wao wanalitarajia litokee.
Tukubali kuwa watawaliwa, ambao, watawala watakuwa na uhuru wa kufanya lolote wanalotaka juu yetu.
Wachache miongoni mwetu, kama akina Tundu Lissu; akina John Heche; viongozi mbalimbali wa dini wakionekana kuwa pingamizi, wachukuliwe mmoja mmoja na kutendewa watakavyo watawala ili kutuonyesha mfano wa kutawaliwa.
Hii ndiyo hali halisi tunayo iingia sasa hivi.
Ni juu yetu sasa kulipa gharama kubwa juu ya ujinga wa baadhi yetu ambao hawakuona ulazima wa kutoka ili tuwaondoe madarakani hawa waovu.
Naamini "mjinga" yeyote anao uwezo wa kuuondoa ujinga wake. Ndiyo maana naamini waTanzania wataachana na ujinga huu.
Mungu Ibariki Tanzania.
Mashujaa, waTanzania wote, hasa vijana mliojitokeza maeneo yote ya nhi yetu kuandamana kupinga uhalifu uliofanyika; na baadhi yenu kupoteza maisha, nawapongeza kwa moyo safi kabisa kwa niaba ya waTanzania wote wapenda haki.
Kazi hii inaendelea, msikate tamaa.
Leo niseme tu kwamba waTanzania tumeipoteza nafasi muhimu kabisa ya kubadilisha hali hii inayo tukabili kwa sababu moja tu; ya kukosa uelewa kwa baadhi ya wengi miongoni mwetu.
Kilichotakiwa kufanyika ni kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano haya ili kazi iwe nyepesi kwa kila mmoja wetu.
Lakini nafasi hiyo tumeipoteza, na sasa italazimu tulipie gharama kubwa sana kwa kupambana na hawa waovu wanaolazimisha kututawala.
WaTanzania, sasa tunao uamzi kati ya mambo mawili:
Mosi, kwa ujumla wetu na umoja kati yetu tuendelee kukataa kwa nguvu zaidi kujisalimisha kwa hawa watu, kwa njia zote hadi wakubali kusalimu amri ili tuwawajibishe kwa maovu yao.
Au, sisi wenyewe kwa kushindwa kupata ushirikiano miongoni mwetu, tujisalimishe kwao, jambo ambalo wao wanalitarajia litokee.
Tukubali kuwa watawaliwa, ambao, watawala watakuwa na uhuru wa kufanya lolote wanalotaka juu yetu.
Wachache miongoni mwetu, kama akina Tundu Lissu; akina John Heche; viongozi mbalimbali wa dini wakionekana kuwa pingamizi, wachukuliwe mmoja mmoja na kutendewa watakavyo watawala ili kutuonyesha mfano wa kutawaliwa.
Hii ndiyo hali halisi tunayo iingia sasa hivi.
Ni juu yetu sasa kulipa gharama kubwa juu ya ujinga wa baadhi yetu ambao hawakuona ulazima wa kutoka ili tuwaondoe madarakani hawa waovu.
Naamini "mjinga" yeyote anao uwezo wa kuuondoa ujinga wake. Ndiyo maana naamini waTanzania wataachana na ujinga huu.
Mungu Ibariki Tanzania.