Centrehalf
JF-Expert Member
- Jun 9, 2013
- 509
- 145
Wana Jf nimefurahishwa sana na tabia ya dr. Kitila Mkumbo,nimemfuatilia sana tangu zilipoibuliwa tuhuma dhidi yake pamoja na Zitto na Samson Mwigamba,amekuwa katika hali ya utulivu mkubwa kuliko watuhumiwa wenzie.
Maana baada ya kamati kuu kuwavua nyadhifa zao na kuwapa siku 14 dr amejitokeza mara mbili tu kwenye media kuzungumzia suala hilo.
Kutokana na sababu hiyo nimeanza kuamini kwamba maneno aliyosema kwenye kamati kuu kwamba aliingizwa tu kwenye mkenge na Zitto pamoja na Mwigamba ni ya kweli.
Nasema hivyo kwa sababu ukiangalia baada ya wote wa 3 kurudisha fomu zilizokuwa na mashtaka 11, dr. Mkumbo amekuwa kimya akisubiri hatma yake,tofauti na wenzie ambao wameendelea kuhangaika kwa kisngizio cha kupigania haki yao ndani ya chama hata kabla ya chama kutoa hitimisho.
Zitto Kabwe ndio huyo yuko Kigoma akiomba huruma ya wananchi,Mwigamba ndio huyo katia timu kwa msajili wa vyama.
Swali linakuja ni kwanini hawa wawili wanatafuta utetezi nje ya chama chao mapema?Na kwa nini dr. Mkumbo katulia akisubira maamuzi ya vikao vya chama?
Je ni kutofautiana kwa viwango vyao vya elimu ndio kulikowatofautisha?Hakika dr. Mkumbo umenikosha sana na ukimya wako hivyo kuthibitisha kwamba hakika ww ni msomi uliye elimika.
GUILTY ARE ALWAYS AFRAID.
Hongera sana dr. Mkumbo.
Nawasilisha.
Maana baada ya kamati kuu kuwavua nyadhifa zao na kuwapa siku 14 dr amejitokeza mara mbili tu kwenye media kuzungumzia suala hilo.
Kutokana na sababu hiyo nimeanza kuamini kwamba maneno aliyosema kwenye kamati kuu kwamba aliingizwa tu kwenye mkenge na Zitto pamoja na Mwigamba ni ya kweli.
Nasema hivyo kwa sababu ukiangalia baada ya wote wa 3 kurudisha fomu zilizokuwa na mashtaka 11, dr. Mkumbo amekuwa kimya akisubiri hatma yake,tofauti na wenzie ambao wameendelea kuhangaika kwa kisngizio cha kupigania haki yao ndani ya chama hata kabla ya chama kutoa hitimisho.
Zitto Kabwe ndio huyo yuko Kigoma akiomba huruma ya wananchi,Mwigamba ndio huyo katia timu kwa msajili wa vyama.
Swali linakuja ni kwanini hawa wawili wanatafuta utetezi nje ya chama chao mapema?Na kwa nini dr. Mkumbo katulia akisubira maamuzi ya vikao vya chama?
Je ni kutofautiana kwa viwango vyao vya elimu ndio kulikowatofautisha?Hakika dr. Mkumbo umenikosha sana na ukimya wako hivyo kuthibitisha kwamba hakika ww ni msomi uliye elimika.
GUILTY ARE ALWAYS AFRAID.
Hongera sana dr. Mkumbo.
Nawasilisha.