Pombe ina faida gani kwa Mlevi?

Pombe ina faida gani kwa Mlevi?

RAHA NA KARAHA BIA YA SITA!

Kwa wanywaji wazuri wa bia, chupa ya kwanza huwa haileti hisia yoyote. Mnywaji humaliza chupa hiyo bila kuona matokeo yoyote zaidi ya kupoza koo. Na mara nyingi huwa mkimya, pengine huwa anasoma gazeti lake au kwa siku hizi anawasiliana na ndugu na jamaa kupitia simu yake.

Baada ya kumaliza chupa ya pili kimsingi ndipo mazungumzo ya awali na wanywaji jirani huanza na haya huwa mazungumzo ya busara, yakihusu muelekeo wa ligi mbalimbali, siasa, idadi za ajali na kadhalika na wakati huu hata takwimu hutolewa zilizo sahihi.

Mtu anaweza kukutajia wachezaji wote wa ligi daraja la tatu la huko Ujerumani bila kukosea, hata idadi ya wagonjwa wa Ebola waliopona katika nchi ya Liberia. Ila wakati huu kama unaanzisha mashindano ya kucheua ni wakati mzuri kwani bia ya pili huongeza hisia za kucheua.

Bia ya tatu huanza kumfanya mnywaji aanze kusikia furaha na pia huu huwa wakati ambapo karanga na korosho huliwa sana. Pamoja na mazungumzo kuhusu mpira na siasa, ghafla mazungumzo kuhusu michepuko huanza kujitokeza.

Bia ya nne huanza kusababisha masikio yaanze kupoteza nguvu za kusikia kwani utaona mnywaji ghafla amepandisha sauti, na ukijumlisha na kuwa baa zetu huwa na muziki una kelele utadhani waliopo wote wana matatizo ya kusikia, bia hii humsaidia kuongea kwa nguvu kushindana na kelele za muziki.

Bia ya tano ni hatari kidogo kwani ukiinuka kwenda chooni mara nyingi unarudi hujafunga zipu, na kipindi hiki ni kibaya kwa wanywaji wa kike maana unaweza kumkuta akienda chooni akijiangalia kwenye kioo anaanza kulia peke yake na kulalamika; ‘Mi sipendwi mpaka leo sijaolewa’ au ‘ Mume wangu sijui yukoje hanijali’

Japokuwa lazima isemwe ukweli ukifikisha bia hii, maisha ni raha sana unaweza ukaanzisha shoo ya kukata mauno katikati ya baa na kudai wewe ni mkali kuliko Shilole.

Kuanzia bia ya sita na kuendelea, chochote utakachosema au kufanya ni wazi kesho yake asubuhi utajilaumu sana. Kuna watu husema ukilewa ndipo unakuwa mkweli, hivyo basi wakati huu hata bosi wako akitokeza unamueleza ukweli jinsi alivyo ---- na hajui kuendesha kampuni.

Au unasema ukweli jinsi unavyompenda mke wa jirani yako ambaye mmekaa mnakunywa naye. Kimsingi uwezekano wa kutapika pia upo karibu na kama umekaa na mchumba wako huu ni muda ambao pia uchumba unaweza kuvunjika.

Maskini mbavu zanguuuu
 
Vikao hivi vina faida nyie acheni tu. Huku utaelekezwa shule nzuri kumpeleka mwanao, jambo la kufanya kama una kesi mahakamani, fundi ujenzi mzuri na hata mahali pa kupata kiwanja kwa bei poa. Afu kwa ujumla unaburudika...
Kweli kabisa
 
Faida ya kulewa ni kuongea kingereza fluent bila kukosea. Pombe zikiisha na english inayeyuka
 
Pombe ni kinywaji (alcohol) cha aina yoyote ambacho kikinywewa, kinabadili utaratibu mzima wa kazi ya ubongo wa kati (akili) na mwili kwa ujumla. Au kinywaji chochote chenye vilevi.
Madhara ya pombe hutegemea kiasi mtu alichokunywa, mazoea ya kunywa pombe, afya ya mnywaji pombe, jinsi gani ya kunywa pombe (inanywewa haraka haraka au taratibu na wakati mtumiaji alikula nini kabla).Kutokana na hali hiyo, matokeo kwa watu wanaokunywa pombe hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.

Kwanini watu wanakunywa pombe?
Tafiti ndogo niliyoifanya inasema kuwa, baadhi ya watu wanajiingiza katika matumizi ya pombe kwa lengo la kutaka kujiunga na jamii inayowazunguka, jambo ambalo halina ulazima kwani upo uwezekano wa kujumuika na jamii inayokuzunguka bila kutumia pombe.
Wengine wanakunywa ili kukwepa matatizo waliyonayo kwa muda (stress), huku wengine wakinywa kutokana na upweke walionao katika maisha yao. Aidha wapo wanaokunywa ili kujihisi vizuri wakichukulia kama mtindo wao wa maisha huku wengine wakisukumwa na marafiki wao ambao ni wanywaji wa pombe ili wote wafanane katika mtindo huo wa ulevi.

Ulevi ni ugonjwa (unywaji pombe ni hatari)
Ulevi sugu (ALCOHOLISM) ni ugonjwa kama ulivyo ugonjwa wa Ukimwi, kisukari, magonjwa ya moyo, kansa, nk
Pombe inapimwa kama yanavyopimwa magonjwa mengine kwa kutumia vipimo mbalimbali ikiwemo kipimo cha damu.

Unaitwa ugonjwa kwa sababu zipo dalili pekee, kuwa na madhara ya ndani na nje ya mwili kama yalivyo magonjwa mengine. Mtu anayetumia pombe anapatiwa matibabu hospitali, au nyumba salama (sober house, rehab) na wala hakuna matibabu ya miti shamba. Pia mtu anayekunywa pombe anaweza kufa kwa haraka au kufa taratibu (LIFESPAN) kuliko mtu asiyetumia pombe.
Mtumiaji hawezi kuona madhara ya pombe moja kwa moja kwa sababu hana nguvu ya kushinda pombe kwani imetawala mwili wake na imekuwa sehemu ya mwili wake, ndiyo maana wengi wanaona kiu kali ya pombe. Baadhi ya watu wanaokunywa pombe wanathamini sana pombe kuliko hata chakula kwani wanaweza kuacha chakula kimetengwa na kuambatana na rafiki zao kwenda kunywa pombe, (ADDICTION).

Mtu wa aina hiyo anahitaji msaada wa haraka (RECOVERY PROGRAM FROM ALCOHOLISM) ili kumrudisha katika hali ya kawaida. Kabla ya kupewa huduma yoyote, mhusika anatakiwa kwanza kujikubali pamoja na kukubali (ACCEPTANCE) kuwa madhara anayoyapata katika maisha yake yanachangiwa na yeye kunywa pombe.
Iwapo atapata ushauri kutoka kwa watoa huduma hospitali pamoja na watu wa saikolojia (ADDICTION COUNSELOR) ataweza kujikubali na kugundua kuwa pombe anayokunywa ndiyo inamletea shida katika maisha yake.

Madhara ya ulevi
Kukosa raha; Mtu akisha lewa huwa hana raha yoyote kwani hata akilala hujisikia kizunguzungu, huweza kutapika na hata kukosa hamu ya kula chakula. Afya yake hupungua kwani anapoteza vyakula vingi. Maumivu makali hutokea sehemu za mbavu na kifuani na tumboni kwa kuwa misuli huwa haina nguvu kutokana na kuchoshwa wakati wa kutapika.

Ufukara; Mlevi husahau kununua mahitaji ya nyumbani ikiwemo nguo, chakula, vyombo na vinginevyo kwani fedha nyingi hutumika katika unywaji. Watoto hukosa chakula bora na hii huleta madhara mengi katika familia. Mtu akishiriki ulevi hawezi kufanya kazi yoyote, anakuwa mvivu na mzembe.

Ugomvi; Kutokana na kulewa watu hupigana na hata kuumizana. Watu wa namna hii hawaheshimiani kwani huwa hawana siri mbele ya watoto na ni aibu kubwa kwa wageni na watu wote. Mlevi hupenda kuharibu na hata kugawa vitu alivyonavyo hata vile ambavyo ni vya familia hivyo husababisha ufukara nyumbani.

Ajali; Mlevi hupoteza akili na hata hajisikii kama ameumizwa vibaya. Haoni sawasawa na mwendo wake hubadilika. Vilevile anaweza kushindwa kabisa kutembea akalala popote barabarani au porini. Ajali nyingi hutokea kama kukanyagwa na gari, pikipiki na kusababisha vilema vya ukubwani, kuumwa na wadudu wakali kama nyoka na nge.

Ugonjwa; Ukimwi, Kaswende, Kisonono, na mengine ya kuambukiza ni magonjwa ambayo mlevi anaweza kuyapata kwa urahisi kutokana na kufanya vitendo visivyofaa katika jamii pale anapokuwa amelewa. Anayefanya vitendo hivyo ni pombe sio yeye.

Kukosa kuzaa; Ukishiriki Ulevi, sehemu nyingi za mwili hulegea sana hasa sehemu za viungo vya uzazi, kwani viungo huwa havina nguvu tena na mapato yake ni kuwa tasa.

Uzembe; Mtu mlevi huwa mzembe, hulewa tu kusahau na hata kudharau kazi yake. Mapato yake ni kufukuzwa kazi au kuachishwa kazi. Miradi yake husimama.

Kukosa afya; Pombe kama inazidi katika damu hufanya kazi ya kudhoofisha mwili. Watu wengi wakilewa hupoteza nguvu zao, hawapendi kula au wanakula kidogo sana. Pia hawapati chakula bora ikiwa fedha nyingi hutumika katika ulevi. Udhaifu wa mwili nao unaweza kusababisha magonjwa mengine ikiwemo kifua kikuu.

Matatizo ya moyo; Hii ni shida kubwa ambayo inahitaji muda mwingi kukaa hospitalini ili kupata nafuu, wakati huo miguu na mikono huvimba pamoja na kupata matatizo katika mfumo wa upumuaji.

Figo; Hushindwa kufanya kazi yake sababu mara nyingi huchoshwa na sumu ya pombe huku maini yakishindwa kufanya kazi ipasavyo kutokana na kuzidiwa na kiwango kikubwa cha sumu kitokanacho na pombe, (TOXIC). Pia tumbo huvimba na kutokana na hatua hii maisha huwa ni mafupi sana. Kulewa kunaifanya mishipa ya fahamu kuharibika, kuumwa mwili wote na kukosa raha kabisa. Aidha pombe inaweza kusababisha upofu wa macho ambao hutokea baada ya mishipa ya macho kuharibika kwa kuwa haiwezi tena kupeleka mionzi inayofanya mtu kuona.

By: Nelson R +255 789 78 05 29
Email: rnelsontz@yahoo.com
 

faida zake ni [1] umaskini [2] figo maini kwisha [3] na mwisho mauti,,,
:hatari:,,​

Heri yako wewe utakufa ukiwa tajiri na figo na maini vyote vikiwa katika hali nzuri:confused2::confused2::confused2:
 
Asilimia kubwa ya walevi baada ya pombe kuisha kichwani,hujuta na kusema sinywi tena na leo ndiyo mwisho.
 
Asilimia kubwa ya walevi baada ya pombe kuisha kichwani,hujuta na kusema sinywi tena na leo ndiyo mwisho.

aaaah as for me
 

Attachments

  • 1430496243591.jpg
    1430496243591.jpg
    82.7 KB · Views: 91
We shika adabu yako !!!
Kwani ulevi sio faida?
We ulitegemea nini? Pesa au wanawake?
 
Jamani kwa wale walevi hivi mkinywa pombe mnapata faida gani? Kuna pombe kama GONGO,BIA,WHISKY,KONYAGI. VIROBA nk. hivi mkinywa hizi pombe zaidi ya kupoteza pesa,kulala nje ya nyumba, kutopeleka matumizi nyumbani, ni faida gani ambayo anaipata mlevi?

Wale wataalam wa hii fani waje watujuze

Futa kauli ya kuita wanywaji ni walevi! Ulevi upo wa aina nyingi, hata kupenda sana ni ulevi!
 
Back
Top Bottom