Polisi yakana kumkamata Salum Mwalimu, yadai alijipeleka mwenyewe ili akamatwe

87aa0f2e6ae05ba4eb9d6f5cdd0b977c.jpg
Kamanda wa Polisi wilaya ya Kinondoni, Jumanne Muliro amesema mgombea ubunge wa CHADEMA jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu hakukamatwa na Polisi, bali alijipeleka mwenyewe ili akamatwe wakati si mtuhumiwa.

Akizungumza na MCL Digital leo Frebuari 17, 2018, Kamanda Muliro amesema mgombea huyo alijipeleka mwenyewe kwenye gari la Polisi wakati si mtuhumiwa, akiamini kuwa kitendo hicho kitawafanya waandishi wa habari kumpiga picha ili ionekane kuwa amekamatwa.

"Hizi ni hadithi za abunuwasi. Haya mambo ya kufikirika hayatakiwi kabisa. Yeye ameshapiga kura akae asubiri matokeo", amasema Muliro.

"Amelazimisha kuchukuliwa na kuingia kwenye gari wakati si mtuhumiwa".

Timu ya waandishi wa habari ilishuhudia leo saa 6 mchana, Mwalimu akiondoka na Polisi katika Defender na kupelekwa katika kituo cha Magomeni ambapo alikaa kwa takribani robo saa na kuachiwa.

Mwalimu alifika katika kituo hicho baada ya kusikia taarifa za baadhi ya wananchi wa kata hiyo wakidai kuwa kuna mtu ameondoka na sanduku lenye kura, baadaye kukamatwa na Polisi akiwa na sanduku hilo.

Chanzo: Mwananchi
We are now living in a fully fledged Police State. Hatuna tofauti na Uganda Wakati wa Iddi Amin.

Hata ushahidi wa video clips wanaona ni uongo.
 
Polisi walimkwida na kumpeleka kwenye gari tena aliyemkwida ni askRi mwenye nyota
Hawa watu waache comedy

Ova
 
polisisii+pic.jpg


Kwa picha hapa juu, Salum amekamatwa au amejikamata?

Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi wilaya ya Kinondoni, Jumanne Muliro amesema mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu hakukamatwa na Polisi, bali alijipeleka mwenyewe ili akamatwe wakati si mtuhumiwa.

Akizungumza na MCL Digital leo Februari 17, 2018, Kamanda Muliro amesema mgombea huyo alijipeleka mwenyewe kwenye gari la polisi wakati si mtuhumiwa, akiamini kuwa kitendo hicho kitawafanya waandishi wa habari kumpiga picha ili ionekane kuwa amekamatwa.

“Hizi ni hadithi za abunuwasi. Hayo mambo ya kufikirika hayatakiwi kabisa. Yeye ameshapiga kura akae asubiri matokeo,” amesema Murilo.

“Amelazimisha kuchukuliwa na kuingia kwenye gari wakati si mtuhumiwa.”

Timu ya waandishi wa habari ilishuhudia leo saa 6 mchana, Mwalimu akiondoka na Polisi katika defender na kupelekwa katika kituo cha Magomeni ambapo alikaa kwa takribani robo saa na kuachiwa.

Mwalimu alifika katika kituo hicho baada ya kusikia taarifa za baadhi ya wananchi wa kata hiyo wakidai kuwa kuna mtu ametoroka na sanduku lenye kura, baadaye kukamatwa na polisi akiwa na sanduku hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka polisi, “Nilipata taarifa za kuibwa kwa sanduku hilo na nilifika eneo la tukio na kuzungumza na wakala wa Chadema, msimamizi wa uchaguzi na polisi ambao wote walikiri kuwepo kwa tukio hilo.”

“Waliniambia nijaze fomu namba 16 na kisha niondoke kwa maelezo kuwa polisi wamemkamata mtu huyo. Nikasema hilo suala haliwezekani kabisa. Wakati naendelea kuzungumza nao polisi walinichukua.”

Amesema alipofika kituo cha Magomeni alikaa kwa muda mfupi na kuachiwa huku akibainisha kuwa uchaguzi huo umekuwa na kasoro nyingi.

“Kile kituo cha Idrisa nimekikataa, yaani sikifahamu kabisa maana ushahidi upo wazi wote wamekiri sanduku kuibwa, nikitoka hapa naelekea tena huko,” amesema Mwalimu.
 
Duh Nina Mashaka ama sipo Tanzania au ninaota katikati ya usingizi mzito. Nakupenda Nchi yangu, bora iwe ndoto niamke niendelee na kulainisha vyuma
 
polisisii+pic.jpg


Kwa picha hapa juu, Salum amekamatwa au amejikamata?

Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi wilaya ya Kinondoni, Jumanne Muliro amesema mgombea ubunge wa Chadema jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu hakukamatwa na Polisi, bali alijipeleka mwenyewe ili akamatwe wakati si mtuhumiwa.

Akizungumza na MCL Digital leo Februari 17, 2018, Kamanda Muliro amesema mgombea huyo alijipeleka mwenyewe kwenye gari la polisi wakati si mtuhumiwa, akiamini kuwa kitendo hicho kitawafanya waandishi wa habari kumpiga picha ili ionekane kuwa amekamatwa.

“Hizi ni hadithi za abunuwasi. Hayo mambo ya kufikirika hayatakiwi kabisa. Yeye ameshapiga kura akae asubiri matokeo,” amesema Murilo.

“Amelazimisha kuchukuliwa na kuingia kwenye gari wakati si mtuhumiwa.”

Timu ya waandishi wa habari ilishuhudia leo saa 6 mchana, Mwalimu akiondoka na Polisi katika defender na kupelekwa katika kituo cha Magomeni ambapo alikaa kwa takribani robo saa na kuachiwa.

Mwalimu alifika katika kituo hicho baada ya kusikia taarifa za baadhi ya wananchi wa kata hiyo wakidai kuwa kuna mtu ametoroka na sanduku lenye kura, baadaye kukamatwa na polisi akiwa na sanduku hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka polisi, “Nilipata taarifa za kuibwa kwa sanduku hilo na nilifika eneo la tukio na kuzungumza na wakala wa Chadema, msimamizi wa uchaguzi na polisi ambao wote walikiri kuwepo kwa tukio hilo.”

“Waliniambia nijaze fomu namba 16 na kisha niondoke kwa maelezo kuwa polisi wamemkamata mtu huyo. Nikasema hilo suala haliwezekani kabisa. Wakati naendelea kuzungumza nao polisi walinichukua.”

Amesema alipofika kituo cha Magomeni alikaa kwa muda mfupi na kuachiwa huku akibainisha kuwa uchaguzi huo umekuwa na kasoro nyingi.

“Kile kituo cha Idrisa nimekikataa, yaani sikifahamu kabisa maana ushahidi upo wazi wote wamekiri sanduku kuibwa, nikitoka hapa naelekea tena huko,” amesema Mwalimu.
Chadema ilijengwa na Mbowe + Slaa, Mnyika, Zitto, Lissu na inabomolewa na Mbowe + Lowassa, Msigwa, Lema, Mashinji!!
 
Eti alijipeleka mwenyewe! Kwanini wasimwambie aondoke na badala yake wakaamua kumbeba hadi kituoni. Hivi huyu kamanda aliyetoa maelezo haya ni yule shahidi aliyezawadiwa mvua ya maswali na Lissu pale Kisutu kortini au huyu ni mwingine? Huyu kamanda naye atakuwa ni miongoni mwa wale wenye vyeti feki.
 
Alipojipeleka kwenye gari ''kuuza sura'' kwanini police hawakumfukuza na badala yake wakasepa nae? Hekaya hizi..
 
Salum Mwalimu mgombea wa CHADEMA akielezea kupitia kituo cha television cha ITV live/mubashara jinsi alivyotiwa nguvuni na polisi wakati akifuatilia tukio la sanduku la kura kuporwa na watu wasiojulikana

 
Nilifikiri sisi waafrika tutahitaji miaka 100 kufikia ustaarabu wa watu weupe; hapana nafikiri itakuwa zaidi ya miaka 500 ijayo (kizazi cha tano toka leo) maana tuyafanyayo leo wenzetu waliyapitua. Karne ya 15. (Mwaka 1500)

Tunayoyafanya yanatia aibu.
100 ni kidogo aise
 
TBC : " ITV matatani baada ya mkurugenzi wa uchaguzi NEC kuhoji taarifa zilizorushwa na ITV za sanduku la kura kuporwa mtaa wa Idrissa kitongoji cha Magomeni jimbo la Kinondoni Dar-es-Salaam bila kupata idhidi ya NEC/TUME au msimamizi wa kituo husika"

 
Huenda bangi inayokamatwa na maasikari huwa wanaiweka stoo kwa matumizi yao,maana kuna mambo mengine hata wao wanaona aibu kuyazungumza mbele za watu
 
Hawa ndio polisi wetu. Yaani ka kwidwa na mkuu wa kituo halafu RPC anasema kajipeleka mwenyewe. We need to evaluate our police officers
 
Back
Top Bottom