Mawazo yako ni mazuri kaka. Tatizo ni vigezo gani hawa jamaa watavitumia kuwachagua hao vijana. Kuna uwezekano wakachagua kwa vigezo vitakavyohakikisha vijana wakiharakati hawaingii humo.
Si rahisi!
Kumbuka kuwa wengi wa Masheikh wa BAKWATA, Makatibu wa Wilaya, Mikoa, Makarani, waratibu wa BAKWATA ndio hao hao wajomba zetu, kaka zetu, shemeji zetu, jirani zetu, baba wakwe zetu,wengine tumesoma nao madrasah moja kwa Sheikh mmoja n.k
Tunakutana na kukaa nao chini tukazungumza misibani, maharusini au hata kwenye barza za kawaida tu.
Shushu yoyote atakayetoka nje ya jamii ya Waislamu mfano umlete shushu mwenye asili ya sumbawanga katika moja ya misikiti ya Singida mjini basi athari zake ni ndogo sana "hana meno" wala hatishi, kama hivi ndivyo wanavyokusudia basi sina wasiwasi, na nina hakika kuwa wanao mashushu wa namna hii na wanaona kuwa matokeo yake ni hafifu sana ndio maana wanawashirikisha BAKWATA waziwazi hivi sasa ili wawapate watu ndani ya jamii husika ya Waislamu.
Mfano,mtu mmoja alimfuata sheikh mmoja nchini (jina la Sheikh ninalihifadhi) akamwambia kuwa mimi ninataka kusilimu, alipoulizwa sababu zake za kutaka kusilimu akasema amevutiwa sana na Osama na al-qaeda.
Sheikh akamsilimisha na kuanza kumpa daawah kwa siku 4 mfululizo baada ya siku 4 na kuona kuwa hapati anachokitaka yule mtu akakimbia hakuonekana tena!...mashushu wa namna hawana athari zozote wala hawanisumbua kichwa changu!
Wamejileta wenyewe na pesa zao mkononi, hii ni zawadi adhimu na adimu sana kwa wanaharakati ni kujipanga tu.
*Hata hao BAKWATA wenyewe wengine unawaona hivi hivi macho yako yanakuonyesha kuwa huyu anahitaji "a gentle push" tu basi.