Ponda: Risasi ilinichanganya

Ponda: Risasi ilinichanganya

Status
Not open for further replies.
Hapo nimeelewa wenye akili wanatambua Ponda ni jembe


Yaani typical Msukule wa kiislam, sasa jembe la nini? Mtu GAIDI na hana faida kwa nchi wewe unamuita jembe au ni kwa vile alichanganikiwa baada ya kutunguliwa na hajafa, wewe unaona maajabu?
 
ponda gaidi mkubwa yule akitoka hospital mahakamani wangemuua tuu.
 
Jina lako na hoja vinafanana!
Unasema ponda ni hatari! Amekuwa yeye Ni Panga? Au silaha?
Midomo ya asiekuwa na elimu inanuka sana!
Unanikumbusha wakati nasoma! Tulikuwa tunachuma hizo@ntonga ! Halafu unainusa! Ikianza kunuka ujue haifai! Unaitupa mbali, na ile isio na harufu safi!
Lkn kwa maelezo yako wewe, wala nisingekuwa na haja ya kujua harufu yako! We mi ningetupa chooni tu!
Akili yako ya kushikiwa wewe endelea kufata mkumbo siku ya hukumu hata mungu atawashangaa mnakufa sababu ya ufuasi wa Ponda Mrundi.. hujasikia Ndugu zake boko haramu waliwakuta waislamu wenzie wanaswali swala ya asubuhi wakawamiminia risasi wote bado nyie mnaoamini kipofu awaongoze njia..
 
Sioni haja sana ya kuzungumzia kuhusu mtu ambaye hapo awali tuliiomba serikali imchukulie hatua kwa mihadhara yake ya uchochezi wa kidini tena ukizingatia hata Baba yake Mzee Issa alikimbia kwao kwa sababu ya vidomo domo hivyo hivyo, anakuja ugenini anafungulia domo la chuki kwa wananchi kwa mwavuli wa dini. None sense!!!
 
Picha linaendelea,nao wamepata mkanda wa ushahidi!let us wait

Inaelekea siku hizi watu wana record kila tukio kuweka ushahidi for future use. Daaaah...
Simu nazo zimekua nyingi sana aisee.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hakuna haki pasipo utii wa sheria! That's all
Wewe soma SOMA soma hapo juu kwanza afu kasoma magazeti la leo ,Mwananchi utaelewa yote !!

kuwa mvumilivu HAKI ipo na sote tunaitii sheria. na Shk. PONDA ni wa kwanza kutii sheria anafahamu yote.
 
Sioni haja sana ya kuzungumzia kuhusu mtu ambaye hapo awali tuliiomba serikali imchukulie hatua kwa mihadhara yake ya uchochezi wa kidini tena ukizingatia hata Baba yake Mzee Issa alikimbia kwao kwa sababu ya vidomo domo hivyo hivyo, anakuja ugenini anafungulia domo la chuki kwa wananchi kwa mwavuli wa dini. None sense!!!
Mkuu wetu,Mhe.wetu, mpendwa wetu mchana mwema ; HAPA issue sii uchochezi bwanaa. LaMuhimu hapa ni KUPIGWA RISASI mbele ya halaiki na umma wa watu waliyohudhuria uwanjani wakiwemo watoto wazee wanawake.... (forget about hatred au uchchezi huko Urrusi kuna wachochezi,wabaguzi,makatili huko Ulaya wapo,huko marekani wapo kila aina ya chuki juu ya wageni) mchana kweupee na kwa karibu (point blank) " JUST BE FAIR "
Mimi naamni wee ni msomi na mwenye busara katika weledi wa kijamii tafadhali speak the TRUTH and JUSTICE for the sack of huminity... good luck
 
ponda gaidi mkubwa yule akitoka hospital mahakamani wangemuua tuu.
Mpendwa vipi... You like killing?
Ahsante Oohh kuuwa kwako ndiyo ibadaa uliyofundishwa.... basi mtaua wengi !! humu wapo miloni 35 nza zaidi..!
Mzuri wewee basi nikupe somo ambalo hujalisikia walakulitafakari maishani mwako:-
Wenzio tukiuwawa bila hatia malazi yetu ni pepo ya juu AL-FERDOUS (paradisoo ndo nyumbani kwetu)
Nakusikitikia.
 
Akili yako ya kushikiwa wewe endelea kufata mkumbo siku ya hukumu hata mungu atawashangaa mnakufa sababu ya ufuasi wa Ponda Mrundi.. hujasikia Ndugu zake boko haramu waliwakuta waislamu wenzie wanaswali swala ya asubuhi wakawamiminia risasi wote bado nyie mnaoamini kipofu awaongoze njia..

We tukana kadri unavyoweza lkn umaarufu wa shekh ponda umemshinda kiongozi yyt wa upinzani kwa sasa! Na laiti huyu jamaa kesho akiingia kugombea! Atazikomba kura kama mchenzo!
Na wewe hilo li ntonga lako kichwani linatakiwa kufanyiwa service kabla hujatupa nguo!
 
Ipo siku ukishabikia unyama huu utakuja kuona mama yako anabakwa live na policcm

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Mama yako kwa uzuri upi? msikariri suala la ubakaji kwa vyombo vya usalama! tendo hilo huwahusisha zaidi waasi wanaoishi msituni kwa muda mrefu ndo wakivamia vijiji hubaka! polisi na wanawake wote hawa mtaani watafute mtu wambake? hizo huwa uzushi,
 
ponda_wife.jpg

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda akiwa na mkewe Hadija Ahamad alipomtembelea jana. Picha na Beatrice Moses na Venance Nestory



KWA UFUPI

  • Namshauri Rais (Jakaya Kikwete), kuhakikisha kwamba haki za wanyonge zinawafikia, asije akafikiri hili lililotokea kwa Sheikh Ponda ni suluhisho, ni vyema kufanya mazungumzo ili kuweka mabadiliko.


Dar es Salaam. Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amesema alichanganyikiwa kiasi cha kushindwa kujielewa kwa muda baada ya kupigwa risasi.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mwananchi kwenye wodi binafsi ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (Moi) alikolazwa jana, Sheikh Ponda alisema kutokana na hali hiyo hakumbuki matukio yaliyofuata baada ya hapo.

“Sikumbuki hata nilipata huduma ya kwanza hospitali gani kwa sababu sikuwa katika hali ya kawaida. Mambo mengine yaliyotendeka kabla ya kujeruhiwa ninayakumbuka vizuri,” alisema Ponda ambaye inasadikiwa kwamba alipigwa risasi ya begani, Ijumaa iliyopita mjini Morogoro.

Alisema alihutubia katika Kongamano la Waislamu kwa muda mfupi akizingatia muda uliokuwa umetolewa kumaliza mkutano huo na baada ya hapo alishuka na kupanda kwenye gari binafsi ambalo lilizingirwa na polisi ndipo akaamua kushuka na kuanza kutembea kabla ya kujeruhiwa.

Mahojiano maalumu na Sheikh Ponda

Swali: Je, watu waliokupa huduma ya kwanza mara baada ya kujeruhiwa walikuta risasi iliyokujeruhi?

Jibu: Nilipigwa risasi kwa nyuma ikatokea mbele kwa hiyo haikubaki mwilini wala haikuonekana ilipoangukia kwa wakati huo maana kulikuwa na purukushani.

Swali: Ulipata wapi huduma ya kwanza?

Jibu: Kwa kweli kwa sasa siwezi kukumbuka nilihudumiwa wapi kwa sababu mara baada ya kujeruhiwa sikuwa katika hali yangu ya kawaida, nilichanganyikiwa.

Swali: Utathibitisha vipi kama ulipigwa risasi?

Jibu: Bahati nzuri ni kwamba tukio hili lilitokea kweupe wapo wengi walioshuhudia, kwa hiyo wanaweza kusaidia kuthibitisha na ushahidi mwingine ni jeraha hili.

Swali: Nini msimamo wako baada ya tukio? Jibu: Nitaendelea kuzungumzia haki za Waislamu na siwezi kurudi nyuma. Pamoja na kwamba wananiona mimi ni mtu mchochezi lakini wanaeneza chuki dhidi yangu kwa njia wanazojua wao. Nitaendelea, risasi haitaninyamazisha.
Swali: Umehusishwa kufanya uchochezi Zanzibar, unalizungumzia vipi hilo?

Jibu: Zanzibar nilichozungumza ni kuhusu kesi dhidi ya viongozi wa Kundi la Uamsho. Watu wamewekwa ndani kwa miezi tisa sasa, kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, kesi wanayoshtakiwa ina dhamana, sasa nikauliza kwa hao viongozi, kwa nini hawazingatii sheria? Kesi zina muda mrefu hazitolewi uamuzi, nikawasisitiza wazingatie misingi ya sheria kwa kuwa hivyo wanavyowatendea wananchi wajue kwamba hawastahili kupewa tena ridhaa ya kuongoza nchi, nilifikisha ujumbe wangu.

Swali: Kuna tukio la kumwagiwa tindikali mabinti wawili wa Uingereza lililotokea Zanzibar, ambalo wewe pia unahusishwa, hili unalizungumziaje?

Jibu: Sijaona huo ushahidi ambao wanahangaika kunihusisha na tukio hilo, nahusishwa vipi? Matukio ya kumwagiwa tindikali yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara huko kabla sijakwenda kuhutubia. Vyombo vya dola vifanye kazi yake vyema ili kubaini ukweli wa jambo hili.

Pia Mwananchi ilizungumza na mke wake, Sheikh Ponda, Hadija Ahmad ambaye alikuwa ameketi pembeni ya kitanda alicholazwa mumewe.

Swali: Unazungumziaje tukio hili la kujeruhiwa kwa mumeo?

Jibu: Hili ni dhumuni la Serikali, lililenga moja kwa moja kumdhuru ili kunyamazisha harakati zake za kutetea wanyonge. Ni tukio la kupangwa, halijatokea bahati mbaya. Serikali inamfuatilia sana hivyo ililenga kumnyamazisha.

Namshauri Rais (Jakaya Kikwete), kuhakikisha kwamba haki za wanyonge zinawafikia, asije akafikiri hili lililotokea kwa Sheikh Ponda ni suluhisho, ni vyema kufanya mazungumzo ili kuweka mabadiliko.

Alivyowaponyoka polisi

Mtu wa karibu wa Sheikh Ponda alisimulia jinsi walivyomsafisha kiongozi huyo kutoka Morogoro hadi Dar es Salaam na kukwepa vizuizi vya polisi ambao walikuwa wakiendelea kumsaka. “Msafara ulikuwa na magari mawili. Moja lilitumika kwa uangalizi, lingine lilimbeba Sheikh Ponda. Tulipofika Chalinze tulikuta kizuizi tukakikwepa kwa kupitia Msata kisha Bagamoyo hadi Dar es Salaam na kumfikisha Muhimbili,” alisema.
Waigomea polisi

Msemaji wa familia ya Sheikh huyo, Isihaka Rashid alisema hawaitambui tume iliyoundwa na polisi kwa kuwa jeshi hilo ndilo linalotuhumiwa.

“Tunachofanya hivi sasa ni kukusanya ushahidi wetu, kwa bahati nzuri tayari tumepata mkanda wa tukio lenyewe ambao utatuwezesha kumbaini aliyemshambulia Sheikh Ponda.

“Hatuwezi kuhitaji majibu ya hiyo tume yao na hata leo kuna maofisa wa polisi kutoka Makao Makuu na Kituo cha Kati, Dar es Salaam walifika wakitaka kumhoji eti kuhusu uchochezi lakini alikataa kuzungumza hadi mwanasheria wake awepo, wakaondoka,” alisema Rashid.

chanzo. Ponda: Risasi ilinichanganya - Kitaifa - mwananchi.co.tz





 
Coincidence? Umechemka mkuu..sio lazima utumie kidhungu kama hujui mahali sahihi pa kutumia. Coincidence is when two or more similar or related events occur at the same time by chance and without any planning.

muelimishe
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom