Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,845
Ulishawahi kupata tatizo na ukahitaji msaada wa polisi? Au ulishwahi kufika kwenye kituo chochote cha polisi kwasababu zozote zile na ukaona jinsi huduma zinavyotolewa kwa matabaka na upendeleo wa wazu kabisa?
Kama huna hela kituo cha polisi huna thamani yeyote, lugha inayozungumzika pale ni lugha ya pesa, rushwa na hongo za wazi kabisa hakuna kificho, hasa kama kesi yako inahusiana na pesa nyingi aidha kuibiwa/ kutapeliwa au kutarajiwa kulipwa utaambiwa tu wazi kuwa kupata huduma ya namna hiyo ni lazima uwe na kiasi Fulani mfano halisi ni kupata nyaraka kwa ajili ya kwenda kulipwa bima ishu inayohusu ajali
Tunaweza kuwalaumu polisi wetu lakini tatizo ni la kimfumo zaidi, hatukuwa na matabaka zamani kila huduma ilikuwa inatolewa kwa jumuiya nzima, lakini siku hizi mambo ni tofauti huduma muhimu za kijamii zina matabaka hospital zipo za kulipia na zipo za serikali, shule na vyuo kuna matabaka mahoteli mpaka sehemu za starehe, japo si wazi sana lakini pesa yako ndio itakubagua tuu, utaenda unapomudu.
Bahati mbaya sana sana matabaka yote hayo yanakuja kukutana sehemu moja yanapotokea matatizo ya kipolisi na kisheria. Ni polisi pekee wameshindwa kuwa na vituo kulingana na bei ya mtu hivyo mtu wa being fulani aliyezoea kupata huduma ya daraja la kwanza alifika polisi hupata shida na hivyo kuamua kutumia pesa kupata huduma anayostahili.
Na polisi wetu kwakuwa nao ni binadamu na nje ya mavazi yao rasmi ya kazi wana changamoto za kawaida kabisa za kibinamu huangukia kwenye mtego huu kwa urahisi kabisa na kujikuta wanatoa huduma kwa macho ya makengeza, ni mfumo ndio umewajenga.
Kama huna hela kituo cha polisi huna thamani yeyote, lugha inayozungumzika pale ni lugha ya pesa, rushwa na hongo za wazi kabisa hakuna kificho, hasa kama kesi yako inahusiana na pesa nyingi aidha kuibiwa/ kutapeliwa au kutarajiwa kulipwa utaambiwa tu wazi kuwa kupata huduma ya namna hiyo ni lazima uwe na kiasi Fulani mfano halisi ni kupata nyaraka kwa ajili ya kwenda kulipwa bima ishu inayohusu ajali
Tunaweza kuwalaumu polisi wetu lakini tatizo ni la kimfumo zaidi, hatukuwa na matabaka zamani kila huduma ilikuwa inatolewa kwa jumuiya nzima, lakini siku hizi mambo ni tofauti huduma muhimu za kijamii zina matabaka hospital zipo za kulipia na zipo za serikali, shule na vyuo kuna matabaka mahoteli mpaka sehemu za starehe, japo si wazi sana lakini pesa yako ndio itakubagua tuu, utaenda unapomudu.
Bahati mbaya sana sana matabaka yote hayo yanakuja kukutana sehemu moja yanapotokea matatizo ya kipolisi na kisheria. Ni polisi pekee wameshindwa kuwa na vituo kulingana na bei ya mtu hivyo mtu wa being fulani aliyezoea kupata huduma ya daraja la kwanza alifika polisi hupata shida na hivyo kuamua kutumia pesa kupata huduma anayostahili.
Na polisi wetu kwakuwa nao ni binadamu na nje ya mavazi yao rasmi ya kazi wana changamoto za kawaida kabisa za kibinamu huangukia kwenye mtego huu kwa urahisi kabisa na kujikuta wanatoa huduma kwa macho ya makengeza, ni mfumo ndio umewajenga.