LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,497
- 3,388
Kauli ya PM!
Piga tu! Pig tumechoka! Uawa! Na ndiyo inaendelea kwa matendo sasa!
Piga tu! Pig tumechoka! Uawa! Na ndiyo inaendelea kwa matendo sasa!
Usitetee uovu wa polisi wewe.
Polisi risasi siku hizi wanapiga risasi ovyo hata sehemu isipohitajika kufanya hivyo.
inaweza kuwa ni hoja, lkn si yenye mashiko. tatizo kubwa tulilonalo, tunapenda kuwapeleka watuhumiwa wa uhalifu polisi kama kuwahifadhi. hakuna anayejitokeza kudai kafanyiwa uhalifu, hakuna aliyetayari kutoa ushahidi mahakamani na hakuna anayefuatilia kujua mtuhumiwa aliyefikishwa kituo cha polisi ana kesi gani ya kujibu. tunachokosea, tukiwafikisha kituoni, tayari tunajua tumeshamaliza kila kitu.
mara nyingi polisi huabika mahakamani, pale hakim anapohitaji kumwona mlalamikaji dhidi ya mtuhumiwa. akikosekana mlalamikaji, mtuhumiwa hana kesi ya kujibu, hivyo anaachiwa huru, anarudi kitaa.
Hii haijaanza leo, ipo tangu enzi na enzi, ndio maana huwa nakataa hoja ya kuwa wananchi wamepoteza imani na wananchi, ni hoja ambayo ukiichambua haina ukweli wowote.
mimi niliwahi kumpeleka mwizi wangu polisi na vidhibiti vilikuwepo kabisa kilichotokea tukaishia kupigwa tarehe kila mara mpaka tukachoka huku mwizi akiwa na mawasiliano ya karibu sana na huyo polisi. tukienda tunaambiwa mwizi kapata matatizo atakuja siku ingine. Kifupi mwizi aligeuka kuwa bosi wa polisi na sisi walalamikaji. nikaona muda wangu unazidi kupotea tukaachana nao. Inaonekana polisi wanajua kuwa watu hawako tayari kupoteza muda wao hivyo huanzisha mazingira ya kuzungusha mpka mlalamikaji anachoka.
kwani wananchi hawana silaha hizo? si polisi kila siku wanauwawa kwa risasi? halafu chukulia wako polisi wawili, ndio wanataka kuokoa maisha ya mtu anayetuhumiwa kufanya kosa, lakini wananchi wanaotaka kuua mtuhumiwa wapo 20 hadi 50. polisi atachukua mawe mangapi kukabiliana na watu 50? tumia akili wewe
unasema unayoyajua au unasema ili mradi tu umesema? kidhana wanatakiwa kuwa na vifaa vyote mhimu vya kujilinda lkn ukweli uliopo vifaa vilivyopo ni vichache ndio maana tunawaona wanafanya kazi wakiwa hawajavivaa. hata leo ukikatizza mtaani, utawakuta wanapiga kazi bila vifaa hivyo. nimekutana nao wengi tu.
Halafu hata kama una vifaa vya kujilinda, mwananchi anapokabiliana na wewe, lengo lake unalijua? tujifunze kuheshim kazi za watu wengine, la sivyo sote tutalia. polisi watalia na raia tutalia
Polisi hana mamlaka ya kuua. Ndiyo maana nchi za wenzetu polisi akiua huwa uchunguzi kuhakiki. Haki huwa inatendeka. Kwa Tanzania hii kitu haipo. Ndiyo maana polisi wanakuwa na mabomu ya machozi, au "hand grenade" za kujilindia. Hizi "hand grenade" huwa maalumu sanasana zinajeruhi tu.
Leo hii ukishikwa na polisi ukataka kutoroka atakulima risasi ya mgongoni. Wakati anapaswa kutumia nguvu kukudhibiti na ikishindikana, kama una silaha, anapaswa kukulima risasi ya mguu, mkono, au popote ILA ASIKUUE.
Polisi kutokuvaa vifaa vya kazi yake nani alaumiwe? Mwananchi? Unadhani ni kwanini Polisi wa Tanzania si watu wema? Zamani tulikuwa tunakimbilia polisi. Siku hizi, ukishitaki polisi ishu ambayo ni ya hatari, wanaenda kumwambia muhusika, au akikamatwa anaachiwa.
Leo hii Polisi wakifanya msako nyumbani kwako, lazima watakuta "bangi" japokuwa wewe si mshiriki wa hiyo kitu. Sasa jiulize hiyo "bangi" imetoka wapi?
Polisi wenyewe wa kuwaamini sio hawa.
Polisi kutokuvaa vifaa vya kazi yake nani alaumiwe? Mwananchi? Unadhani ni kwanini Polisi wa Tanzania si watu wema? Zamani tulikuwa tunakimbilia polisi. Siku hizi, ukishitaki polisi ishu ambayo ni ya hatari, wanaenda kumwambia muhusika, au akikamatwa anaachiwa.
Leo hii Polisi wakifanya msako nyumbani kwako, lazima watakuta "bangi" japokuwa wewe si mshiriki wa hiyo kitu. Sasa jiulize hiyo "bangi" imetoka wapi?
ww una akili kweli mtuhumiwa yuko mikononi mwa polisi ww unataka umwadhibu?. Safi sana polisi
kwani we kwa mtazamo wako unadhani polisi analenga kuua? lengo ni kukudhibiti usitoroke, sasa katika kukudhibiti, risasi inaweza kupita sehem siyo. mfano, polisi analenga miguu, lkn wkt risasi inatoka, anayekimbia akawa anataka kudesh down, risasi badala ya mguu hupitia kichwa.
Lakini kwa mtu anayejitambua, kwa nini uanze kufukuzana na polisi? jambo gani halimaliziki jamani tanzania hii? Liyumba si huyo kashinda kesi? woga wako kifo chako. kwa msataarabu yeyote hawezi kujaribu kutoroka polisi ili hali amesha wekwa chini ya ulinzi, kujaribu kufanya hivyo inaashiria nia yako si njema.
Ashakum si matusi, nadhani ntamaholo unahitaji shule ya "balistic science"...
Risasi iliyofyatuliwa kutoka kwenye AK47 inachukua "dakika" ngapi kufikia kusudio (target) umbali wa mita 300-400? (Mwendokasi wa AK47 ni 710 mita kwa sekunde).
Maelezo yako hayana mashiko!
umefanya utafiti lkn? zamani hata wakiua hakuna aliyekuwa anawahoji, ni mara chache sana, lkn siku hizi kila mtu mwandishi wa habari ukifanya lolote tayari limerushwa hewani. polisi naamini wako makini zaidi ukilinganisha na zaman