Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 990
SOURCE: JIBU LA MAISHA
DATE: Sunday, May 12, 2013
ISSN: 1821-6463, No. 241
PAGE: 115
HEADLINE: ASKOFU PENGO AZIDI KUTISHIWA
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Kwa matoleo kadhaa ya nyuma tumeripoti matukio ya kichochezi ya kusambazwa kwa CD na DVD zinazochochea utengano baina ya wakristo na waislamu nchini. Tumefanya hivyo kwa tahadhari kubwa na hata wakati mwingine kujitahidi kujiepusha na kuchapisha habari hizo.
Hata hivyo, tunalazimika kuripoti matukio haya ili kuzikumbusha mamlaka zenye dhamana zichukue hatua kali dhidi ya makundi haya ambayo yanaonekana moja kwa moja ni maadui wa umoja wa watanzania.
Katika kile kinachoonekana nia utaratibu maalumu, imetolewa CD mpya iliyopewa jina Ndege wote walie akilia bundi uchuro ambay pamoja na mambo mengine inaonyesha picha ya Askofu Kardinal Polycarp Pengo ikiwa na maandishi yanayosomeka WANTED ikiambatana na maneno makali ya kulaani Kanisa Katoliki na hata mengine, huku picha ya mtu anayechinjwa ikitumika kama logo inayojirejea kila wakati.
Juhudi za kumpata mtu anayeonekana katika DVD hiyo akitajwa kama Imam Hamza Omary, ili kufafanua ujumbe uliopo ndani ya mkanda huo hazikfanikiwa.
DVD hiyo ambayo JIBU LA MAISHA lina nakala yake inaonyesha mhadhiri akinukuu aya za Kuran na kuwaalika wenzake kwenye kile alichokiita Jihad (baadhi ya yale yanayosemwa hatuwezi kuyaandika kutokana na sababu za kimaadili)
Katika hilo Imam Omary anasema serikali imekuwa ikiegemea upande wa maaskofu na mabaraza yake, lakini si kwa waislamu.
Mkanda huo umeonyesha baadhi ya mazoezi makali ya vijana wa Kiislamu ingawa haionyeshi yanafanyika wapi.
Mhubiri huyo aliyashutumu pia mataifa ya kimagharibi akidai yamekuwa yakitoa silaha na kuwagombanisha wao kwa wao pasipo wenyewe kujua na hilo limeonekana kwa Saddam Hussein.
Aidha alionekana akidai kuwa jambo kubwa na la hatari kwa waislam wa sasa ni kutoongelea kabisa suala la Jihad, na hilo limekuwa donda ndugu.
Bila kupepesa maneno, Imam huyo alitaja viongozi ambao alidai eti wamekuwa wakibadili yale waliyokubaliana na waislam na wamekwenda kinyume kutokana na kutiwa msukosuko.
Vingozi na wasaniasa wanaotajwa katika DVD hiyo ni pamoja na Waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe, Katibu Mstaafu wa CCM, Yusufu Makamba, na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Alipomaliza hilo alimgeukiwa Rais wa Uganda, Museveni na kudai yeye ni kiongozi wa Afrika Mashariki anayetaka kuhakikisha anaungoa uislam kupitia mashehe kwa juhudi zote.
Aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow, anatajwa kwenye mkanda huo, lakini JIBU LA MAISHA halitaongelea kilichoongelewa humo.
Yusuf Makamba ambaye ni muislam, wanadai naye mwaka 1998 akiwa Mkuu wa Mkoa Dar, wakati wao wakisema nchi inatawaliwa kwa mfumo Kristo, yeye alipinga na hilo likaonekana kuwa yuko kinyume na uislam.
Mwinjilisti Cecil Simbaulanga ambaye amekuwa akipita huku na kule kutetea wakristo ili wajue haki zao anatajwa kuwasisitiza wakristo kuchinja nyama wakati inajulikana siku zote kwamba waislamu ndiyo wenye kufanya jambo hilo hapa Tanzania.
.
Wakati hayo yakitokea, tukio la kurushwa bomu katika Kanisa la Parish of St. Joseph the Worker (Olasiti), mkoani Arusha, linarandana na maudhui ya kile kinachoelezwa kwenye mikanda kadhaa inayotolewa na watu wanaoaminika kuwa na imani kali ikionyesha chuki ya wazi dhidi na kanisa hilo.
Ndani ya DVD kadhaa zenye mlengo mmoja ambazo zimezagaa maeneo kadhaa jijini Dar, hasa maeneo ya Buguruni_Chama, inaelezwa kukamatwa kukamatwa kwa maaskofu ili kuwachinja ikiwa muislam atafanyiwa ubaya wowote au kuuliwa.
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
DATE: Sunday, May 12, 2013
ISSN: 1821-6463, No. 241
PAGE: 115
HEADLINE: ASKOFU PENGO AZIDI KUTISHIWA
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Kwa matoleo kadhaa ya nyuma tumeripoti matukio ya kichochezi ya kusambazwa kwa CD na DVD zinazochochea utengano baina ya wakristo na waislamu nchini. Tumefanya hivyo kwa tahadhari kubwa na hata wakati mwingine kujitahidi kujiepusha na kuchapisha habari hizo.
Hata hivyo, tunalazimika kuripoti matukio haya ili kuzikumbusha mamlaka zenye dhamana zichukue hatua kali dhidi ya makundi haya ambayo yanaonekana moja kwa moja ni maadui wa umoja wa watanzania.
Katika kile kinachoonekana nia utaratibu maalumu, imetolewa CD mpya iliyopewa jina Ndege wote walie akilia bundi uchuro ambay pamoja na mambo mengine inaonyesha picha ya Askofu Kardinal Polycarp Pengo ikiwa na maandishi yanayosomeka WANTED ikiambatana na maneno makali ya kulaani Kanisa Katoliki na hata mengine, huku picha ya mtu anayechinjwa ikitumika kama logo inayojirejea kila wakati.
Juhudi za kumpata mtu anayeonekana katika DVD hiyo akitajwa kama Imam Hamza Omary, ili kufafanua ujumbe uliopo ndani ya mkanda huo hazikfanikiwa.
DVD hiyo ambayo JIBU LA MAISHA lina nakala yake inaonyesha mhadhiri akinukuu aya za Kuran na kuwaalika wenzake kwenye kile alichokiita Jihad (baadhi ya yale yanayosemwa hatuwezi kuyaandika kutokana na sababu za kimaadili)
Katika hilo Imam Omary anasema serikali imekuwa ikiegemea upande wa maaskofu na mabaraza yake, lakini si kwa waislamu.
Mkanda huo umeonyesha baadhi ya mazoezi makali ya vijana wa Kiislamu ingawa haionyeshi yanafanyika wapi.
Mhubiri huyo aliyashutumu pia mataifa ya kimagharibi akidai yamekuwa yakitoa silaha na kuwagombanisha wao kwa wao pasipo wenyewe kujua na hilo limeonekana kwa Saddam Hussein.
Aidha alionekana akidai kuwa jambo kubwa na la hatari kwa waislam wa sasa ni kutoongelea kabisa suala la Jihad, na hilo limekuwa donda ndugu.
Bila kupepesa maneno, Imam huyo alitaja viongozi ambao alidai eti wamekuwa wakibadili yale waliyokubaliana na waislam na wamekwenda kinyume kutokana na kutiwa msukosuko.
Vingozi na wasaniasa wanaotajwa katika DVD hiyo ni pamoja na Waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe, Katibu Mstaafu wa CCM, Yusufu Makamba, na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Alipomaliza hilo alimgeukiwa Rais wa Uganda, Museveni na kudai yeye ni kiongozi wa Afrika Mashariki anayetaka kuhakikisha anaungoa uislam kupitia mashehe kwa juhudi zote.
Aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow, anatajwa kwenye mkanda huo, lakini JIBU LA MAISHA halitaongelea kilichoongelewa humo.
Yusuf Makamba ambaye ni muislam, wanadai naye mwaka 1998 akiwa Mkuu wa Mkoa Dar, wakati wao wakisema nchi inatawaliwa kwa mfumo Kristo, yeye alipinga na hilo likaonekana kuwa yuko kinyume na uislam.
Mwinjilisti Cecil Simbaulanga ambaye amekuwa akipita huku na kule kutetea wakristo ili wajue haki zao anatajwa kuwasisitiza wakristo kuchinja nyama wakati inajulikana siku zote kwamba waislamu ndiyo wenye kufanya jambo hilo hapa Tanzania.
.
Wakati hayo yakitokea, tukio la kurushwa bomu katika Kanisa la Parish of St. Joseph the Worker (Olasiti), mkoani Arusha, linarandana na maudhui ya kile kinachoelezwa kwenye mikanda kadhaa inayotolewa na watu wanaoaminika kuwa na imani kali ikionyesha chuki ya wazi dhidi na kanisa hilo.
Ndani ya DVD kadhaa zenye mlengo mmoja ambazo zimezagaa maeneo kadhaa jijini Dar, hasa maeneo ya Buguruni_Chama, inaelezwa kukamatwa kukamatwa kwa maaskofu ili kuwachinja ikiwa muislam atafanyiwa ubaya wowote au kuuliwa.
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -